"Tazama, naja kama mwivi. Heri akeshaye, na kuyatunza mavazi yake, asiende uchi hata watu wakaione aibu yake...ufunuo 16:15"

Monday, May 28, 2018

MASWALI NA MAJIBU: SEHEMU YA 25

SWALI 1: Nina swali kidogo wapendwa , hivi roho ya sauli (sauli asiye paulo ) ilienda wapi baada ya kufa?(KUZIMU au PEPONI?) maana bwana alimuacha?
JIBU: Ukisoma kwenye biblia kuna kitu kinachoitwa DHAMBI YA MAUTI na DHAMBI ISIYO YA MAUTI. (1Yohana 5:16)..Sasa Hii dhambi isiyo ya mauti mtu anaweza akaitenda na ndugu wakamuombea kwa Mungu akamsamehe kutokana na maombi yao na akapata neema ya akaendelea kuishi..Lakini ipo nyingine hiyo hata mtu aombeweje, ndio utasamehewa lakini adhabu ya kifo ipo pale pale..hii inakuja pale mtu wa Mungu anapofanya dhambi ya makusudi angali anafahamu kabisa anachokifanya sio sawa. Mfano wa watu kama hawa ndio kama SAULI.

Sauli Kwanza Alimkosea Mungu kwa kwenda kinyume na maagizo yake ya kutokutii masharti aliyopewa (maana Bwana alimwambia akawaue waamaleki wote asiache kitu chochote binadamu wala mfugo, {1samweli 15} lakini yeye alikaidi, badala ya kuangamiza kila kitu yeye akaacha hai kondoo,ng'ombe na kuteka nyara baadhi ya vitu) hiyo ilimsababishia Mungu kuukataa ufalme wake, Hivyo hata angeombewaje, Mungu asingeweza kumkubali tena, kama ukisoma biblia utaona Samweli alijaribu kumwombea sana kwa Mungu ili apewe rehema lakini Bwana alichokisema juu yake alishakisema "Kwamba ufalme wake umeraruliwa amepewa mtu mwingine" (Soma 1 wafalme 16:1)..

Pili, Sauli alimkosea Mungu kwa kwenda kwa wapunga pepo kutafuta majibu ya maswali yake kitu ambacho anafahamu kabisa ni kinyume na TORATI, isitoshe yeye ndio aliyekuwa wa kwanza kuwaondoa wachawi wote katika Israeli lakini hapa ndiye anayekuwa wa kwanza kuwafuata..Sasa kitendo kama hicho ni sawa na kutenda DHAMBI YA MAUTI. Hata angelia vipi asingeweza kusamehewa aendelee kuishi..Japo baada ya kufa angeweza kuokolewa.

Na ndio maana Sauli Alipomwendea yule mchawi, Samweli alimwambia ..
1Samweli 28: 16 "Samweli akasema, Kwa nini kuniuliza mimi, AKIWA BWANA AMEKUACHA, naye amekuwa adui yako?17 Yeye Bwana amekutendea kama alivyosema kwa kinywa changu; Bwana amekurarulia ufalme mkononi mwako, na kumpa jirani yako, yaani, Daudi.18 Kwa sababu wewe hukuitii sauti ya Bwana, wala hukumtimilizia hasira yake kali juu ya Amaleki; kwa sababu hii Bwana amekutendea hili leo.19 Tena pamoja na wewe Bwana atawatia Israeli mikononi mwa Wafilisti; HATA NA KESHO WEWE NA WANAO MTAKUWAPO ""PAMOJA NAMI""; tena Bwana atawatia jeshi la Israeli pia mikononi mwa Wafilisti. "

Unaona hapo adhabu yake ilikuwa ni ufalme wake kuchukuliwa na mwingine, pamoja na kifo basi!!. Lakini baada ya kufa Samweli anamwambia, Kesho wewe na wanao mtakuwa pamoja nami. Neno pamoja nami linamaanisha, Sauli atakuwepo pamoja na Samweli katika sehemu ya wenye haki, Hivyo Sauli yupo Paradiso na akina Samweli sasa, kwasababu pia kumbuka alikuwa ni mtiwa mafuta na BWANA na ndio maana Daudi hakudhubutu kumwangamiza popote pale. Ila kwasababu ya uzembe wake mwenyewe alijiondolea thawabu zake alipokuwa duniani
. Kwa maelezo marefu kuhusu "dhambi ya mauti" soma kupitia linki hii>>> https://wingulamashahidiwakristo.blogspot.com/2017/07/dhambi-ya-mauti.html#links

