"Tazama, naja kama mwivi. Heri akeshaye, na kuyatunza mavazi yake, asiende uchi hata watu wakaione aibu yake...ufunuo 16:15"

Saturday, October 22, 2016

CHAPA YA MNYAMA

Ndugu William Branham alifundisha sana, kuhusu chapa ya mnyama, alisema kuwa kuipokea chapa ya mnyama ni kuukataa muhuri wa Mungu ambao ni Roho Mtakatifu, alisema kuna pande mbili tu, upande wa Mungu na upande wa shetani, hivyo ukikosa kuwa na Roho wa Mungu, maana yake ni una roho ya shetani nayo ndiyo chapa ya mnyama.

Kwahiyo roho ya mpinga kristo ambayo ndani yake imebeba chapa ya mnyama iliyozungumziwa kwenye kitabu cha ufunuo 17:1-6 tusome..


 " Akaja mmoja wa wale malaika saba, wenye vile vitasa saba, akanena nami, akisema, Njoo huku, nitakuonyesha hukumu ya yule kahaba mkuu aketiye juu ya maji mengi; 2 ambaye wafalme wa nchi wamezini naye, nao wakaao katika nchi wamelevywa kwa mvinyo ya uasherati wake.
3 Akanichukua katika Roho hata jangwani, nikaona mwanamke, ameketi juu ya mnyama mwekundu sana, mwenye kujaa majina ya makufuru, mwenye vichwa saba na pembe kumi.
4 Na mwanamke yule alikuwa amevikwa nguo ya rangi ya zambarau, na nyekundu, amepambwa kwa dhahabu, na kito cha thamani, na lulu, naye alikuwa na kikombe cha dhahabu mkononi mwake, kilichojawa na machukizo, na machafu ya uasherati wake.
5 Na katika kipaji cha uso wake alikuwa na jina limeandikwa, la siri, BABELI MKUU, MAMA WA MAKAHABA NA MACHUKIZO YA NCHI.
6 Nikamwona yule mwanamke amelewa kwa damu ya watakatifu, na kwa damu ya mashahidi wa Yesu. Nami nilipomwona nikastaajabu ajabu kuu".


Habari hii inamwonyesha mwanamke aliyeketi juu ya mnyama mwekundu sana, na juu ya paji la uso wake, alikuwa na jina limeandikwa la siri, BABELI MKUU, MAMA WA MAKAHABA, NA MACHUKIZO YA NCHI, 

Sasa huyu mwanamke anayezungumziwa katika sura hii, ni KANISA fulani kwasababu mwanamke siku zote katika biblia anawakilisha kanisa, na pia mwanamke huyu tunaona anaitwa MAMA WA MAKAHABA, Hii ikiwa na maana kwamba ni kanisa-kahaba mama, na ikiwa ni "mama" basi ana "MABINTI", na hao mabinti ni makahaba kama mama yao  alivyo. Kwahiyo kahaba ni mwanamke anayezini na wanaume wengi mbali na mume wake. Na tunaona kuwa kanisa pekee lililofanya uasherati kwa kuchanganya mafundisho ya Mungu na mafundisho ya kipagani ni kanisa Katoliki, Hivyo basi yule mama wa makahaba aliyezungumziwa pale ni kanisa Katoliki, Na wale mabinti ni madhehebu mengine yote ya dini yaliyobakia, yaliyoacha uongozi wa Roho Mtakatifu na kuiga desturi zile zile za kipagani kama za mama yao kahaba yaani kanisa katoliki. Na sasa hivi tunaona madhehebu yote ulimwenguni na dini zote ulimwenguni zinaungana, pamoja na mama yao mkuu kahaba katoliki (ecumenical council) na KUIUNDA ILE CHAPA YA MNYAMA.

