Jina la
BWANA wetu YESU KRISTO lihimidiwe daima. Karibu katika uchambuzi wa kitabu cha
Ufunuo leo tukianza na ile sura ya kwanza.; Tunasoma...
“1 Ufunuo wa Yesu Kristo, aliopewa na Mungu awaonyeshe watumwa wake mambo ambayo kwamba hayana budi kuwako upesi; naye akatuma kwa mkono wa malaika akamwonyesha mtumwa wake Yohana; 2 aliyelishuhudia Neno la Mungu, na ushuhuda wa Yesu Kristo, yaani, mambo yote aliyoyaona.”
Awali
ya yote tunaona hapa Yohana akiandika na kusema "Ufunuo wa Yesu
Kristo" akimaanisha kuwa alichokipokea sio ufunuo wake bali ni wa Yesu
mwenyewe. Kumbuka Yohana ndiye Mtume pekee aliyekuwa karibu sana na
Bwana, na
aliyependwa na Bwana kuliko mitume wote, Kiasi kwamba hata siri za
karibu sana
za Bwana alikuwa anazipokea kwanza yeye ndiye ndipo wengine wafuate, ni
mtume
pekee aliyekuwa akiegema kifuani mwa Bwana muda wote (Yohana 13:23, na
Yohana
21:20), Na ndio maana tunaona wakati ule wa jioni wa kuumega mkate,
Bwana aliposema
mmoja wenu atanisaliti, Petro alimpungia mkono Yohana amuulize Bwana ni
nani
atakayemsaliti, na Bwana akamfunulia Yohana ni yule atakaye mmegea tonge
na kumpa, kwasababu Petro alijua Yohana ndiye kipenzi wa Bwana.
Kwasababu
ya uhusiano wake wa kipekee na Bwana, ilimpelekea, mpaka kufikia hatua ya kupewa neema
hii ya MAFUNUO na Bwana mwenyewe, mambo ambayo yatakuja kutokea katika siku
zake na siku za mwisho. Yohana ni mfano wa Danieli ambaye naye alikuwa ni mtu
aliyependwa sana na Mungu, Ikapelekea yeye naye kupewa mafunuo yanayofanana na
ya Yohana. Kwahiyo kama ukichunguza utagundua watu wanaofunuliwa Mafunuo makuu
kama haya sio tu kila mkristo, au mwamini yoyote bali ni mtu yule anayependezwa na
Mungu, Vivyo hivyo na sisi tukimpendeza Bwana atatupa siri zake za ndani zaidi.
Mstari
wa 3 unasema; "Heri asomaye na wao wayasikiao maneno ya unabii huu, na
kuyashika yaliyoandikwa humo; kwa maana wakati u karibu". Hapa Biblia
inasema heri ikiwa na maana kuwa amebarikiwa mtu yule ASOMAYE, ASIKIAYE,
na AYASHIKAYE ..Na kusikiwa kunakozungumziwa hapo ni kusikia kwa
masikio ya ndani (yaani
kupata Ufunuo ) na sio masikio ya nje, na kuyashika ikimaanisha kuyaishi
uliyoyasikia. Hivyo Mtu yeyote afanye hivyo biblia inasema amebarikiwa.
Kumbuka
Si watu wote wanapata neema hii ya kikielewa kitabu hichi, kwasababu ni
kitabu
kilichofungwa hivyo kinahitaji kufunguliwa na Roho mwenyewe. Kwahiyo
kama wewe
umepata neema, jitahidi kuyaishi yaliyoandikwa humo ili na wewe uitwe
HERI.
Tukiendelea
mistari inayofuata;
"4 Yohana, kwa yale makanisa saba yaliyoko Asia; Neema na iwe kwenu na amani, zitokazo kwake yeye aliyeko na aliyekuwako na atakayekuja; na zitokazo kwa roho saba walioko mbele ya kiti chake cha enzi;
5 tena zitokazo kwa Yesu Kristo, shahidi aliye mwaminifu, mzaliwa wa kwanza wa waliokufa, na mkuu wa wafalme wa dunia. Yeye atupendaye na kutuosha dhambi zetu katika damu yake,
6 na kutufanya kuwa ufalme, na makuhani kwa Mungu, naye ni Baba yake; utukufu na ukuu una Yeye hata milele na milele. Amina".
