"Tazama, naja kama mwivi. Heri akeshaye, na kuyatunza mavazi yake, asiende uchi hata watu wakaione aibu yake...ufunuo 16:15"

Tuesday, May 29, 2018

MASWALI NA MAJIBU: SEHEMU YA 26

 SWALI:Barikiwa sana swali langu je mwanadamu wa kwanza kuumbwa.ni yupi mzungu mwafrika au mchina na kama ni mmojawapo kati ya hao je hao wengine wametoka wapi ? By lucas
JIBU: Ni muhimu kufahamu kuwa Mungu aliiumba jamii moja tu ya watu..Hakuumba jamii nyingi za watu pale Edeni na hii jamii tunaipata kutoka kwa Adamu na Hawa (Mwanzo 1: 27 Mungu akaumba mtu kwa mfano wake, kwa mfano wa Mungu alimwumba, mwanamume na mwanamke aliwaumba ). Watu Hawa wawili ndio Mungu aliowaumba kwa ukamilifu wote bila kasoro kubwa wala ndogo,sasa Adamu na mke wake hawakuwa wazungu hapo mwanzo, kama wengi wanavyodhani, au waafrika au wachina au wahindi au jamii nyingine yeyote ya watu tunayoiona leo. la! Adamu na Hawa walikuwa ni watu wenye upekee wao ambao leo hii hatuwezi kuuona kwa mtu yeyote aliyeko duniani, wala hakuna mfano wa kulinganishwa nao kwa uzuri na mvuto waliokuwa nao kwasababu Mungu aliwaumba wakamilifu sana pasipo mapungufu yeyote. Lakini baada ya wao kumkosea Mungu na kuasi ule ndipo utukufu waliokuwa nao ukaanza kuondoka kidogo kidogo na mauti kuingia ndani yao.Siku baada ya siku wakaanza kubadilika mionekano yao ikaanza kuwa kama yetu sisi tunavyoonekana sasa hivi.
Hivyo miili yao ikaanza kubadilika ghafla kutokana na kwamba Utukufu wa Mungu umewaondokea, ardhi ikalaaniwa kama tunavyosoma, jua likaanza kuwa kali, mimea ikaanza kukauka baadhi ya maeneo, na kusababisha majagwa kutokea duniani, jasho likaanza kuwatoka kutokana na jua kuwa kali, ngozi zikazidi kubadilika, makovu yakaanza kutokea..Watu wakaanza kuzaliana kwa kasi na baada ya gharika dunia ilipozidi kuharibika zaidi na kupoteza taswira iliyokuwa nayo kwanza, tunakuja kuona watu wakaanza kuweka tena ustaarabu mpya duniani wakaanza kujenga ule mnara wa Babeli ili wamfikie Mungu..Lakini Mungu alipoona matendo yao ndipo akawatawanya waende katika pembe zote za dunia..
Sasa kuanzia hapo jamii ya watu walikwenda zile sehemu zenye majangwa, wakakaa huko, wengine walikimbilia nchi za baridi, wakaa kaa huko, wengine sehemu za barafu, wengine visiwani, wengine misituni n.k...Hivyo walipoendelea kukaa kwa muda mrefu kutokana na mazingira waliyopo, wakaanza kuendana na yale mazingira, ndipo watu wakaonekana tofuati zao kulingana na mahali walipotokea.. Kwa mfano watu waliokuja pande za Afrika, mazingira ya huku tunafahamu ni ya joto, hivyo ni dhahiri kuwa ngozi ikipigwa na jua kwa muda mrefu inakuwa nyeusi, na pia nywele zinapungua..kwahiyo hatushangai kuona watu wa Afrika ni weusi, kadhalika na watu waliopo nchi za baridi miili yao kwa kawaida itahitaji joto, hivyo nywele zitalazimika kukua na kuwa ndefu huko ndipo tunapowaona watu jamii ya wazungu, ukitazama nchi kama ya India, wahindi waliopo pande za kaskazini za baridi kama DELHI n.k utaona ngozi yao ni nyeupe, kadhalika waliopo pande za kusini(mf. Sri Lanka) ambako kuna joto kali utaone ngozi yao umefifia kidogo(inakuwa nyeusi) n.k. Na kumbuka hii sio tu kwa wanadamu..bali hata kwa wanyama..Kama ukichunguza wanyama kama kondoo,ng'ombe au mbuzi mwitu, au farasi,mbwa,tembo n.k wanaotoka nchi za baridi utawaona wana manyoya mengi zaidi, kuliko wale wanaotokea nchi za joto. Hivyo kwa ufupi mazingira ndiyo yaliyowabadilisha watu, na si kingine.
SWALI:: Hivi wakati Yohana akiwa kule kisiwa cha Patmo alivyopewa ule Ufunuo wale mitume wenzake walikuwepo duniani au walikuwa wameshaondoka duniani.??Na kama walikuwepo je! walikifundisha?? Swali:Kule Yohana alisema alikuwa kisiwa cha Patmo.kisiwa cha Patmo kipo Nchi gani ndugu?? .

JIBU: Kitabu cha Ufunuo kulingana na Historia kiliandikwa kati ya mwaka AD 90 na AD 96..Wakati huo yeye(Yohana) alikuwa ni mzee sana na mitume wengine walikuwa wameshakufa.. Na aliyekipeleka katika yale makanisa saba yaliyokuwa Asia ndogo ni yeye mwenyewe. Na kuhusu kisiwa cha Patmo kilikuwa Maeneo kando kando ya Uturuki ni kisiwa kidogo sana kilichokuwa umbali kama wa km 60 mpaka 120km kutoka Uturuki (Asia ndogo) mahali makanisa yalipokuwepo.

SWALI: Ndugu Hivi yale makanisa 7 halisi aliyoonyeshwa Yohana yaliyokuwepo Asia ndogo ambayo Yohana alionyeshwa yalikuwa ni ya watu waliookoka kwa kuhubiriwa injili na mitume ndugu?!
JIBU: Kwanza ni vizuri kufahamu yale ni maeneo tofauti tofauti kama vile ilivyo leo Tanzania..kuna moshi, arusha, tanga n.k. Ndivyo ilivyokuwa pia kwa Asia ndogo (Uturuki) kulikuwa na maeneo tofauti tofauti kama Efeso, smirna, Laodikia n.k. Sasa katikati ya hayo maeneo kulikuwa na wakristo waliohubiriwa injili na mitume na kuamini. Hivyo zile barua zilipelekwa kwa wakristo waliokuwepo katika hayo maeneo husika, kila kanisa na barua yake...ukisoma kitabu cha matendo utaona ziara za mitume katikati ya baadhi ya hayo makanisa. Tazama picha chini ya hayo makanisa na kisiwa cha Patmo yalipokuwepo.
 (Ramani ya Asia ndogo(Uturuki) kipindi cha kanisa la kwanza)



  (nchi ya Uturuki kwa sasa hivi ilivyo)
Ubarikiwe.

No comments:

Post a Comment