CHAPA YA MNYAMA INATENDA KAZI KWA NAMNA MBILI:
Chapa ya mnyama ipo rohoni na mwilini, (nje na ndani). kwa NDANI ni kama hauna Roho Mtakatifu, umeshaipokea ile chapa ya mnyama, kwahiyo ndugu tafuta kuwa na Roho wa Mungu angali muda upo, maana biblia inasema huo ndio muhuri wa Mungu, (soma waefeso 4:30). Na pia kuipokea chapa ya mnyama kwa NJE ni kama upo au umejiunganisha au umejifunga  na mifumo yote ya madhehebu ambayo yameuacha uongozi wa Roho Mtakatifu, na kuweka mifumo ya kipagani, pamoja na taratibu za kibinadamu na desturi zisizoendana na NENO la Mungu. hivyo kuipokea chapa ya mnyama ni kujishona na madhehebu na kuwa na utambulisho mwingine wowote nje ya UKRISTO mfano, kujitambulisha kama mlutheri, mwanglikana, msabato,mbaptisti, mkatoliki, mbranhamite n.k. badala ya kujitambulisha kama MKRISTO. (kumbuka maana ya haya majina sio mbaya, lakini madhehebu ambayo yamebeba hayo majina yana ile chapa ya mnyama ndani yake kwasababu yameshafanya uasherati kama wa mama yao katoliki, na Mungu ameyakataa soma ufunuo 3:1 " ...Nayajua matendo yako, ya kuwa una jina la kuwa hai, nawe umekufa. ")  kwahiyo kwa kujiita tu hivyo tayari umeshakwisha kubaliana na ile chapa bila ya wewe mwenyewe kujijua. Fikiria tu hili kama sisi sote ni WAKRISTO huo utambulisho mwingine unatoka wapi?. Ujue tu unatoka kwa mpinga kristo ambao mwisho wake unapelekea kuiunda ile alama ya mnyama. Na nguvu ya hii chapa itakuja kujidhihirisha sana katika kipindi cha dhiki kuu, baada ya kanisa (bikira safi)  kunyakuliwa.

Kwahiyo hii chapa ya mnyama kwasasa ipo sana katika roho na watu wanaendelea kuipokea kwa kukosa Roho Mtakatifu, lakini kwa nje, ipo wanakubaliana nayo ila itakuja kutenda kazi kwa Nguvu katika kipindi cha dhiki kuu. pale mpingakristo atakaponyanyuka na kupewa mamlaka juu ya ulimwengu mzima, na huyu mpinga kristo atakuwa sio mwingine zaidi ya Papa kiongozi wa kanisa katoliki wa Roma. Sio kwamba wakatoliki ni watu wabaya, Hapana ni watu wazuri wote bali ni vizuri kujua roho inayoliendesha kanisa katoliki ni roho ya mpinga kristo na haitokani na Mungu, Hivyo watu wa Mungu lazima waujue ukweli watoke huko.

Tunaweza tukaona leo hii, mambo  mengi ya ajabu, yakitokea ulimwenguni ikiwemo vitendo vya kigaidi vikizidi  kukithiri, amani inazidi kutoweka duniani,watu wanaishi kwa hofu za machafuko na vita, siasa na umoja wa mataifa umeshindwa kuihifadhi amani ya dunia, dunia inatafuta suluhisho la mambo hayo na bado haijapata, hivyo anatafutwa kiongozi atakayeonekana ana uwezo wa kurejesha amani duniani  naye atakuwa si mwingine zaidi ya PAPA ili maandiko yatimie. Kama tunavyomwona leo hii anajulikana ulimwenguni kote kama mtu wa amani(MAN OF PEACE). Hivi karibuni tunaweza tukaona jinsi kiongozi huyu wa kanisa Katoliki (papa Francis), akirejesha mahusiano kati ya Marekani na Cuba, ambayo yalikuwa yamevunjika kwa muda mrefu. Leo analeta dini zote ulimwenguni pamoja, anakubalika na kuheshimika na watu wote, Ni kiongozi mwenye ufuasi mkubwa wa watu kushinda kiongozi yeyote ulimwenguni.
                                      (papa akiwa na viongozi wa dini mbalimbali duniani)

Kwahiyo katika kipindi cha ile dhiki kuu, atakuja na wazo la kukomesha ugaidi na vitendo viovu duniani akitaka watu wote, wasajiliwe kulingana na madhehebu yao na mashirika yao ya dini, kwasababu vitendo vinavyosababisha amani kutoweka vinasababishwa na dini na ndivyo ilivyo. kwahiyo ni lazima tatizo litatuliwe kwa namna ya KIDINI na si vinginevyo. Hivyo itahitaji kiongozi wa kidini na hakuna mwingine anayekidhi hivi vigezo zaidi ya Papa kiongozi wa kanisa katoliki.