Tunasoma
hapa Yohana anaanza na salamu kwa yale makanisa 7 aliyopewa kuyaandikia
maneno
hayo. Anasema neema iwe kwenu na amani zitokazo kwa yeye "aliyekuwako,
aliyeko na atakayekuja", Hii inafunua umilele wa Mungu Elohimu, Yeye
pekee
ndiye asiyekuwa na mwanzo wala mwisho. Tena zitokazo kwa Roho saba
walioko
mbele ya kiti cha enzi cha Mungu. Sasa kumbuka Mungu hana Roho 7,
Tunajua wote
Mungu mwenyewe ni Roho(1),na nafsi moja, hapo anaposema hapa roho 7
haina maana kuwa anazo roho 7,
bali anaonyesha jinsi Roho ya Mungu ilivyokuwa inatenda kazi katika yale
makanisa 7
ambayo tutasoma habari zake hapo baadaye. Na pia anasema Neema na Amani
zitakazo kwa Yesu Kristo aliyeshahidi mwaminifu, mzaliwa wa kwanza wa
waliokufa. Kama tunavyojua Mungu alitoka katika UMILELE akaingia katika
MUDA
ili kumkomboa mwanadamu. Hivyo akaundaa mwili ili akae ndani yake. Na
huo mwili
ukawa YESU.
Kwahiyo Mungu alikuwa ndani ya Yesu akiupatanisha ulimwengu na nafsi yake (2Wakorintho 5:18-19). Kwahiyo hapa haizungumzii UTATU, hapana Mungu ni mmoja anayo nafsi moja, na Roho moja. Kwa mfano mimi nazungumza na wewe kwa kutumia account ya facebook, yenye jina, picha na utambulisho wangu. Ninazungumza, ninaongea na wewe ninajibu maswali, lakini haimaanishi sisi tupo wawili. kwamba wa kwanza ni mimi na wapili yule wa mtandaoni hapana mimi ni yule yule mmoja isipokuwa nimeingia ndani ya facebook ili nikutane na jamii ya watu fulani. vivyo hivyo na Mungu ambaye hana mwanzo wala mwisho aliingia ndani ya mwili wa kibinadamu (1Timotheo 3:16) ili tu kutupata sisi wanadamu..Na kama vile ile account yangu siku moja ilikuwa na mwanzo wake vivyo hivyo Bwana Yesu alikuwa na mwanzo, na ndio maana atakuja kuona kuna mahali anasema yeye ni ALFA NA OMEGA. Lakini haimaanishi kuwa Mungu(ELOHIM) ni mwanzo na mwisho..hapana Yeye hana mwanzo wala mwisho.
Kwahiyo Mungu alikuwa ndani ya Yesu akiupatanisha ulimwengu na nafsi yake (2Wakorintho 5:18-19). Kwahiyo hapa haizungumzii UTATU, hapana Mungu ni mmoja anayo nafsi moja, na Roho moja. Kwa mfano mimi nazungumza na wewe kwa kutumia account ya facebook, yenye jina, picha na utambulisho wangu. Ninazungumza, ninaongea na wewe ninajibu maswali, lakini haimaanishi sisi tupo wawili. kwamba wa kwanza ni mimi na wapili yule wa mtandaoni hapana mimi ni yule yule mmoja isipokuwa nimeingia ndani ya facebook ili nikutane na jamii ya watu fulani. vivyo hivyo na Mungu ambaye hana mwanzo wala mwisho aliingia ndani ya mwili wa kibinadamu (1Timotheo 3:16) ili tu kutupata sisi wanadamu..Na kama vile ile account yangu siku moja ilikuwa na mwanzo wake vivyo hivyo Bwana Yesu alikuwa na mwanzo, na ndio maana atakuja kuona kuna mahali anasema yeye ni ALFA NA OMEGA. Lakini haimaanishi kuwa Mungu(ELOHIM) ni mwanzo na mwisho..hapana Yeye hana mwanzo wala mwisho.
"7 Tazama, yuaja na mawingu; na kila jicho litamwona, na hao waliomchoma; na kabila zote za dunia wataomboleza kwa ajili yake. Naam. Amina.
8 Mimi ni Alfa na Omega, mwanzo na mwisho, asema Bwana Mungu, aliyeko na aliyekuwako na atakayekuja, Mwenyezi".
Sasa
Biblia inasema upo wakati Bwana
aliouweka wa yeye kurudi tena ambao kila jicho litamwona na hao
waliomchoma mkuki
pale Kalvari (yaani wayahudi na watu wa mataifa) watamwombolezea,
kumbuka hapa sio
ule wakati wa kulichukua kanisa lake, hapana bali utakuwa ni ujio wa
Bwana Yesu
kuja duniani na watakatifu wake waliokuwa wameshanyakuliwa muda wa miaka
7 iliyopita tangu tukio hilo litokee. Hapo ndipo kila jicho
la watu waliosalia ambao majina yao hayakuandikwa katika kitabu cha
uzima tangu
kuwekwa misingi ya ulimwengu watamwona na kumuombolezea..
