"Tazama, naja kama mwivi. Heri akeshaye, na kuyatunza mavazi yake, asiende uchi hata watu wakaione aibu yake...ufunuo 16:15"

Thursday, July 20, 2017

MASWALI NA MAJIBU: SEHEMU YA 17

SWALI 1: Biblia inasema 1wakoritho 6:2-3 "Au hamjui ya kwamba watakatifu watauhukumu ulimwengu? Na ikiwa ulimwengu utahukumiwa na ninyi, je! Hamstahili kukata hukumu zilizo ndogo? HAMJUI YA KUWA MTAWAHUKUMU MALAIKA,basi si zaidi sana mambo ya maisha haya? " . Swali ni je! sisi tutahukumuje malaika?.


JIBU: Watakatifu wamefananishwa na BWANA wetu YESU KRISTO kwa sababu yeye aliitwaa asili ya mwanadamu na sio asili ya malaika wala kiumbe kingine chochote, maandiko yanamtaja yeye kama mzaliwa wa kwanza kati ya ndugu wengi (ambao ndio sisi), Waebrania 2: 16 " Maana ni hakika, hatwai asili ya malaika, ila atwaa asili ya mzao wa Ibrahimu.
17 Hivyo ilimpasa kufananishwa na ndugu zake katika mambo yote, apate kuwa kuhani mkuu mwenye rehema, mwaminifu katika mambo ya Mungu, ili afanye suluhu kwa dhambi za watu wake".

 Unaona hapo na kama vile Mungu alivyompa vitu vyote vya mbinguni, na vya duniani na vya kuzimu vivyo hivyo alimpa pamoja na hukumu yote (Yohana 5:22), na pia tukisoma:
Waefeso 1:20 aliotenda katika Kristo alipomfufua katika wafu, akamweka mkono wake wa kuume katika ulimwengu wa roho;
21 juu sana kuliko ufalme wote, na mamlaka, na nguvu, na usultani, na kila jina litajwalo, wala si ulimwenguni humu tu, bali katika ule ujao pia;
22 akavitia vitu vyote chini ya miguu yake, akamweka awe kichwa juu ya vitu vyote kwa ajili ya kanisa; ambalo
23 ndilo mwili wake, ukamilifu wake anayekamilika kwa vyote katika vyote. "

Kwahiyo kama Mungu amempa vyote ikiwemo na hukumu ya viumbe vyote  vya mbinguni na vya duniani, visafi na vichafu, vilivyopo na vitakavyokuja, hivyo ni dhahiri kuwa malaika wote watakatifu na walioasi wapo chini yake na watahukumiwa na yeye kulingana na njia zao, aidha ni nzuri au mbaya, kwa mfano ule ule atakavyowahukumu wanadamu wote watakatifu na waovu.Hivyo basi kama watakatifu watakuja kuketi pamoja na KRISTO (Ufunuo 3:21) ni wazi kuwa watahukumu pamoja na Kristo, maana wakati huo watasimama kama ndugu zake.
kwahiyo ndio ni kweli malaika wote watahukumiwa na watakatifu, wale malaika watakatifu watazidi kutukuzwa zaidi pamoja na  Kristo katika umilele ujao, na wale waovu (shetani na malaika zake) watahukumiwa na kutupwa katika lile ziwa la moto pamoja na wanadamu walioasi. kumbuka hizi hukumu zitafanywa na YESU pamoja na watakatifu wake tu!. Na ndio maana maandiko yanasema tutauhukumu ulimwengu na malaika wote. 

Ufunuo 20:4 inasema..." KISHA NIKAONA VITI VYA ENZI, WAKAKETI JUU YAKE, NAO WAKAPEWA HUKUMU; nami nikaona roho zao waliokatwa vichwa kwa ajili ya ushuhuda wa Yesu, na kwa ajili ya neno la Mungu, na hao wasiomsujudia yule mnyama, wala sanamu yake, wala hawakuipokea ile chapa katika vipaji vya nyuso zao, wala katika mikono yao; nao wakawa hai, wakatawala pamoja na Kristo miaka elfu. "

Kwahiyo wale tu watakaoshinda na KUKETI PAMOJA NAYE KATIKA KITI CHAKE CHA ENZI hao ndio watakaohukumu ULIMWENGU na MALAIKA. Amina.
Kumbuka watakaokuwa na mamlaka hayo ni wale watakaoshinda tu (watakaonyakuliwa)..