 Leo hii duniani vita vya kidini vimeiweka dunia katika mtazamo mpya, mfano mabomu ya kujitoa muhanga, na vikundi vya kigaidi, kama ISIS, Alqaeeda, Alshabaab, Boko haram Anti-balaka, LRA n.k.vimekuwa ni tatizo sugu kwa dunia nzima, ni mada iliyopo mezani kila siku sio kwa mataifa maskini wala matajiri wote wamevamiwa na tatizo hili .Hivyo kiongozi huyu atapewa nguvu kwa kujipendekeza (danieli 11:21), Jambo hili  litatimiza ule unabii wa Daniel 9:27 "Naye atafanya agano thabiti na watu wengi kwa muda wa juma moja;..... " Agano hili la amani litafurahiwa na dunia nzima, kwani litadhaniwa kuwa litaleta amani duniani, 

Hapo ndipo utakapowekwa utaratibu mpya wa ulimwengu (NEW WORLD ORDER). chini ya uongozi wa papa (mpinga kristo)  baada ya kupewa nguvu na mataifa yote duniani kumbuka hatajiita mpingakristo wala hatakuwa na uso wa shetani, wala usidanganyike kama atakuwa freemason au illuminati, au kikundi chochote cha kichawi hapana bali ATATOKEA NDANI YA KANISA ni mtu anayekubalika na watu, anaonekana mpenda amani, anapenda dini, anajali watu wote wa dini zote, anabusu watoto na zaidi ya yote ataonekana ni mnyenyekevu kuliko watu wote duniani, lakini ndani yake ni SHETANI katika utendaji kazi wake. Biblia inasema "Na hao wakaao juu ya nchi, wasioandikwa majina yao katika kitabu cha uzima tangu kuwekwa misingi ya ulimwengu, watastaajabu wamwonapo yule mnyama, ufunuo17:8"

 Kumbuka shetani ananyanyua sasa hivi kwa kasi vikundi vya kuvunja amani na ugaidi duniani kama mbinu yake ya sasa ya kutafuta kuwaangamiza wakristo, kama alivyofanya kwa wakristo katika kanisa la kwanza kwenye utawala ule ule wa KIRUMI chini ya Nero (AD 64),ambapo wakristo wengi waliuawa baada ya kusingiziwa kuwa wameuchoma mji, na ANGALI sio wao waliofanya hivyo. Na kwa njia kama hiyo hiyo shetani anawatafuta wakristo leo hii awaangamize, kwa vitu vya KUSINGIZIWA, maana anajua hakuna namna yeyote mkristo anaweza akashitakiwa na kuuawa kwa makosa yeyote ya kihalifu kwasababu wakristo sikuzote wanaishi maisha ya haki. Hivyo sasa hivi ameunyanyua ugaidi katika uislamu na vikundi vingine kama anti-balaka, ISIS, alshabaab,Boko Haramu, Al-qaeda, Hizbolah,Ku klax klan, pamoja na vikundi vyote vya siri vinavyouchafua ulimwengu, ili baadaye aweze kuwasingizia wakristo kwa urahisi kuwa wao ndio magaidi na kuwaangamiza wote).


                             (wakristo wasingiziwa kuuchoma mji, kusababisha wapitie dhiki kubwa ya                                                kuuawa  kikatili dhidi yao chini ya utawala wa Nero AD 64)
      
Hivyo basi utaratibu huo mpya utakapokuja watu wote watapaswa wahakikiwe taarifa zao muhimu zinazohusiana na DINI ZAO, itahusisha pia na kazi mtu anayofanya, kwenye makampuni, na mashirika. Kila mmoja ni lazima atambuliwe yeye ni dhehebu gani au dini  gani katika shughuli anayoifanya kwa dhumuni la kuwapata watu wachafuaji wa amani duniani, kwamfano waislamu wenye itikadi kali, wanaojihusisha na vikundi vya kigaidi, pamoja na vikundi vya kihalifu vinavyohusisha vita vya kidini na mauaji ya kikatili ya watu watambulike na kukamatwa. Lakini nia ya shetani itakuwa sio kuleta amani wala kuwalenga waislamu au makundi mengine  BALI NI KUWALENGA WAKRISTO,  (kama ilivyotokea kwenye utawala wa NERO,)

