"Tazama, naja kama mwivi. Heri akeshaye, na kuyatunza mavazi yake, asiende uchi hata watu wakaione aibu yake...ufunuo 16:15"

Tuesday, September 25, 2018

TANGAZO.


Shalom!

Tangazo.

Ndugu/Dada atakayehitaji kubatizwa, siku ya jumamosi (yaani tarehe 29/09/2018), tutakuwa na huduma ya ubatizo, maeneo ya Ocean road, Dar es salaam. Ubatizo utakuwa ni wa kuzamishwa katika maji mengi kama maandiko yanavyotuagiza na utakuwa ni katika JINA LA YESU KRISTO sawasawa na Matendo 2:38, mdo 8:16,mdo 10:48, na mdo 19:5. 
 

Hivyo ikiwa na wewe ni mmojawapo atakeyekuwa na uhitaji huo wa kubatizwa, tutawasiliana kwa namba zilizohapo chini au kwa inbox. Kadhalika unapopata ujumbe huu mtaarifu na wenzako anayehitaji kufanya hivyo. Hakuna kiingilio, hakuna madarasa ya kupitia kwanza, kwani biblia inatuongoza kuwa pindi mtu anapoamini tu! anapaswa akabatizwe kwa ajili ya ondoleo la dhambi zake.

Kumbuka ili mtu awe amezaliwa mara ya pili ni lazima awe amebatizwa kwa maji na kwa Roho. Hivyo ikiwa ulishaamini na bado haujabatizwa, au ulibatizwa kimakosa utotoni, basi yakupasa ukabatizwe tena kwa ajili ya ondoleo la dhambi zako. Kumbuka pia ubatizo sio dini mpya au dhehebu jipya bali ni maagizo mwamini yeyote yule anapaswa ayafuate.

Mungu akubariki.

Tuwasiliane kwa namba zifuatazo / 0679804471 au 0787070918.

No comments:

Post a Comment