Kwahiyo tujitahidi tushinde maana biblia inasema..
Ufunuo 3:19-22 "Wote niwapendao mimi nawakemea, na kuwarudi; basi uwe na bidii, ukatubu.
20 Tazama, nasimama mlangoni, nabisha; mtu akiisikia sauti yangu, na kuufungua mlango, nitaingia kwake, nami nitakula pamoja naye, na yeye pamoja nami.
21 YEYE ASHINDAYE, NITAMPA KUKETI PAMOJA NAMI KATIKA KITI CHANGU CHA ENZI, kama mimi nilivyoshinda nikaketi pamoja na Baba yangu katika kiti chake cha enzi.
22 Yeye aliye na sikio, na alisikie neno hili ambalo Roho ayaambia makanisa. "

SWALI 2: Naomba kujua  watakaoenda mbinguni je! ni wengi au wachache?


JIBU: Tukisoma Luka 13:23-28"  Mtu mmoja akamwuliza, Je! Bwana, watu wanaookolewa ni wachache?
 Akawaambia,
24 Jitahidini kuingia katika MLANGO ULIO MWEMBAMBA, kwa maana nawaambia ya kwamba wengi watataka kuingia, wasiweze.
25 Wakati mwenye nyumba atakaposimama na kuufunga mlango, nanyi mkaanza kusimama nje na kuubisha mlango, mkisema, Ee Bwana, tufungulie; yeye atajibu na kuwaambia, Siwajui mtokako;
26 ndipo mtakapoanza kusema, Tulikula na kunywa mbele yako, nawe ulifundisha katika njia zetu.
27 Naye atasema, Nawaambia, Siwajui mtokako; ondokeni kwangu ninyi nyote mlio wafanyaji wa udhalimu.
28 Ndipo kutakapokuwa na kilio na kusaga meno, mtakapomwona Ibrahimu na Isaka na Yakobo na manabii wote katika ufalme wa Mungu, nanyi wenyewe mmetupwa nje. "
Ukisoma tena..Mathayo 7:13 -14 Inasema.. "Ingieni kwa kupitia mlango ulio mwembamba; maana mlango ni mpana, na njia ni pana iendayo upotevuni, nao ni wengi waingiao kwa mlango huo. Bali mlango ni mwembamba, na njia imesonga iendayo uzimani, nao waionao ni wachache. "
Maandiko hayo yanaeleza wazi kabisa kwamba watakaokolewa ni WACHACHE, kwasababu njia imesongwa sana! lakini swali linakuja je hii njia imesongwa na nini? Ni wazi kabisa imesongwa na mambo mengi  ya ulimwengu huu ambayo ni, anasa, upendaji fedha kupita kiasi, wivu, chuki,tamaa, uasherati uliokithiri ambao sasa upo mpaka kwenye mitandao mambo ambayo hapo zamani hayakuwepo, mitindo ya wanawake kutembea nusu uchi, burudani na miziki ya kidunia,ufisadi n.k. na zaidi ya yote ni kuongezeka kwa wimbi kubwa la manabii wengi wa uongo na hivyo kuifanya ile njia ya kweli isitambulike kirahisi, kwasababu imechanganyikana na njia nyingine nyingi za uongo mambo ambayo hapo nyuma hayakuwepo, na jinsi siku zinavyozidi kwenda ndivyo ile njia ya ukweli inavyozidi kuwa nyembamba zaidi, imefikia hatua ya kwamba ukristo wa leo unapimwa na kiwango cha mafanikio ya kidunia aliyonayo mtu na sio mafanikio ya kiroho (yaani utakatifu), Neno la kweli limetupwa nje!. 