Lakini wale ambao hawatakubaliana kujiunga na huo mfumo wa yule mnyama ambao ni MUUNGANIKO WA MADHEHEBU NA DINI ZOTE. Mtu huyo hataweza kuuza wala kununua wala kuajiriwa asipokuwa na huo utambulisho, Hataruhusiwa kuabudu kwenye kanisa ambalo halijasajiliwa na muungano wa madhehebu, ndugu Branham alitabiri akasema itafika wakati haya makanisa tuliyonayo sasa yatafungwa yote.kwahiyo huu usajili utaanza karibu duniani kote, katika kila nyanja na kila taasisi, kwa waajiriwa na wasio waajiriwa, katika vitambulisho vya taifa,kura na serikalini na taasisi binafsi kama mabenki, ATM cards, VISA n.k. na sehemu nyingine zitatumika MICRO-CHIPS sana sana kwa mataifa yaliyoendelea.

 Itakuwa ni sheria kila raia lazima ahakiki taarifa zake za kidini, na huo mfumo mpya. watu wengi wataukubali na kuupenda na kuhakiki taarifa zao pasipo kujua kuwa ndio wanaipokea ile chapa ya mnyama, na mfumo huo utafanikiwa kukamata wahalifu wengi.Ni wazi kuwa itakuwa ni ngumu kwa mtu kufanya biashara yeyote ya kuuza wala kununua wala kuajiriwa usipokuwa na huo utambulisho wa kidini. kwahiyo ukishahakikiwa taarifa zako utakuwa huru kufanya shughuli yako yoyote unayotaka.lakini sio kujiita MKRISTO tu! haitafanya kazi tena kipindi hicho, huko kutakuwa ni kuonyesha tu ID au CHIP ambayo imebeba taarifa zako zilizohakikiwa na huo mfumo mpya wa mpingakristo,

 Tazama mwenyewe video hii hapa chini, Papa akizungumza juu ya jambo hili ya kwamba kuwa mkristo ni lazima uwe mshirika wa kanisa fulani (dhehebu)..je! Ni nyakati gani hii tunaishi??




Lakini wale wakristo watakaokuwepo watamtambua yule mpingakristo na chapa yake, watakataa kuupokea huo utambulisho na usajili wake (chapa ya mnyama). Sasa hao ndio watakaotafutwa na kuitwa magaidi, na hao tu ndio watakaopitia dhiki kuu wakati dunia inaendelea kufurahi. Na hawa hawatauliwa ovyo ovyo tu, kama inavyodhaniwa. bali watachukuliwa na serikali,(maana serikali itawatambua kama wahalifu na sio raia wa kawaida kwa maana serikali itashirikiana na mpingakristo kufanya kazi). Maana hawatakuwa wengi, na watapelekwa kwenye magereza maalumu ya mateso ya siri (concentration camps), huko ndiko kutakuwa na dhiki kuu ambayo haijawahi kutokea wala haitakaa itokee kama Bwana YESU KRISTO alivyosema. 

Wakristo wengi watateswa kama magaidi, watasingiziwa wao ndio wanaoharibu amani ya dunia kama sivyo kwanini wakatae kusajiliwa, lazima kuna mambo ya siri wanayo. watakataliwa na jamii nzima, hata ndugu za hao jamaa hawatawaelewa.Hapo ndipo ndugu atamsaliti ndugu ili auawe, Tunaona kama vile wayahudi walivyofanyiwa na Adolf Hitler katika vita ya pili ya dunia kwenye zile concentration camps. watu jinsi walivyokuwa wakiuliwa kikatili na mateso makali yasiyoelezeka ndivyo itakavyokuwa tena na zaidi ya hapo katika wakati wa dhiki kuu kwa wakristo , mpinga kristo atawaua wote, (Na dhiki hii kuu itawahusisha na wayahudi pia) na itadumu kwa muda wa miaka mitatu na nusu ya mwisho wa lile juma la 70 la Danieli. Na kwa mataifa yote yaliyobaki ambayo yamepokea ile chapa (yaani kwa kuukubali mfumo na utambulisho wa yule mnyama katika vitambulisho vyao na ID, na CHIP zao na vyeti vyao). wataingia katika ile siku ya KUOGOFYA ya BWANA ambayo itaanza mara tu baada ya ile miaka mitatu na nusu kuisha (baada ya dhiki kuisha),hapo ndipo hukumu ya mataifa itakapoanza.
                                    (wayahudi katika mateso kipindi cha utawala wa Hitler)