Mathayo 24: 29 "
Lakini mara, baada ya dhiki ya siku zile, jua litatiwa giza, na mwezi hautatoa mwanga wake, na nyota zitaanguka mbinguni, na nguvu za mbinguni zitatikisika;
30 ndipo itakapoonekana ishara yake Mwana wa Adamu mbinguni; ndipo mataifa yote ya ulimwengu watakapoomboleza, nao watamwona Mwana wa Adamu akija juu ya mawingu ya mbinguni pamoja na nguvu na utukufu mwingi. (soma pia Yuda 1:14 na Ufunuo 19:11-21,)
Tukiendelea mistari inayofuata....
" 9 Mimi Yohana, ndugu yenu na mwenye kushiriki pamoja nanyi katika MATESO na UFALME na SUBIRA ya Yesu Kristo, nalikuwa katika kisiwa kiitwacho Patmo, kwa ajili ya Neno la Mungu, na ushuhuda wa Yesu.
10 Nalikuwa katika Roho, siku ya Bwana; nikasikia sauti kuu nyuma yangu, kama sauti ya baragumu,
11 ikisema, Haya uyaonayo uyaandike katika chuo, ukayapeleke kwa hayo makanisa saba: Efeso, na Smirna, na Pergamo, na Thiatira, na Sardi, na Filadelfia, na Laodikia."
Yohana
anasema "mimi ndugu yenu
mwenye kushiriki pamoja nanyi"...Ikiwa na maana kuwa kile alichokuwa
anakipitia, ndugu wengine walikuwa wanakipitia pia.mateso,
dhiki,vifungo, na
subira ya Yesu Kristo. Hii inaonyesha kabisa mojawapo ya utambulisho wa
mkristo
kwamba yupo katika safari ya Imani ni kupitia hayo kwa ajili ya
Bwana.(Kumbuka ni kwa ajili ya Bwana, na si kwasababu nyingine zozote)
Lakini
tunapokuwa wakristo lakini hatuna subira, kwa ajili ya Bwana, inaonyesha kabisa
hatupo miongoni mwa hao ndugu waaminio.. Yohana anasema alikuwa katika kisiwa
kiitwacho PATMO.Hichi ni kisiwa kilichokuwa maeneo ambayo sio mbali sana na yale
makanisa 7 yaliyokuwepo Asia ndogo (ambayo kwasasa ni maeneo ya UTURUKI) umbali wa
takribani km 60-120.
Ni kisiwa ambacho wafungwa walikuwa
wanaenda kuachwa huko wafe, ni kisiwa kilichokuwa na mawe mawe tu, mijusi nyoka
na kenge, na nge. Hakuna mimea kumezungukwa na maji kote, hivyo ni mahali
pasipokuwa na jinsi yoyote ya kuishi au kutoroka mtu utaishia kufa kwa njaa au
kuuawa na wanyama wakali. Hivyo Yohana naye alitupwa kule kama mmojawapo wa
wafungwa. Na ndipo huko huko Bwana akamfunulia mambo ya siri kama tunavyoyasoma. Nasi
pia tunajifunza wakati mwingine tukitupwa katika majaribu mazito (maadamu ni
wakristo) tujue ni Bwana anaruhusu mwenyewe ili kutupa mafunuo zaidi.
Hivyo maono hayo Yohana
aliyoonyeshwa hayakuwa ndani ya siku moja yote..Bali ulikuwa ni mfululizo wa
maono kwa kipindi cha muda fulani.Ndipo akapewa maagizo kwamba ayaandike mambo yote
anayoyaona na ayapeleke kwa yale makanisa saba yaliyopo Asia, yaani
Efeso, na Smirna, na Pergamo, na Thiatira, na Sardi, na Filadelfia, na Laodikia.
MTU MFANO WA MWANADAMU.
"12 Nikageuka niione ile sauti iliyosema nami. Na nilipogeuka, niliona vinara vya taa saba vya dhahabu;
13 na katikati ya vile vinara nikaona mtu mfano wa Mwanadamu, amevaa vazi lililofika miguuni, na kufungwa mshipi wa dhahabu matitini.
