"Tazama, naja kama mwivi. Heri akeshaye, na kuyatunza mavazi yake, asiende uchi hata watu wakaione aibu yake...ufunuo 16:15"

Thursday, January 31, 2019

MASWALI NA MAJIBU: SEHEMU YA 53


SWALI 1: Je!Mungu anaweza kuleta majibu kupitia nguvu za giza maana nashindwa Kuelewa ninaposoma habari za Mfalme Sauli kupata majibu kwa mwanamke mwenye pepo.

JIBU:Shalom!. Ni vizuri tuifahamu sifa ya Mungu, ili tusiishie tu kumchukulia yeye yupo mbinguni kaketi kwenye kiti cha Enzi, mahali pengine popote palipo pachafu hawezi kuingia wala kukanyaga, wala kujua kinachoendelea huko.

Zaburi 139:7 “Niende wapi nijiepushe na roho yako? Niende wapi niukimbie uso wako?
8 Kama ningepanda mbinguni, Wewe uko; Ningefanya ku
zimu kitanda changu, Wewe uko.
9 Ningezitwaa mbawa za asubuhi, Na kukaa pande za mwisho za bahari;
10 Huko nako mkono wako utaniongoza, Na mkono wako wa kuume utanishika.
11 Kama nikisema, Hakika giza litanifunika, Na nuru inizungukayo ingekuwa usiku;
12 Giza nalo halikufichi kitu, Bali usiku huangaza kama mchana; Giza na mwanga kwako ni sawasawa.”

Na ndio maana ukisoma ule mstari ule mstari wa 6 juu yake kidogo unasema hivi.. “Maarifa hayo ni ya ajabu, yanishinda mimi, Hayadirikiki, siwezi kuyafikia.” Hii Ikiwa na maana kuwa uweza wa Mungu hautambulikani, na njia zake hazitafutikani hata tukijaribu kumtafakari Mungu vipi, hatuwezi kumpima kwa akili zetu hizi za kibinadamu kwa jinsi alivyoenea kila mahali.

Hiyo Inatuthibitishia kuwa Mungu pekee ndiye anayeweza kuwepo kila mahali, na ndio pekee mwenye funguo za makao ya viumbe vyote ulimwenguni,..hakuna mwingine yeyote mwenye uwezo huo.Kama tunavyofahamu..Zipo falme Kuu tatu zinazotembea katika duara lote la uumbaji wa Mungu, Ufalme wa kwanza ni ufalme wa Mungu mwenyewe ambao huo upo katika ulimwengu wa roho, na ufalme wa pili ni ufalme wa giza nao pia upo katika ulimwengu wa roho, na ufalme ya tatu ni ufalme ya wanadamu ambao ndio huu tunaouona katika mwili na ndio huu tunaoishi mimi mimi na wewe.

Na falme hizi zote kila mmoja inayo utendaji kazi wake wenyewe, na nguvu zake, na mamlaka yake yenyewe, na kama zilivyojipanga ile Falme ya kwanza ndiyo yenye nguvu zaidi mbali na nyingine zote ndiyo ya Mungu wetu, kisha hapo chini unafuata ufalme wa giza ambao ndio shetani anaumiliki, na wa mwisho ndio huu wa kwetu sisi wanadamu.

Sasa Yule mwenye nguvu zaidi ndiye mwenye uwezo wa kuingia na kutoka kwenye ufalme wa chini yake. Kwa mfano ufalme wa mbinguni ambao ndio wa Mungu wetu, unaouwezo wa kuamua lolote juu hizi falme mbili za chini, unaouwezo wa kuzitumia au kuziamurisha lolote la kufanya, zinaweza kutumiwa pia kutimiza kusudi Fulani la Mungu kwa muda kwa kipindi fulani. Vivyo hivyo na ufalme wa pili ambao ni wa giza unao nguvu wa kuumurisha ufalme wa chini yake (yaani sisi tunaouishi), kamwe mwanadamu hata afanyaje hawezi kuushinda ufalme wa ibilisi kama hana Mungu, atatawaliwa tu na falme hizo mbili, na ndio maana shetani naye alikuwa na ujasiri wa kujigamba mbele ya Yesu na kumwambia hivi vyote ni vyangu nami humpa yeyote nimtakaye na huku sisi tunajua kuwa dunia na vyote viijazavyo ni mali ya Mungu. Unadhani shetani alikuwa anajisifia bure?, hapana kwasababu ufalme wake ni kweli una nguvu zaidi ya ufalme wa wanadamu..Hivyo alikuwa na haki ya kusema vile. Hali kadhalika ule ufalme ulio dhaifu hauwezi kuelewa mambo yanayoendelea katika ufalme ulio juu yake wenye nguvu hata uwe na bidii kiasi gani.