Bwana Yesu Kristo aliweka wazi pale aliposema kama ilivyokuwa katika siku za Nuhu, ndivyo itakavyokuwa siku za kuja kwake mwana wa Adamu? je! katika siku za Nuhu waliokoka watu wangapi? tunaona waliokoka watu 8 tu kati ya mabilioni ya watu waliokuwepo duniani wakati ule..na tena alisema kama ilivyokuwa katika siku za Lutu ndivyo itakavyokuwa kuja kwake mwana wa Adama..je! wakati wa Lutu walipona watu wangapi?..Jibu ni dhahiri kuwa ni walipon watu 3   tu kati ya mamilioni waliokuwa wanaishi Sodoma na Gomora wakati ule. Na kumbuka Bwana Yesu hawezi kusema uongo,kizazi cha Nuhu na Lutu kimefananishwa na kizazi chetu.

 NA NI KWELI KABISA! watakaookolewa katika kizazi hiki cha mwisho tunachoishi ni WACHACHE MNO!!! Hivyo ndugu tujitahidi tuwe kati ya hao wachache watakaokolewa kwa kupita hiyo njia nyembamba iliyodharauliwa na kuchekwa na ulimwengu wote nayo ni UKRISTO ULE WA MTINDO WA KALE WA MITUME..ikiwa wewe ni mwanamke tupa nguo za kizinzi uvae kama mwanamke wa kikristo mwanamke wa kikristo havai vimini, suruali wala kaptula, hapaki wanja wala lipsticks, mwanamume wa kikristo hanywi pombe, sio mtukanaji, mkristo yoyote hapaswi kupenda mambo ya ulimwengu? Bwana Yesu alisema itakufaidia nini kuupata ulimwengu mzima na kupata hasara ya nafsi yako.? Ni wakati wa kutafuta vitu vya kimbinguni ile siku ile isitujie kama mwivi.
Muda umeenda sana tunaishi katika kizazi kibaya kushinda vyote, tuwe macho Bwana yu mlangoni kuja. Amen.


SWALI 3: Maandiko yanasema wakolosai 3:20" Ninyi watoto, watiini wazazi wenu katika mambo yote; maana jambo hili lapendeza katika Bwana. "..Lakini sehemu nyingine YESU alisema kwenye luka 14:26"Kama mtu akija kwangu naye hamchukii baba yake, na mama yake, na mke wake, na wanawe, na ndugu zake waume na wake; naam, na hata nafsi yake mwenyewe, hawezi kuwa mwanafunzi wangu. " ..Naomba ufafanuzi hapo sijaelewa heshima kwa mzazi ni ipi?.



JIBU: Biblia pia inasema Efeso 6:1 Enyi watoto, watiini wazazi wenu 'KATIKA BWANA', maana hii ndiyo haki.Waheshimu baba yako na mama yako; amri hii ndiyo amri ya kwanza yenye ahadi,Upate heri, ukae siku nyingi katika dunia. " ..

Ni kweli tunapaswa tuwatii na kuwaheshimu wazazi lakini kuna 1) utii ambao hautokani na Mungu na 2) Utii unaochukua nafasi ya Mungu..huo ndio Kristo alioukataa..kwa mfano utii usiotokana na Mungu ni kama unakuta mzazi ni mshirikina halafu anataka kukufundisha na wewe kuwa mchawi, au mzazi ni mlevi anataka na wewe uwe mlevi au mzazi anafanya biashara haramu anakulazimisha na wewe ufanye biashara haramu kwa namna hiyo basi biblia imeruhusu kutokutii na sio dhambi mbele za Mungu kwasababu inakuharibia mahusiano yako wewe na Mungu kumbuka huo mstari hapo unaposema watiini wazazi wenu, unasema hivi watiini "katika BWANA" kwahiyo ulevi, uchawi, ufisadi, uasherati, uuaji n.k. hayo sio katika Bwana, Hivyo kwa kukataa kushirikiana naye Mungu hatahesabu kama hukumtii japo yeye ataona kama hukumtii.
Na namna ya pili ni ule utii unaotaka kuchukua nafasi ya Mungu, Kwamfano mzazi anakuzuia wewe usimpokee Kristo, anakuzuia usiombe, anakuzuia usitende matendo mema, anakuzuia usiitii sauti ya Mungu kwamfano pale Mungu anapokuambia acha kufanya jambo fulani  na mzazi hataki  hapo sasa hauna budi kutupa  chini la mzazi na kuchukua la Mungu hata kama mzazi wako ana maana nzuri kiasi gani kwako hapo ndipo  Bwana YESU aliposema ASIYEMCHUKIA baba yake au mama yake hawezi kuwa mwanafunzi wangu. 