14 Kichwa chake na nywele zake zilikuwa nyeupe kama sufu nyeupe, kama theluji; na macho yake kama mwali wa moto;
15 na miguu yake kama shaba iliyosuguliwa sana, kana kwamba imesafishwa katika tanuru; na sauti yake kama sauti ya maji mengi".
Tunaona Yohana alipogeuka aisikie
ile sauti akaona mtu "MFANO" wa mwanadamu. aliyevaa vazi lililofika
miguuni, na kufungwa mshipi wa dhahabu matitini. Kumbuka Yohana kuonyeshwa vile
haikuwa na maana kuwa Bwana Yesu anataka kuonyesha mwili wake jinsi ulivyo na
utukufu au unavyotisha mbele za wanadamu, hapana, bali kila kitu alichokuwa anakiona katika mwili
wake kilikuwa kina maana fulani.. Kumbuka lile lilikuwa ni ONO sio kitu halisi.
Tukisoma
tunaona
Mtu yule alikuwa na nywele kama sufu nyeupe. Ikiashiria kuwa
ni HAKIMU. (Kumbuka mahakimu huwa ni desturi yao kuvaa wigi nyeupe
kichwani) Hivyo yule ni Muhukumu wa mambo yote, na weupe wake inaashiria
usafi na haki ya
hukumu yake. Atakapokuja kuketi katika kiti chake cha enzi cheupe,
atawahukumu
kwa haki watu wote. Tutakuja kuona vizuri katika sura 20.
Na
pia mtu huyu alionekana ana macho kama mwali wa moto, na miguu iliyosuguliwa
kama shaba. Ikifunua hukumu yake juu ya waovu katika kanisa na wasiomcha yeye
ulimwenguni kote,.Kumbuka na macho kazi yake ni kuona, na miguu ni kukanyaga.
Hivyo anapoonekana na macho ya moto inamaanisha kuwa anaona mambo yote
yanayopaswa kuhukumiwa kwa moto. Tutakuja kuona pia katika kanisa la tatu la
Thiatira (jinsi Bwana alivyojionyesha kwao kama miale ya moto na miguu ya shaba,
kutokana na maovu yaliyojificha ndani ya kanisa hilo,).
Na
kama miguu yake ilivyokuwa ya SHABA atakanyaga mambo yote maovu ndani ya kanisa lake
kwanza kisha baadaye atamalizia na kwa ulimwengu mzima tutakapofika katika sura ya 14
tutaona pia jinsi atakavyokuja kukanyaga shinikizo la mvinyo ya ghadhabu ya
hasira ya Mungu mwenyezi(Ufunuo 19:15).
Tukizidi kuendelea
kusoma mistari inayofuata..;
“16 Naye alikuwa na nyota saba katika mkono wake wa kuume; na upanga mkali, wenye makali kuwili, ukitoka katika kinywa chake; na uso wake kama jua liking'aa kwa nguvu zake.
17 Nami nilipomwona, nalianguka miguuni pake kama mtu aliyekufa. Akaweka mkono wake wa kuume juu yangu, akisema, Usiogope, Mimi ni wa kwanza na wa mwisho,
18 na aliye hai; nami nalikuwa nimekufa, na tazama, ni hai hata milele na milele. Nami ninazo funguo za mauti, na za kuzimu. 19 Basi, uyaandike mambo hayo uliyoyaona, nayo yaliyopo, na yale yatakayokuwa baada ya hayo.
20 Siri ya zile nyota saba ulizoziona katika mkono wangu wa kuume, na ya vile vinara saba vya dhahabu. Zile nyota saba ni malaika wa yale makanisa saba; na vile vinara saba ni makanisa saba”.
Tunaona pia mtu huyu anaonekana akiwa na nyota saba katika mkono wake wa kuume. Hizi nyota saba tafsiri yake kama inavyoelezwa ni malaika saba, mkono tunajua kazi yake ni kubeba, na ukiwa wa kuume, inamaana unabeba kitu stahiki, hivyo wale malaika (wajumbe 7) watakuwa wamebeba ujumbe stahiki kwa kanisa husika. na pia alionekana akitembea katikati ya vile vinara 7 vya taa ambavyo ndiyo yale makanisa 7. Jiulize ni kwanini hakuonekana akiwa katikati ya madhabahu, au katika birika ya shaba Katika Hekalu la Mungu?, bali anaonekana katikati ya vile vinara 7 vya Taa akitembea katikati yake?. Inamaana kuwa makao yake ni katikati ya yale makanisa saba. Huko ndipo jicho lake lilipo na Roho yake ilipo.