USHUHUDA WETU:
kuna ushuhuda tungependa kukushirikisha kwa uhakika zaidi na uhalisia wa hili jambo.
Sisi wawili mwezi wa 4 mwaka 2015...Tulipokuwa tunaishi kule kigamboni,  tulikuwa na rafiki yetu muislamu alikuwa yupo na mpenzi wake ambaye ni mkristo wanaishi pamoja, siku moja ya mkesha wa pasaka, walituomba tuwasindikize kanisani kwenye mkesha wa maigizo ya pasaka. Hilo kanisa lilikuwa ni kanisa kubwa maarufu la katoliki. kwa kuwa ilikuwa ni usiku, hawakujua shortcut ya kufika pale kwahiyo walituomba sisi tuwapeleke kwasababu sisi tu ndio tulikuwa tunaifahamu shortcut ya kufika pale. Basi tulienda tukawafikisha hadi getini tukawaingiza ndani, wakati sisi tumeachana nao tunatoka nje getini. Walinzi wa geti wakatusimamisha wakaanza kutuhoji, kwanini mnaondoka kabla ya ibada kuisha, sisi tukawaelezea tumewaleta tu ndugu zetu na kuondoka.hatujaja kwenye ibada. kulikuwa na mmoja ambaye ni kiongozi wa kanisa lile mahali pale akaja karibu, akatuuliza nyie ni dhehebu gani? ..Tukamwambia sisi hatuna dhehebu sisi ni wakristo. kitendo cha sisi kusema tu vile, tuliwasha moto, wakaitana wengine, wakaanza kutushambulia kwa maneno mengi, nikizungumza yote hapa muda hautatosha. tulikuwa tunajaribu kuwajibu kulingana na NENO kuwa ukristo sio madhehebu, bali ni kuamwamini YESU KRISTO. Lakini jinsi tulivyozidi kuwaeleza ndivyo walivyozidi kutushambulia na kutukasirikia. kulikuwa na vijana wengine pale, wakawaachia wote wapate nafasi ya kutugeukia sisi.Walikuwa hawana nia nyingine bali kusikia kutoka katika vinywa vyetu sisi ni madhehebu gani lakini tulipokataa kufunua madhehebu bali ukristo ndipo vita vilipoanza, saa hiyo hiyo tulipigwa pingu. tukakalishwa chini, defender ya polisi ikaitwa, simu ilipigwa kituoni wakisema tumewakamata ma-alshababu, tukafikishwa kituoni, tukapigwa na makuni, tukasingiziwa kwanini tumeiba,wakatutupa ndani gerezani, wafungwa kule, walidhani sisi ni magaidi wa ajabu kwajinsi tulivyokuwa tunapigwa, ile alfajiri walitudekisha lile gereza,.Lakini Mungu alitupa neema asubuhi alfajiri sana tukatoka kule, hiyo siku tukio hilo lilipotokea ilikuwa ni siku ya kupatwa kwa mwezi, (maarufu kama bloodmoon duniani), hiyo ilikuwa ni uthibitisho wa somo Mungu alilotufundisha. Lakini kwanini tulifikia mpaka huku magerezani na kupigwa? jibu ni dhahiri ni kwasababu tuliukiri UKRISTO na sio madhehebu, shetani hapendi kuona mtu anaukiri UKRISTO anatamani uendelee hivyo hivyo kujitambulisha kwa madhehebu yako ili iwe rahisi kwako baadaye kuipokea ile CHAPA YA MNYAMA.

Kwahiyo Baada ya tukio hilo ndipo Mungu alituthibitishia hili somo. jinsi wakristo watakavyokuja kupitia katika dhiki ile kuu. Kanisa Katoliki ndio linaloongoza kwa kuwaua na kutesa wakristo wengi, na inakadiriwa kuua zaidi ya wakristo milioni 68 katika historia ya kanisa. Na ndivyo linavyofanya hata sasa kwa siri na litakavyokuja kufanya katika kile kipindi cha dhiki kuu ambacho kipo karibuni kuanza. Na ndio maana yule mwanamke aliyeonekana kwenye ufunuo 17 alionekana amelewa kwa damu ya watakatifu. Kuna wakristo wengi wanaoteswa na kuawa kwa siri duniani kote, kwa ajili tu wao ni wakristo na sio jambo lingine.
Shetani hapendi kuona mtu anajiita MKRISTO, kama vile asivyopenda kuona watu wakibatizwa kwa jina la YESU KRISTO, na ndivyo asivyopenda kumwona mkristo anautambulisho wa asili wa KUMKIRI KRISTO, Hakuna mahali popote mkristo katika biblia alikuwa anajiita mpaulo au mpetro au m-yohana mbatizaji, au m-eliya au m-timotheo, biblia inasema wote walikuwa wanaitwa wakristo. Kwahiyo utambulisho mwingine zaidi ya huo unatoka kwa shetani, na hiyo ndiyo chapa ya mnyama yenyewe. amina.