Hivyo ufalme wa ibilisi hauwezi kujua lolote linaloendelea katika ufalme wa Mungu, hata atafute kiasi gani hawezi kujua chochote.

Sasa Tukirudi kwenye swali lililoulizwa Je!Mungu anaweza kuleta majibu kupitia nguvu za giza maana nashindwa Kuelewa ninaposoma habari za mfalme Sauli .kupata majibu kwa mwanamke .mwenye pepo.nisaidie hapo.

Jibu ni Ndio Mungu anaoweza kuleta majibu sio tu kupitia ufalme wa giza, bali pia kupitia ufalme wa kibinadamu, Kwasababu yeye yupo mahali popote,.kama hapo juu anavyosema “Kama ningepanda mbinguni, Wewe uko; Ningefanya kuzimu kitanda changu, Wewe uko.9 Ningezitwaa mbawa za asubuhi, Na kukaa pande za mwisho za bahari; 10 Huko nako mkono wako utaniongoza, Na mkono wako wa kuume utanishika".


Lakini yeye kuwa uwezo huo wa kupitisha ujumbe wake kupitia falme hizo zote mbili haimaanishi kuwa unampendeza au umemfikia Mungu kinyume chake ni hukumu inafuata…Pia hiyo haimaanishi kuwa mtu anapokwenda kwa mganga kumtafuta Mungu atamwona, kumbuka wote wanaokwenda kwa waganga hawana lengo la kumtafuta Mungu, hakuna hata mmoja, huwa wanakwenda kutafuta njia za kutatuliwa matatizo yao na wala sio kumtafuta Mungu,kama wangekuwa na lengo la kumtafuta Mungu wasingedhubutu kutumia njia hizo ambazo wanajua kabisa Mungu amezikataa. Hata Sauli mwenyewe hakwenda kumtafuta Mungu kule kwa mganga,bali samweli amsaidie kutatua ufumbuzi wa shida iliyo mbele yake..

Na ndio huko huko Mungu wakati mwingine anatokea kuzungumza na watu, na ikishafika hatua kama hiyo basi ujue kuwa kinachofuata ni hukumu tu kwa kwenda kinyume na mapenzi ya Mungu.

Hata wachawi wenyewe huwa wanakutana na sauti ya Mungu huko huko katika shughuli zao zikiwaonya matendo yao, lakini hawawezi kusema siri hizo wanazo wao wenyewe, wale ambao wanakuja kuokolewa ukiwauliza watakuthibitishia hilo kwamba kuna wakati Fulani ambao Mungu alishawahi kuwaonya.

Sio tu Sauli alikwenda kwa waganga..Yupo ambaye alikuwa ni mchawi kabisa biblia inamtaja naye ni Balaamu, nabii wa uongo, huyu naye Mungu alikuwa anazungumza naye akimwonya asiwalaani Israeli, lakini yeye hakusikia sauti ile ya Mungu akatia ukwazo kwa wana wa Israeli, Mungu baadaye akaja kumuua.

Hivyo huo uwezo Mungu anao,lakini sio njia Mungu anayoitumia kuleta majibu ya maombi wa watu. Njia yoyote nje ya Yesu Kristo, yaani njia ya sanamu, njia ya uganga, njia ya sayansi, hakuna hata moja yenyewe uwezo wa kufikisha maombi kwa Mungu, wala usijaribu kufanya hivyo utaangukia hukumu, isiyoponyeka. japo Mungu anaweza kuzitumia hizo kuleta majibu kwa watu tena majibu yaambatanayo na hukumu wala sio jambo jema.

