"Tazama, naja kama mwivi. Heri akeshaye, na kuyatunza mavazi yake, asiende uchi hata watu wakaione aibu yake...ufunuo 16:15"

Sunday, September 18, 2016

KIMBIA! KIMBIA! KIMBIA!

Makanisa yanayohubiri injili ya mafanikio tu. Na kukwambia kuwa uthibitisho wa Mungu kuwa yupo na wewe, ni kuwa tajiri ...JIHADHARI NA HILO KANISA!

Makanisa yasiyohubiri toba ya msamaha na kuwafanya watu wajione ni kawaida kuishi na dhambi zao...JIHADHARI!

Makanisa yanayochanganya NENO la Mungu na siasa na vikundi vya kijamii, jambo ambalo huwezi kutofautisha jukwaa la siasa na kanisa....JIHADHARI SANA!

Makanisa yasiyohubiri utakatifu na kufundisha watu ukweli kulingana na Biblia...KUWA MWANGALIFU NA HILO KANISA..

Makanisa yanayohubiri ujumbe wa kutoa tu, na kuacha mafundisho ya adili kama upendo, utakatifu na imani,,,,JIHADHARI KWAUSALAMA WA MAISHA YAKO YA MILELE.

Kanisa lisilokufundisha wala kugusia kujiandaa kwenda katika unyakuo...KUWA MAKINI!

Kanisa lisiloruhusu karama za Roho kufanya kazi, kama uponyaji wa kiungu, unabii, lugha, miujiza n.k. jua hilo kanisa limekufa au lipo karibuni kufa. JIHADHARI NDUGU!











 


No comments:

Post a Comment