Na wengi hapa wanakwama unakuta Bwana kamwita mtu atoke katika imani fulani ya uongo inayoabudu masanamu ili amtumikie katika roho na kweli lakini kwasababu ya wazazi wake na ndugu zake ni washirika wazuri katika hiyo imani, anaamua kuwafuata wazazi wake kwa hofu kwamba atakuwa hajawaheshimu wazazi wake. Kumbuka YESU alisema adui za mtu ni watu wa nyumbani mwake mwenyewe. Huo ndio wakati wa kubeba msalaba wako na kumfuata Kristo. soma mafungu yafuatayo;..


Mathayo 10:32-38" Basi, kila mtu atakayenikiri mbele ya watu, nami nitamkiri mbele za Baba yangu aliye mbinguni.
33 Bali mtu ye yote atakayenikana mbele ya watu, nami nitamkana mbele za Baba yangu aliye mbinguni.
34 MSIDHANI YA KUWA NIMEKUJA KULETA AMANI DUNIANI; LA! SIKUJA KULETA AMANI BALI UPANGA.
35 Kwa maana nalikuja kumfitini mtu na babaye, na binti na mamaye, na mkwe na mkwe mtu;
36 na adui za mtu ni wale wa nyumbani mwake.
37 Apendaye baba au mama kuliko mimi, hanistahili; wala apendaye mwana au binti kuliko mimi, hanistahili.
38 Wala mtu asiyechukua msalaba wake akanifuata, hanistahili. "


Kwahiyo Mungu anapokuita hamaanishi kwamba anataka kukuletea maafa wewe katika familia yako au kati ya ndugu zako, Hapana lakini mwanzo lazima mafarakano yaje kwasababu hautaeleweka ila mwisho wake huwa mzuri. maana kwa kumtii wewe Mungu utawapata na ndugu zako lakini usidhani kwa kuwatii wazazi wako ukamweka Mungu kando ndio umewaokoa wazazi wako la! hasha kinyume cha hapo utaipoteza roho yako pamoja na zao. Mfano mzuri tunaye Bwana wetu alionekana amerukwa na akili kwa ajili ya Mungu, watu wa nyumbani mwake hawakumwamini maandiko yanasema hivyo soma Yohana 7:5 na (Marko 3:21" Jamaa zake walipopata habari wakatoka kwenda kumkamata; maana walisema, Amerukwa na akili. ") kama Bwana hakuona haya kuonekana amerukwa na akili inatupasaje sisi?..Lakini tunaona kwa kumtii kwake Mungu watu wa nyumbani mwake walikuja kuokolewa pamoja na dunia nzima. Haleluya.!
       UBARIKIWE NA BWANA YESU!

Wednesday, July 19, 2017

MASWALI NA MAJIBU: SEHEMU YA 16

SWALI 1: Bwana aliposema kuwa yeye ni "Mungu wa miungu" alikuwa na maana gani?..je! yeye ni Mungu wa sanamu?

JIBU: Tukisoma kumbukumbu 10:17 "Kwa maana Bwana, Mungu wenu, yeye ndiye Mungu wa miungu, na Bwana wa mabwana, Mungu mkuu, mwenye kuogofya, asiyependelea nyuso za watu, wala hakubali rushwa. ". Hapa  tunaona Mungu anajitambulisha yeye kama Mungu wa miungu sasa swali hawa miungu ni wakina nani?.
Bwana Yesu alisema

 Yohana 10:33 "Wayahudi wakamjibu, Kwa ajili ya kazi njema hatukupigi kwa mawe; bali kwa kukufuru, na kwa sababu wewe uliye mwanadamu wajifanya mwenyewe u Mungu.
34 Yesu akawajibu, Je! Haikuandikwa katika torati yenu ya kwamba, Mimi nimesema, Ndinyi miungu?
35 Ikiwa aliwaita miungu wale waliojiliwa na neno la Mungu; (na maandiko hayawezi kutanguka); " .
36 je! Yeye ambaye Baba alimtakasa, akamtuma ulimwenguni, ninyi mnamwambia, Unakufuru; kwa sababu nalisema, Mimi ni Mwana wa Mungu? "

