"Tazama, naja kama mwivi. Heri akeshaye, na kuyatunza mavazi yake, asiende uchi hata watu wakaione aibu yake...ufunuo 16:15"

Monday, January 22, 2018

MAELEZO JUU YA UFUNUO 22:

Bwana wetu YESU KRISTO apewe sifa, Karibu katika mfululizo wa mwendelezo wa kitabu cha ufunuo leo tukiwa katika sura ya 22 na ya mwisho, Tusome..

    Mlango 22

1 Kisha akanionyesha MTO WA MAJI YA UZIMA, wenye kung'aa kama bilauri, ukitoka katika kiti cha enzi cha Mungu, na cha Mwana-Kondoo,
2 katikati ya njia kuu yake. Na upande huu na upande huu wa ule mto, ulikuwapo MTI WA UZIMA, uzaao matunda, aina kumi na mbili, wenye kutoa matunda yake kila mwezi; na majani ya mti huo ni ya kuwaponya mataifa.
3 Wala hapatakuwa na laana yo yote tena. Na kiti cha enzi cha Mungu na cha Mwana-Kondoo kitakuwamo ndani yake. Na watumwa wake watamtumikia;
4 nao watamwona uso wake, na jina lake litakuwa katika vipaji vya nyuso zao.
5 Wala hapatakuwa na usiku tena; wala hawana haja ya taa wala ya nuru ya jua; kwa kuwa Bwana Mungu huwatia nuru, nao watatawala hata milele na milele.
6 Kisha akaniambia, Maneno haya ni amini na kweli. Naye Bwana, Mungu wa roho za manabii, alimtuma malaika wake kuwaonyesha watumwa wake mambo ambayo hayana budi kuwako upesi.

Tukirejea kidogo kwenye historia ya Edeni, tunafahamu kuwa katikati ya Bustani, kulikuwa na ule mti wa uzima, na pia kulikuwa na mto kando ya mti wa uzima ambao ulikuwa unaitilia bustani yote maji, na kisha baada ya hapo uligawanyika na kuwa vichwa 4 (Mwanzo 2),ambavyo vilikwenda kuimwagilia dunia yote. Hivyo tunajua kuwa ule mti wa uzima, haukuwa mti kama mti wa matunda ya asili kama vile zabibu au peasi, la! bali ulikuwa ni mti wa rohoni, ambao matunda yake mtu akila anapata uzima wa milele, vyakula vya mwilini haviwezi kumpa mtu uzima wa milele, ukisoma kwa makini pale utaona Mungu alichepusha miti ya aina tatu: wa kwanza ulikuwa ni kila mti unaotamanika kwa macho na kufaa kwa kuliwa(haya ndio matunda ya asili kama vile zabibu, embe, tufaa, n.k.)..aina ya pili ni mti wa uzima, na aina ya tatu ni mti wa ujuzi wa mema na mabaya,(Mwanzo 2:9), sasa hii miti aina 2 za mwisho ni miti ya rohoni.

Hivyo ule "mti wa uzima" ulikuwa ni NENO LA MUNGU ambao ndio baadaye ulikuja kuuvaa mwili ukaitwa YESU KRISTO, Sasa hili NENO LA MUNGU ndilo lililokuwa sheria na maagizo yote ambayo Adamu na Hawa walipewa na Mungu ili wakidumu katika hayo waishi milele. Hivyo pale Edeni Adamu na Hawa walikula matunda ya kawaida ya asili pamoja na maji ya asili kuwapa uzima miili yao, lakini pia walikula chakula cha rohoni (Matunda ya mti wa uzima), na maji ya rohoni, kuwapa uzima katika roho zao.

Lakini baada ya Adamu kuasi(kukaidi sheria ya MUNGU) tunaona njia ya mti wa uzima ilifungwa(kumbuka mti wenyewe haukuondolewa), ilipofika wakati uliokusudiwa ile njia ilifunguliwa tena, na tunajua huyu si mwingine zaidi ya BWANA wetu YESU KRISTO, Yohana 14:6"Yesu akamwambia, Mimi ndimi NJIA, na kweli, na UZIMA; mtu haji kwa Baba, ila kwa njia ya mimi. "
Hivyo YESU KRISTO ni NENO/maagizo yale yale ya Mungu yaliyouvaa mwili.

Yeye ndiye ule mti wa uzima, na pia ndio anayetoa yale maji ya uzima.
 
 ukisoma Yohana 4:14"
13 Yesu akajibu, akamwambia, Kila anywaye maji haya ataona kiu tena;
14 walakini ye yote atakayekunywa MAJI YALE nitakayompa mimi hataona kiu milele; bali yale maji nitakayompa yatakuwa ndani yake chemchemi ya maji, yakibubujikia UZIMA WA MILELE. "
 
Sasa tukirudi juu, katika kitabu cha UFUNUO, tunasoma..
 