KUHUSU 666
Papa akiwa kama kiongozi wa kanisa katoliki ana nembo katika enzi yake inayojulikana na kusomeka kama VICARIUS FILII DEI. tafsiri  yake kwa kiswahili ni  "BADALA YA MWANA WA MUNGU."
 kwahiyo papa kulingana na kanisa katoliki anasimama hapa duniani badala ya mwana wa Mungu, anauwezo kama vile, kusamehe dhambi, kubariki, na kusujudiwa n.k.
Haya ni machukizo mbele za Mungu,. Na hesabu ya hilo jina, kwa kirumi  ni 666. unaweza ukaona hesabu yake hapa chini.


kwahiyo kutiwa chapa katika mkono wa kuume au kwenye kipaji cha uso, ni kukubaliana na ule mfumo kichwani kwako,(hiyo ni kwenye kipaji cha uso) na kukubali kuutumia huo mfumo kama kitu cha kujipatia riziki au chakula (hiyo ni kwenye mkono wa kuume) tunafahamu kama vile mkono tunautumia kwa kula, kukubaliana na kitu, kusaini mikataba n,k  kwa wale watakaokubali kuuza na kununua ndio watapokea hiyo chapa (666). Kumbuka hii 666 ni namba inayomtambulisha mpingakristo na chapa yake, na sio chapa yenyewe. 

TAFUTA ROHO MTAKATIFU, EPUKA KAMBA NA UTAMBULISHO WA MADHEHEBU.

ukiulizwa wewe ni dhehebu gani, sema mimi ni mkristo usione haya Bwana Yesu alisema katika marko 8:38"Maana kila mtu atakayenionea haya mimi, na maneno yangu, katika kizazi hiki cha uzinzi na dhambi, Mwana wa Adamu atamwonea haya mtu huyo, atakapokuja katika utukufu wa Baba yake pamoja na malaika watakatifu". Uvae ukristo umfuate Yesu usiuvae udhehebu utakupeleka jehanum.

Bwana Yesu anasema mathayo 16:24-26 "Wakati huo Yesu aliwaambia wanafunzi wake, Mtu ye yote akitaka kunifuata, na ajikane mwenyewe, ajitwike msalaba wake, anifuate. Kwa kuwa mtu atakaye kuiokoa nafsi yake, ataipoteza; na mtu atakayepoteza nafsi yake kwa ajili yangu, ataiona. Kwani atafaidiwa nini mtu akiupata ulimwengu wote, na kupata hasara ya nafsi yake? Au mtu atatoa nini badala ya nafsi yake?."

Tubu ndugu mgeukie Mungu haya mambo yote, yatatokea kizazi tunachoishi sisi, unaona jinsi gani MPINGAKRISTO kashaweka mambo yake yote tayari, ni kutekeleza tu! mambo yaishe. YESU KRISTO YUPO MLANGO KURUDI, MUDA UMEENDA SANA KUSHINDA  UNAVYOFIKIRI.

MUNGU AKUBARIKI!

4 comments:

  1. Ameeeeeeeeeeeen mda umeenda kweli kweli,,, MUNGU atusaidie tujue tumesimama wap na tuko wakati gan

    ReplyDelete
  2. Jaman Ujumbe mzuri kweli kweli,,, ni kusimama nao na kuomba Roho Mtakatifu ambaye Ndo muhuri ,, Bwana yesu Kristo akubariki Kwa Ujumbe mzuri

    ReplyDelete
  3. Amina sana mbarikiwe

    ReplyDelete
  4. hatima ya Binadamu anayo Mungu baba pekee, mamlaka nazo ameziweka na pia anaweza kuzisambaratisha. Imani ni Muhimu sana Kwa muumini, shika ulichonacho, amini unachokiamini.

    ReplyDelete