 Kwahiyo unaona hapo miungu inayozungumziwa hapo ni WATOTO WA MUNGU. wengi wanadhani kuwa miungu iliyozungumziwa pale ni "SANAMU" LA! sivyo. Mungu hawezi akawa ni Mungu wa sanamu. Na tunajua tabia za miungu ni lazima zifanane na Mungu, Hivyo basi kazi zile zile Mungu anazozifanya lazima na miungu izifanye, kwa mfano Mungu alitumia NENO lake kuumba na kufanya kila kitu na sisi vivyo hivyo kwa NENO lake tunaweza tukafanya kazi za Mungu vile vile kama yeye. Lakini tusipoweza kufanya hivyo inamaana sisi sio miungu kwasababu hatufanani na yeye. Kwahiyo ili sisi tuwe miungu lazima tuwe ni WATOTO WA MUNGU wenye tabia hizi: Upendo, Imani, Haki, Utakatifu,  n.k.


Swali 2:
Naomba kufahamu maana ya huu mstari...Mathayo 5:39 "Lakini mimi nawaambia, Msishindane na mtu mwovu; lakini mtu akupigaye shavu la kuume, mgeuzie na la pili. "


JIBU:  Bwana Yesu aliposema mtu akupigaye shavu la kuume, mgeuzie na la pili na sawasawa na alivyosema pia “mtu atakaye kukushitaki na kuitwaa kanzu yako, mwachie na joho pia.” Hii ikiwa na maana kuwa kwa kufanya hivyo utakuwa umeushinda uovu na utafanikiwa kuiokoa roho ya mtu kuliko kuingamiza. kwasababu kwa kufanya vile Biblia inasema utakuwa umempalia makaa ya moto kichwani pake, akijiuliza ni kwanini sikutendewa kama mimi nilivyomtendea hivyo baadaye atajiona yeye ndiye mwenye makosa na kugeuka na kutubu. Lakini atakapokupiga na wewe ukamrudishia, au atakapochukua mali yako nawe  ukaenda kuchukua ya kwake atachomwaje dhamira na kujiona yeye ni mwenye dhambi? hivyo atabakia kuwa vilevile tu na kukuona wewe ni mtu wa kawaida tu kama watu wengine. 

Na ndio maana Bwana Yesu alisema tuushinde ubaya kwa wema, ili tuwe wakamilifu kama Baba yetu alivyomkamilifu. Aliendelea kusema...
Mathayo 5:41 “Na mtu atakayekulazimisha mwendo wa maili moja, nenda naye mbili.
42 Akuombaye, mpe; naye atakaye kukopa kwako, usimpe kisogo.
43 Mmesikia kwamba imenenwa, Umpende jirani yako, na, Umchukie adui yako;
44 lakini mimi nawaambia, Wapendeni adui zenu, waombeeni wanaowaudhi,
45 ili mpate kuwa wana wa Baba yenu aliye mbinguni; maana yeye huwaangazia jua lake waovu na wema, huwanyeshea mvua wenye haki na wasio haki.
46 Maana mkiwapenda wanaowapenda ninyi mwapata thawabu gani? Hata watoza ushuru, je! Nao hawafanyi yayo hayo?
47 Tena mkiwaamkia ndugu zenu tu, mnatenda tendo gani la ziada? Hata watu wa mataifa, je! Nao hawafanyi kama hayo?
48 Basi ninyi mtakuwa wakamilifu, kama Baba yenu wa mbinguni alivyo mkamilifu. “


SWALI 3:
Je! Kuna malaika wanaotembea na watu?