1 Kisha akanionyesha mto wa maji ya uzima, wenye kung'aa kama bilauri, ukitoka katika kiti cha enzi cha Mungu, na cha Mwana-Kondoo,
2 katikati ya njia kuu yake. Na upande huu na upande huu wa ule mto, ulikuwapo MTI WA UZIMA, uzaao matunda, aina kumi na mbili, wenye kutoa matunda yake kila mwezi; na majani ya mti huo ni ya kuwaponya mataifa.

Hapa tunaona mto wa maji ya uzima unaonekana ukitoka katika kiti cha enzi cha Mungu, na cha mwanakondoo, kumbuka kama tulivyosoma katika sura iliyopita kwamba katika ile Yerusalemu mpya(ambayo ni BIBI-ARUSI) ndipo patakapokuwa makao ya Mungu(Ufunuo 21:3-4"Nami nikauona mji ule mtakatifu, Yerusalemu mpya, ukishuka kutoka mbinguni kwa Mungu, umewekwa tayari, kama bibi-arusi aliyekwisha kupambwa kwa mumewe. Nikasikia sauti kubwa kutoka katika kile kiti cha enzi ikisema, TAZAMA, MASKANI YA MUNGU NI PAMOJA NA WANADAMU, naye atafanya maskani yake pamoja nao, nao watakuwa watu wake. Naye Mungu mwenyewe atakuwa pamoja nao. ), hivyo kiti chake cha enzi cha Mungu kitakuwepo huko, Na MTI wa UZIMA pamoja na mto wa maji wa uzima utatokea huko.

Kwahiyo bibi-arusi wa Kristo ambaye ndo ile Yerusalemu mpya na ndio watu wale wote watakaoshinda kutoka katika nyakati mbalimbali za Kanisa, Kama Bwana Yesu alivyoahidi katika Ufunuo 2:7 "Yeye aliye na sikio, na alisikie neno hili ambalo Roho ayaambia makanisa. Yeye ashindaye, nitampa kula matunda ya mti wa uzima, ulio katika bustani ya Mungu. "
Hii Ikiwa na maana kuwa wale watakaoshinda tu ndio watakula mema yote na kuzishiriki baraka zote ambazo Mungu alimwahidia YESU KRISTO atakapokuja kuumiliki ulimwengu, Yaani kwa lugha rahisi hawa watu watakatifu watafanana na YESU KRISTO mwenyewe. Kwa kuwa maisha yao walipokuwa hapa duniani yalifanana sana na mwana wa Mungu, hivyo watavuna walichokipanda kwa kula matunda yake.(yaani matunda ya mti wa uzima-YESU KRISTO mwenyewe.)

Lakini pia majani yatakuwa ni ya kuwaponya mataifa, kama tunavyofahamu mti wowote wa matunda, kwa mfano mti wa mwembe, huwezi ukala majani, ukasema, huu mwembe ni mzuri pengine yanaweza kukusaidia kama dawa ukiyatwanga, au kuongeza tu virutubisho fulani mwilini, lakini anayekula EMBE ndie anayejua uzuri wa mwembe, Vivyo hivyo kwa YESU KRISTO yeye kama mti wa UZIMA matunda yake watakayoyafurahia aliyopewa na BABA yake ni BIBI-ARUSI tu, wengine wote watamfahamu YESU katika sehemu ya matawi yake, kama biblia inavyosema yatakuwa ni kwa ajili ya kuwaponya tu, waendelee kuishi milele, lakini BIBI-ARUSI atakuwa na vyote.

Kama ilivyokuwa katika bustani ya Edeni mto ulitoka katika bustani na kusambaa duniani kote, vivyo hivyo na huu mto utokao katika kiti cha Enzi cha mwanakondoo katika ile YERUSALEMU MPYA, maji yake yatasambaa ulimwenguni kote kuwanywesha mataifa, ikiwa na maana kuwa yale maji ya uzima ambayo chanzo chake ni YESU KRISTO, kwa kupitia bibi-arusi wake, yataenea duniani kote kwa kufandisha mataifa kanuni zote za Mungu na utukufu wake.

Hivyo hawa watu ambao wanaaunda huu mji Yerusalemu mpya, watakuwa wametawanyika duniani kote . Unaona uzuri wa kuwa bibi-arusi wa Kristo? Kama dunia ya leo ni wasomi tu, ndio wanaotoa mwongozo wa mataifa ya dunia na kupewa kipaumbele, vivyo hivyo na kule ni BIBI-ARUSI tu, ndiye atakayetawala na KRISTO, na litakuwa ni kundi dogo, ni kwa wale watakaoshinda tu!

Tukiendelea..