ubarikiwe.
 SWALI 2: Ndugu zangu kwenye biblia kuzaliwa kwa mtu Utaratibu wa Mungu ni mimba inatungishwa kwenye TUMBO LA UZAZI LA MWANAMKE. Swali ni kwamba mtu anayetungisha mimba kwenye "CHOMBO(CHUPA)MAABARA",Huyu ana hatia mbele za Bwana Mungu?
JIBU: Kwanza ni muhimu kufahamu nini maana ya watoto wa kwenye chupa...ikitokea mama anakuwa ana mayai lakini anapata shida kushika mimba huwa kuna uwezekano wa kuyatoa mayai yake kutoka kwenye uzazi na kuyaweka kwenye kifaa maalum kinachoitwa test tube au kwa kiswahili chupa, sasa wakishaliweka hilo yai la mwanamke mule huwa wanachukua mbegu za mwanamume na kuziweka kule kitaalamu ili kurahisisha lile yai kurutubishwa kirahisi...na baada ya lile yai kurutubishwa ndani ya ile chupa wanalichukua lile yai na kulirudisha kwenye tumbo la yule mama na kuendelea na hatua nyingine za ukuaji wa yule mtoto kwenye tumbo la mama yake...hiyo ndio maana ya mtoto wa kwenye chupa, sio kwamba yule mtoto anawekwa kwenye chupa maisha yake yote hapana....ni yai tu ndio linalorutubishiwa kule na kurudishwa mahali husika…kwahiyo hakuna mazingira yoyote nje na tumbo la mama mtoto anaweza kukua..wanadamu hawajafikia huo uwezo. Tumbo la mama ndio sehemu pekee mtoto anaweza kukua mpaka kufikia hatua ya kuzaliwa.

Sasa tukirudi kwenye swali je! ni dhambi yai kurutubishiwa kwenye chombo hicho maalumu nje na tumbo la mama?? Jibu ni kwamba Mungu anaangalia nia ya mtu kufanya vile ni ipi, wengi wanaofanya hivyo unakuta wana matatizo ya kutokushika mimba, kwahiyo njia rahisi wanayoshauriwa na madaktari ni kutumia hiyo njia, hivyo sio dhambi kwasababu nia yao ni kutafuta mtoto sio kuua mtoto. Na hatua hiyo ya kurutubisha yai kwenye chupa ni hatua ya awali kabisa hata mtoto hajaanza kutengenezwa. Ingekuwa kufanya hivyo ni dhambi basi pia kuzaa kwa operation ingekuwa ni dhambi kwasababu sio njia ya asili Mungu aliyoiumba kwa kuzalia watoto. Kwahiyo inategemea na sababu ya mtu kufanya hivyo ni nini?, kama mtu anafanya kwa nia nyingine tofauti na hiyo basi ni dhambi, Lakini ingekuwa ni vizuri zaidi kumtegemea Mungu kuliko madaktari yaani kumwamini Mungu kuliko kutafuta njia mbadala, lakini pia hatuna imani zinazofanana…wako wenye imani kuwa Mungu atawapa watoto pasipo njia hizo na wapo wasio na imani hiyo…Lakini mtu akitumia hiyo njia hafanyi dhambi endapo tu atakuwa na nia njema.

 SWALI 3: Napenda kujua maana na tofauti kati ya MYUNANI, MFARISAYO NA MSADUKAYO.

JIBU: Mafarisayo na Msadukayo chimbuko lao ni moja dini zao zimeegemea katika Torati ya Musa, wote hawaamini maagizo mengine nje ya torati isipokuwa tofauti inakuja katika kuamini kiama cha wafu.. Mafarisayo wanaamini kuwa kuna kiama cha wafu (yaani maisha baada ya kufa, wanaamini yote yaliyoandikwa katika torati hata tumaini ya kuja kwa Masihi duniani) lakini masadukayo hawaamini kama kuna kufufuliwa kwa wafu, wanaamini kuwa mtu akishakufa, amekufa hakuna chochote baada ya hapo, wala hakuna malaika wala ulimwengu wa roho wala mbingu.

Ukisoma Mathayo 22:24-34 utaona Bwana Yesu akiwajibu hao mafarisayo kuhusu mitazamao wao hafifu ya maandiko Na kuwaambia kuwa Mungu asingesema yeye ni Mungu wa Ibrahimu, na Isaya na Yakobo kama watu hao ni wafu sasa. Kwasababu siku zote Mungu si Mungu wa wao bali wa wanaoishi..Hivyo Neno hilo linathibitisha kuwa kiama kipo.