JIBU: Ndio wapo malaika wanaotembea na watu lakini sio watu wote ila wale tu wanaotembea katika NENO la Mungu, Tukisoma waebrania 1:13 “Je! Yuko malaika aliyemwambia wakati wo wote, Uketi mkono wangu wa kuume Hata nitakapoweka adui zako chini ya nyayo zako? JE! HAO WOTE SI ROHO WATUMIKAO?, wakitumwa kuwahudumu wale watakaourithi wokovu? “.
Kwahiyo tunaona hapo malaika wanatembea na wale tu “watakaourithi wokovu”,  ambao ni wale wanaolishika NENO la Mungu ndio hao tu “watakaowahudumia”. Tunaweza tukaona mfano wa watu hawa kwenye biblia kama Petro (matendo12:15) na Mtume Paulo tukisoma
 matendo 27:23 Kwa maana usiku huu wa leo malaika wa Mungu yule ambaye mimi ni wake, naye ndiye nimwabuduye, alisimama karibu nami,
24 akaniambia, Usiogope, Paulo, huna budi kusimama mbele ya Kaisari; tena, tazama, Mungu amekupa watu wote wanaosafiri pamoja nawe. “ .Hii inathibitisha kuwa Paulo alikuwa na malaika anayetembea naye.
Pia wana wa israeli jangwani Mungu aliwatumia malaika awaongoze katika safari yao ya kwenda kaanani ndio yule aliyekuwa akisimama katika “nguzo ya moto” usiku na  “nguzo ya wingu” mchana...kutoka 23:20 Tazama, mimi namtuma malaika aende mbele yako, ili akulinde njiani na kukupeleka mpaka mahali pale nilipokutengezea. “...kutoka 23:23 “Kwa kuwa malaika wangu atatangulia mbele yako, na kukufikisha kwenye Mwamori, na Mhiti, na Mperizi, na Mkanaani, na Mhivi, na Myebusi; nami nitawakatilia mbali. “.

Hivyo basi kazi ya malaika wa Mungu ni kuhakikisha NENO la Mungu unalolishikilia linatimia juu yako kwa mfano NENO la Mungu linaposema “KWA KUPIGWA KWAKE SISI TUMEPONA”. Mtu yeyote anayeliamini hili NENO na kulishikilia Bwana anamtuma malaika wake kuhakikisha kwamba hilo NENO linatimia juu yake na hatimaye anapokea uponyaji wake haijalishi itachukua muda gani ni lazima lije kutimia. Lakini kama hauliamini na kulishika NENO la Mungu ni dhahiri kuwa malaika wa Mungu hatakuwa na kazi juu yako hivyo utabakia tu kuwa kama mtu asiyekuwa na msaada.


Mfano mwingine NENO la Mungu linaposema “ Luka 6:38 ..Wapeni watu vitu, nanyi mtapewa; kipimo cha kujaa na kushindiliwa, na kusukwa-sukwa hata kumwagika, ndicho watu watakachowapa vifuani mwenu. Kwa kuwa kipimo kile kile mpimacho ndicho mtakachopimiwa. “..Sasa kitendo cha wewe kuliamini hili NENO na kuwapa watu vitu,(mfano kuwasaidia maskini, na wahitaji) Malaika wa Bwana anakuja kuhakikisha kuwa hilo NENO linakuja kutimia la wewe kulipwa kwa kipimo kile kile ulichompimia mwenzako ili NENO la Mungu liwe dhahiri na kweli. Lakini kama usipolishika hilo NENO yule malaika hawezi kuja kutembea na wewe kwasababu haoni jambo la kufanyia kazi ndani yako.


Vivyo hivyo na maneno mengine yote ya Mungu, kwa jinsi unavyoyashika na kuyaishi maneno ya Mungu ndivyo unavyofungua milango ya malaika wa Mungu kutembea na wewe lakini usipoliamini NENO la Mungu na kuliishi utabakia kuwa mtu usiyeona uweza wa Mungu juu ya maisha yako. Pasipo IMANI haiwezekani kumpendeza Mungu.
 Mungu akubariki!

Monday, July 10, 2017

ALIYE MKUU KATIKA UFALME WA MBINGUNI.