Mtu huyu pia alionekana na Upanga mkali ukatao kuwili unaotoka kinywani mwake. Kwa kawaida mtu hawezi kutoa upanga mdomoni, Tunafahamu Neno la Mungu ndio upanga wa Roho (soma waefeso 6:17) na pia waebrania 4: 12 inasema …“Maana Neno la Mungu li hai, tena lina nguvu, tena lina ukali kuliko upanga uwao wote ukatao kuwili, tena lachoma hata kuzigawanya nafsi na roho, na viungo na mafuta yaliyomo ndani yake; tena li jepesi kuyatambua mawazo na makusudi ya moyo”.
Hivyo upanga huo ambao ni NENO lake ameuandaa tayari kwa ajili ya vita kwa watu wote wanaokwenda kinyume na mapenzi ya Mungu. Na kama anavyosema ni upanga ukatao kuwili anamaanisha kuwa ni upanga unaokata pande zote yaani watu walioko ndani ya kanisa na watu walioko nje ya Kanisa.
Jambo hili tutakuja kuliona jinsi Bwana alivyojifunua kwao(Kanisa
la pili Pergamo) kwamba yeye ndiye mwenye ule upanga mkali ukatao kuwili…aliasema "anayajua
matendo yao na kwamba watubu na wasipotubu
atakuja kufanya vita nao kwa huo upanga wa kinywa chake.(Ufunuo 2:16).
Kadhalika na kwa watu wa mataifa wasiomjua Mungu wao nao
Bwana atakuja kufanya nao vita kwa huo upanga, jambo hili tutakuja kuliona
katika ile sura ya 19:15 katika siku ile atakapokuja mara ya pili na watakatifu wake.
Utaona pia baada ya
Yohana kuuona muonekana wa nje wa yule mtu alianguka chini kwa hofu na
kutetemeka, Tunasoma " 17 Nami nilipomwona, nalianguka miguuni pake kama
mtu aliyekufa. Akaweka mkono wake wa kuume juu yangu, akisema, Usiogope, Mimi
ni wa kwanza na wa mwisho,
18 na aliye hai; nami nalikuwa nimekufa, na tazama, ni hai hata milele na milele. Nami ninazo funguo za mauti, na za kuzimu. "
18 na aliye hai; nami nalikuwa nimekufa, na tazama, ni hai hata milele na milele. Nami ninazo funguo za mauti, na za kuzimu. "
Ndipo
baada ya hayo yule mtu akajitambulisha kwa tabia zake za ndani ambazo Yohana
hakuziona kwa macho..nazo ni
1)yeye ni wa kwanza na wa mwisho,
2)
aliye hai,aliyekuwa amekufa na sasa yu hai milele na milele na ambaye
3)
anazo funguo za Kuzimu.
Sasa
kwa tabia hizo TATU Yohana ndipo alipojua kuwa yule MTU ni YESU KRISTO
mwenyewe. Hivyo ule muonekano wa Nje ni msingi utakaotusaidi kuelezea
ujumbe na kuelewa utendaji kazi wa Yesu katika habari husika zinazofuata. Ni
muhimu kuzingatia hivyo vipengele, mfano tunaweza kuona katika kila kanisa
anaanza kwa kujitambulisha kwa kipengele kimoja wapo cha mwili wake au tabia
zake.
Hivyo
kwa ufupi
Alichoonyeshwa Yohana ni mfano wa ile sanamu aliyoonyeshwa Nebukadreza
juu ya
zile Falme 4 zitakazokuja kutawala mpaka mwisho wa dunia. Na kwamba kila
sehemu
ya ile sanamu (Kichwa cha dhahabu, kifua cha fedha, kiuno cha shaba na
miguu ya chuma) ilikuwa na maana, na ndio iliyounda msingi wa kuelewa
undani wa
kitabu cha Danieli katika sura za mbeleni.Kadhalika na hichi kitabu cha
Ufunuo,
sura hii ya kwanza (Ambayo Inayoonyesha muonekano na tabia za Yesu
Kristo ) ni msingi wa sisi
kuelewa ujumbe katika sura zinazofuata za kitabu cha Ufunuo.
Hivyo
usikose mwendelezo wa sura zinazofuata..
Ubarikiwe
sana.
No comments:
Post a Comment