Ukisoma tena Matendo 23 Utaona Mtume Paulo akiyagonganisha madhehebu hayo mawili.

Matendo 23: 23.6 Paulo alipotambua ya kuwa sehemu moja ni Masadukayo, na sehemu ya pili ni Mafarisayo,
akapaza sauti yake katika ile baraza, Ndugu zangu, mimi ni Farisayo mwana wa Farisayo; mimi
ninahukumiwa kwa ajili ya tumaini la ufufuo wa wafu.
23.7 Alipokwisha kunena hayo palikuwa na mashindano baina
ya Mafarisayo na Masadukayo,
mkutano ukafarakana.
23.8 Kwa maana Masadukayo husema ya kwamba hakuna kiyama wala malaika wala roho; bali
Mafarisayo hukiri yote.
23.9 Pakawa na makelele mengi. Waandishi wengine wa upande wa Mafarisayo wakasimama,
wakateta
, wakisema, Hatuoni uovu wo wote katika mtu huyu; bali ikiwa roho au malaika amesema
naye, ni nini?
23.10 Ugomvi mkubwa ulipotokea, yule jemadari akachelea Paulo asije akararuliwa nao, akaamuru
askari washuke na kumwondoa kwa nguvu mikononi mwao, na kumle
ta ndani ya ngome.”

Hivyo kwa maandiko hayo utapata kuelewa tofauti ya watu hawa ipo wapi..

MYUNANI: Sio dini au imani, bali ni watu wa taifa la uyunani, kwasasa ni Ugiriki.Hivyo katika agano jipya mahali popote anapotajwa myunani, linalenga watu wa aina mbili, aina ya kwanza ni aidha wayahudi wanaotokea katika nchi za wayunani, na hivyo wanajulikana kama wayunani lakini kiasili ni wayahudi, kwa mfano wale watu waliotaka kumwona Bwana zamani zile ni wayahudi lakini sio wa kuzaliwa Israeli. tunasoma:.

Yohana 12:20 Palikuwa na WAYUNANI kadha wa kadha miongoni mwa watu waliokwea kwenda kuabudu kwenye sikukuu.21 Basi hao walimwendea Filipo, mtu wa Bethsaida ya Galilaya,wakamwomba, wakisema, Bwana, sisi tunataka kumwona Yesu

Unaona? Kadhalika pia wale watu waliokuwa Yerusalemu siku ile ya Pentekoste, (Matendo 2) wakishangaa matendo makuu ya Mungu, biblia inasema walikuwa Warparthi na Wamedi na Waelami,n.k. wote hawa hawakuwa watu wa mataifa mengine (yaani watu wasio wayahudi) hapana bali walikuwa ni Wayahudi waliotoka katika hayo mataifa yaliyotajwa hapo,
Na aina ya pili: ni Wayunani ambao asili yao ni Uyunani kabisa, watu wa mataifa. Mfano tunaweza kumwona mwanamke huyu aliyezungumziwa hapa ni myunani lakini hana uyahudi wowote ndani yake:

Marko 7:24 “Akaondoka huko, akaenda zake hata mipaka ya Tiro na Sidoni. Akaingia katika nyumba,akataka isijulikane na mtu; lakini hakuweza kusitirika.
25 Ila mara mwanamke, ambaye binti yake yuna pepo mchafu, alisikia habari zake,
akaja akamwangukia miguuni pake.
26 Na yule mwanamke ni Myunani, kabila yake ni Msirofoinike. Akamwomba amtoe pepo katika
binti yake.
27 Akamwambia, Waache watoto washibe kwanza; maana si vizuri kukitwaa chakula cha watoto,
na kuwatupia mbwa.
28 Naye akajibu, akamwambia, Naam, Bwana, lakini hata mbwa walio chini ya meza hula makombo ya watoto.
29 Akamwambia, Kwa sababu ya neno hilo, enenda zako, pepo amemtoka binti yako.
30 Akaenda zake nyumbani kwake, akamkuta yule kijana amelazwa kitandani, na yule pepo
amekwisha kumtoka.”

Kadhalika tunaona watenda kazi wa Mungu wengine kama Tito, mwanafunzi wa Paulo (Wagalatia 2:3).Na Timotheo (Matendo 16:1) hawa wote biblia inawataja kama ni Wayunani, na sio wayahudi.

No comments:

Post a Comment