Ufunuo 22:7-21 
"7 Na tazama, naja upesi; heri yeye ayashikaye maneno ya unabii wa kitabu hiki.
8 Nami Yohana ndimi niliyeyasikia na kuyaona mambo hayo. Na hapo nilipoyasikia na kuyaona nalianguka, ili nisujudu mbele ya miguu ya malaika yule mwenye kunionyesha hayo.
9 Naye akaniambia, Angalia, usifanye hivi; mimi ni mjoli wako, na wa ndugu zako manabii, na wa wale wayashikao maneno ya kitabu hiki. Msujudie Mungu.
10 Akaniambia, Usiyatie muhuri maneno ya unabii wa kitabu hiki, kwa maana wakati huo umekaribia.
11 Mwenye kudhulumu na azidi kudhulumu; na mwenye uchafu na azidi kuwa mchafu; na mwenye haki na azidi kufanya haki; na mtakatifu na azidi kutakaswa.
12 Tazama, naja upesi, na ujira wangu u pamoja nami, kumlipa kila mtu kama kazi yake ilivyo.
13 Mimi ni Alfa na Omega, mwanzo na mwisho, wa kwanza na wa mwisho.
14 Heri wazifuao nguo zao, wawe na amri kuuendea huo mti wa uzima, na kuingia mjini kwa milango yake.

Ndugu hapa Bwana anatoa angalizo, Hili neno "TAZAMA NAJA UPESI" ..na thawabu yangu ipo mkononi mwangu kumlipa kila mtu kama kazi yake ilivyo, Linaonyesha kwamba wakati umeisha, je! wewe kazi yako ni ipi?, je! umeipima thawabu yako?, je! unastahili kuitwa bibi-arusi ?, je! kazi yako inakupeleka mbinguni au kuzimu?.
 
maana hapa anaendelea kusema...

15 Huko nje wako mbwa, na wachawi, na wazinzi, na wauaji, na hao waabuduo sanamu, na kila mtu apendaye uongo na kuufanya.
16 Mimi Yesu nimemtuma malaika wangu kuwashuhudia ninyi mambo hayo katika makanisa. Mimi ndimi niliye Shina na Mzao wa Daudi, ile nyota yenye kung'aa ya asubuhi.
17 Na "ROHO na BIBI-ARUSI" wasema, NJOO! Naye asikiaye na aseme, NJOO! Naye mwenye kiu na aje; na yeye atakaye, na ayatwae maji ya uzima bure.

Huu ni wakati wako wewe mkristo uliyevuguvugu, kimbilia kwenye chemchemi ya maji ya uzima unywe maji yaliyo hai na ufue nguo zako, ufanyike kiumbe kipya, wakati umeisha Bwana yu karibu kurudi. Mungu alishamtuma mjumbe wake kwa kanisa letu la mwisho linaloitwa LAODIKIA , mjumbe huyu anaitwa WILLIAM MARRION BRANHAM, na ujumbe unaotangaza kuja kwa pili kwa Kristo, Hivyo ni vyema kujua kalenda ya Mungu na ujumbe wa Mungu kwa wakati unaoishi. Kwa kulijua hilo utaishi maisha ya uangalifu tukijua kuwa BWANA wetu yu karibu kurudi kumchukua bibi-arusi wake safi asiye na hila wala mawaa.

Bwana anaendelea kusema...

18 Namshuhudia kila mtu ayasikiaye maneno ya unabii wa kitabu hiki, Mtu ye yote akiyaongeza, Mungu atamwongezea hayo mapigo yaliyoandikwa katika kitabu hiki.
19 Na mtu ye yote akiondoa lo lote katika maneno ya unabii wa kitabu hiki, Mungu atamwondolea sehemu yake katika ule mti wa uzima, na katika ule mji mtakatifu, ambao habari zake zimeandikwa katika kitabu hiki.
20 Yeye mwenye kuyashuhudia haya asema, Naam; naja upesi. Amina; na uje, Bwana Yesu.
21 Neema ya Bwana Yesu na iwe pamoja nanyi nyote. Amina.
Huu ni wakati wa kupiga mbio kweli kweli tuhakikishe hatukosi kuwa katika hiyo YERUSALEMU MPYA bibi-arusi wa Kristo ambayo Bwana anaendelea kuiandaa hadi sasa, na watakaokuwa huko ni kundi dogo, biblia inasema..

Waebrania Mlango 12:
1 Basi na sisi pia, kwa kuwa tunazungukwa na wingu kubwa la mashahidi namna hii, na tuweke kando kila mzigo mzito, na dhambi ile ituzingayo kwa upesi; na tupige mbio kwa saburi katika yale mashindano yaliyowekwa mbele yetu,
2 tukimtazama Yesu, mwenye kuanzisha na mwenye kutimiza imani yetu; ambaye kwa ajili ya furaha iliyowekwa mbele yake aliustahimili msalaba na kuidharau aibu, naye ameketi mkono wa kuume wa kiti cha enzi cha Mungu.
3 Maana mtafakarini sana yeye aliyeyastahimili mapingamizi makuu namna hii ya watendao dhambi juu ya nafsi zao, msije mkachoka, mkizimia mioyoni mwenu. "

Amen.

Maran Atha!
 

No comments:

Post a Comment