Kuna tofauti kati ya MAMLAKA(CHEO) na UTAJIRI. Unaweza ukawa tajiri lakini usiwe na mamlaka au cheo na pia unaweza ukawa na CHEO na usiwe tajiri au unaweza ukawa na vyote viwili kwa pamoja. Kwamfano viongozi wenye vyeo kama wakuu wa mikoa, madiwani, mawaziri na mameya, wana nguvu na usemi juu ya watu wote pamoja na matajiri huko huko, haijalishi matajiri wana fedha kiasi gani, hiyo haiwapi wao mamlaka ya kuiamrisha nchi. Kiongozi akisema ndiyo ni ndiyo na hapana ni hapana japokuwa hao viongozi wanaweza wasiwe na mali na utajiri wowote wa kuwazidi hao matajiri wa nchi lakini wamepewa mamlaka makuu juu ya wote yaani matajiri na wasio matajiri. Lakini matajiri hawawezi wakawa na mamlaka juu ya wakuu wa nchi (Viongozi).


Vivyo hivyo katika ukristo, kuna UKUU na UTAJIRI. tutazame utajiri ni upi na ukuu ni upi;


UTAJIRI KATIKA UFALME WA MBINGUNI:

Kama tunavyofahamu utajiri unakuja kwa bidii na juhudi za mtu, kwa jinsi unavyofanya kazi sana, na kujiwekea hazina ndivyo utajiri wake unavyokuja. Na ndivyo ilivyo hata kwa Mungu utajiri katika Kristo unakuja unapokuwa mwaminifu katika kazi ya Mungu. bidii yako kuitumia karama uliyopewa katika kuhubiri, kuwavuta watu kwa Kristo, kutumika katika kanisa, kutenda wema na ukarimu, kutoa sadaka, kusaidia yatima na wajane pamoja na maskini n.k, kiufupi kazi zote njema zinazotokana na Mungu. Yote haya ni HAZINA unayojiwekea mbinguni ambao ndio huo UTAJIRI wako, Luka 12:33 "Viuzeni mlivyo navyo, mtoe sadaka. Jifanyieni mifuko isiyochakaa, akiba isiyopungua katika mbingu, mahali pasipokaribia mwivi, wala nondo haharibu.Kwa kuwa HAZINA YENU ILIPO, ndipo itakapokuwapo na mioyo yenu. " Unaona jinsi utoavyo sadaka ndivyo utajiri wako unavyoongezeka mbinguni.


Marko 12:41 "Naye akaketi kulielekea sanduku la hazina, akatazama jinsi mkutano watiavyo mapesa katika sanduku. Matajiri wengi wakatia mengi.
42 Akaja mwanamke mmoja, mjane, maskini, akatia senti mbili, kiasi cha nusu pesa.
43 Akawaita wanafunzi wake, akawaambia, Amin, nawaambia, Huyu mjane maskini AMETIA ZAIDI kuliko wote wanaotia katika sanduku la hazina;
44 maana hao wote walitia baadhi ya mali iliyowazidi; bali huyu katika umaskini wake AMETIA VYOTE ALIVYOKUWA NAVYO, ndiyo riziki yake yote pia. " 

Unaona tena hapo kitu cha pekee alichokuwa nacho yule mwanamke ni pale alipotoa vyote alivyo navyo kwa ajili ya BWANA, ikamfanya aonekane mbinguni kuwa mwenye utajiri mkubwa kuliko wote, nasi pia tunafundishwa tufanye hivyo sio tu pale tunapozidiwa na mali tumtolee Mungu, bali hata katika hali ya upungufu tuliyopo tumtolee Mungu vyote ili UTAJIRI wetu mbinguni uwe mkubwa.



UKUU KATIKA UFALME WA MBINGUNI:

Tukisoma..
Mathayo 18:1 "Saa ile wanafunzi wakamwendea Yesu wakisema,
2 Ni nani basi aliye mkuu katika ufalme wa mbinguni? Akaita mtoto mmoja, akamweka katikati yao,
3 akasema, Amin, nawaambia, Msipoongoka na kuwa KAMA VITOTO, hamtaingia kamwe katika ufalme wa mbinguni.
4 Basi, YE YOTE AJINYENYEKESHAYE  MWENYEWE KAMA MTOTO HUYU, huyo ndiye aliye MKUU katika ufalme wa mbinguni."


