"Tazama, naja kama mwivi. Heri akeshaye, na kuyatunza mavazi yake, asiende uchi hata watu wakaione aibu yake...ufunuo 16:15"

Thursday, September 15, 2016

MIAKA 7 YA NEEMA


ujumbe aliopewa dada Nnenna wa Nigeria  na Bwana Yesu Kristo kwa kanisa duniani kote. katika ujumbe huu aliambiwa kanisa limepewa miaka saba ya neema(ya kumrudia Mungu). ambayo ilianza disemba 2014 na itaenda kuisha disemba 2021,katika kipindi hichi hapa katikati Bwana alimwambia atafanya kila namna kuwavuta watu wake kutoka katika madhehebu,dini,upagani n,k na kuwaleta katika nuru ya kweli ya ukristo, kanisa tukufu na katika ufunuo huo Bwana pia alimwambia baada ya hiyo miaka 7 kuisha jambo lolote linaweza kutokea, Na pia alimwambia katika wakati huu wa mwisho Bwana ana kitu cha kufanya na bara la Afrika, alimweleza pia matetemeko ya ardhi tuliyoyazoea kuyaona nchi za Asia sasa yanakuja Afrika ndani ya  kipindi cha mwaka 2016/2017. aliambiwa na mambo mengine mengi, tazama video na uyafahamu haya...

na unabii huu ni kweli kwani tumeshaanza kuona matetemeko makubwa ya ardhi kutokea hata katika nchi yetu ya tanzania na kuleta maafa makubwa na vifo vya watu.

je! swali tujiulize ni wakati gani huu tunaishi??? 
tuamke, muda umeenda kuliko tunavyodhani.

KRISTO YUPO MLANGONI KURUDI!!!!

No comments:

Post a Comment