SWALI 2: Ufunuo Yohana 16:5 anasema "Nikamsikia malaika wa maji akisema",...Huyu malaika wa maji Yohana aliyesema alimsikia akisema "Wewe u mwenye haki, uliyeko na uliyekuwako,Mtakatifu, kwakuwa umehukumu hivi" ndugu tunaweza tukamfahamu huyu malaika ni nani?
JIBU: Ulimwengu wa malaika ni mkubwa/Mpana sana kama vile ulivyo ulimwengu wa wanadamu, Kama vile Mungu alivyotoa vipawa tofauti tofauti kwa wanadamu, vivyo hivyo alitoa vipawa tofauti tofauti kwa malaika zake,..wapo malaika wa maji, wapo malaika wa moto (ufunuo 14:18), wapo malaika wa vita, mfano Mikaeli na wenzake, wapo wajumbe kama Gabrieli na wenzake, na wapo pia wa sifa (makerubi na maserafi) na shetani naye alikuwa kwenye hili kundi kabla ya kuasi, n.k. kwahiyo wapo wengi hata wengine hatuwajui, na wala hatujawahi kuwaona, wapo walinzi, wapo malaika wa kila nchi, wapo wa kila mkristo mmoja mmoja, na wapo wanaosimama kwa kila huduma, n.k kila mmoja anatenda kazi kulingana na alipopangiwa na Mungu mwenyewe....Hawaonekani kwa macho, ni viumbe wa rohoni, isipokuwa mara chache chache sana, wanaonekana kama Bwana akipenda kukufunulia uwaone, Hivyo ukimwomba Mungu akufunulie hata mmoja, siku moja ikimpendeza atakuonyesha, nakumbuka sisi siku moja tulikuwa tunamtafakari Mungu mida ya usiku, kama saa 1:45 jioni, umeme ulikuwa umekatika tunatazama nyota juu tukaona kitu  mfano wa mwanga mkali sana unaofanana na ule wa kuchomelea kama wa blue hivi, tulimwona kama kwa muda wa sekundi 2, tatu hivi akatoweka, eneo lote liliangaza ule mwanga, tuliogopa sana, lakini baadaye tukajua ni Mungu alikuwa anatuonyesha utukufu wake...ndio maana MUNGU WETU ANAITWA BWANA WA MAJESHI! unaweza ukajiuliza hayo majeshi ni akina nani??? sio wanadamu kwasababu wanadamu sisi tunaitwa WANA WA MUNGU (Waebrania 1:5) bali ni malaika ndio wanaoitwa MAJESHI ya BWANA...yapo MAELFU kwa MAELFU ya malaika wanazunguka kila siku duniani kuwahudumia watu wa Mungu(Waebrania 1:13-14).

SWALI 3: Ndugu nielewesheni hapa wapenzi? Ile SANAMU YA MNYAMA ya ufunuo kumi na tatu. Tunajua ni Muungano wa madhehebu yote ulimwenguni kuwa dini moja.ndugu sasa maswali ya ni haya 1.Huu muungano wa madhebu yote na dini zote ulimwenguni yakiungana kuwa KITU KIMOJA (yaani DINI MOJA).sasa watakaokuwa wanahudumu kanisani hilo la DINI MOJA ni mapadre tu? ama watakuwa ni akina nani?.

JIBU: hapana muungano wa madhehebu na dini zote, hautakuwa muungano wa kiimani na kutengeneza kanisa moja,hapana!! bali utakuwa ni muungano wa kiitikadi, kila mtu atabaki na dini yake na dhehebu lake isipokuwa wote watakubaliana katika katiba moja. kwa mfano tanganyika ilivyoungana na zanzibar haikulazimisha watu wote tufanane, kidini, kiutamaduni n.k hapana kila nchi ilibaki na tamaduni zake na sera zake na dini yake isipokuwa mambo ya itikadi ndiyo yaliyoungana kwamfano jeshi moja,lugha moja n.k au vyama vya siasa vinapoungana, mfano kwa hapa Tanzania UKAWA, ni vyama vingi vimeungana kwa lengo fulani, lakini kila chama kina itikadi zake na desturi zake,  wameungana kwa lengo la kutimiza kusudi Fulani, lakini kila chama kinajitegemea, kwahiyo yoyote atakaye kuwa mmoja wa chama hicho automatically atakuwa ameshajiingiza moja kwa moja katika muungano huo hata kama hataki...Na ndio maana yule mwanamke anaitwa mama wa makahaba, ikiwa na maana atakuwa na mabinti anaowaendesha chini yake.. kwahiyo hapo baadaye wakishirikiana pamoja wafikie muafaka wa ustaarabu mpya wakiongozwa na Kanisa lao mama Katoliki, ambao utafanana kwa dini zote, na mtu yoyote asipoufuata, madhara yatamkuta. na hii itagusa karibu dini zote na madhehebu yote duniani..
SWALI 4: Wale mitume wa BWANA wote walikuwa wasomi?
 JIBU: Hapana sio wote walikuwa wasomi, maana biblia kuna sehemu imewataja kuwa ni watu wasio na  Elimu (Matendo 4:13 " 13 Basi walipoona ujasiri wa Petro na Yohana, na kuwajua ya kuwa ni watu WASIO NA ELIMU,WASIO NA MAARIFA , wakastaajabu, wakawatambua ya kwamba walikuwa pamoja na Yesu.") Hivyo walikuwa ni watu wa kawaida, isipokuwa yule mathayo mtoza ushuru( kwasababu mtoza ushuru ni lazima awe mtu aliyesoma).. labda pengine na mwingine ni Yuda iskariote aliyekuwa anashikilia mfuko wa hazina..lakini wengine wote walikuwa ni watu tu wa kawaida wasio na elimu wengi wao walikuwa ni wavuvi

No comments:

Post a Comment