Wengi wanadhani unapohubiri injili, au unapotoa sadaka sana, au unapotumika kanisani sana kunakufanya wewe kuwa MKUU mbinguni hapana huko kote ni kukuongezea utajiri(HAZINA) yako mbinguni lakini sio kukupa wewe UKUU au MAMLAKA, Kama tulivyotangulia kusema mtu anaweza akawa na mamlaka na asiwe tajiri, au anaweza akawa na vyote kwa pamoja na ndivyo ilivyo hata kwa Mungu, UKUU au UKUBWA, au MAMLAKA unakuja kwa njia moja tu. Biblia inaiita "KUJINYENYEKEZA NA KUWA MDOGO KULIKO WOTE KATIKA KRISTO" Kwa mfano wa mtoto mdogo Hilo tu!. 



Na kujinyenyekeza huku kunakuja kwa namna mbili..


1.Unyenyekevu kwa MUNGU.

Bwana Yesu alituambia tuwatazame watoto wadogo, kwasababu watoto wadogo siku zote wanaweka tegemeo lao lote kwa Baba zao kwa kila kitu kwa chakula,afya,malazi,mavazi n.k., wao ni kama kondoo pasipo wazazi wao hawawezi kufanya lolote, wanapoadhibiwa ni wepesi kubadilika na hawana kinyongo, kichwa cha mtoto mdogo ni chepesi kujifunza kuliko cha mtu mzima kwasababu yupo tayari siku zote kukubali kusikia, mtoto mdogo ni mtii, na anaamini lolote atakaloambiwa na wakubwa zake bila kushukushuku, Na ndivyo Bwana Yesu alivyokuwa kwa BABA yake tunasoma kila mahali alikuwa anamtaja BABA, BABA, BABA,ikiashiria pasipo BABA yake hawezi kufanya lolote soma Yohana 5:19"Mwana hawezi kutenda neno mwenyewe ila lile ambalo amwona Baba analitenda; kwa maana yote ayatendayo yeye, ndiyo ayatendayo Mwana vile vile. "..Unaona hapo jinsi YESU alivyojinyenyekesha chini ya mapenzi ya baba yake na kuwa mtii hata MUNGU akamfanya kuwa mkubwa kuliko vitu vyote vya mbinguni na duniani. 


Wafilipi 2:8 "tena, alipoonekana ana umbo kama mwanadamu, ALIJINYENYEKEZA AKAWA MTII HATA MAUTI, naam, mauti ya msalaba.
9 Kwa hiyo tena Mungu alimwadhimisha mno, akamkirimia Jina lile lipitalo kila jina;
10 ili kwa jina la Yesu kila goti lipigwe, la vitu vya mbinguni, na vya duniani, na vya chini ya nchi;
11 na kila ulimi ukiri ya kuwa YESU KRISTO NI Bwana, kwa utukufu wa Mungu Baba. "

Na sisi vivyo hivyo tunapaswa tujinyenyekeze chini ya BABA yetu wa mbinguni mfano wa MTOTO-na-BABA yake. mapenzi yetu yafe lakini ya Mungu yatimizwe maishani mwetu.Hii ndiyo sadaka ya kwanza mtu anaweza akamtolea Mungu yenye kumpendeza. Kumbuka BWANA YESU alishuhudiwa na BABA kwanza kuwa AMEMPENDEZA kabla hata hajaanza kuhubiri injili au kufanya kazi ya Mungu.(mathayo 4). Hii ni namna ya kwanza na ya pili ni;



2.Kujinyenyekeza chini ya ndugu (wakristo).
Bwana Yesu aliwaeleza wanafunzi wake,atakayetaka kuwa mkubwa kati yenu na awe mdogo kuliko wote, kama yeye alivyokuwa mdogo kuliko wote. YESU alimnyenyekea BABA pamoja na wanadamu Vivyo hivyo na sisi pia sio tu kumtii Mungu halafi tunawadharau ndugu zetu, na kujifanya sisi ni KITU fulani cha kipekee zaidi ya wao. tunapaswa tujishushe tuwatumikie wenzetu mfano ule ule wa YESU KRISTO hata kufikia kiwango cha kuona nafsi ya ndugu yako ni bora kuliko ya kwako. Tusome..


Marko 10:42 "Yesu akawaita, akawaambia, Mwajua ya kuwa wale wanaohesabiwa kuwa wakuu wa Mataifa huwatawala kwa nguvu, na wakubwa wao huwatumikisha.
43 Lakini haitakuwa hivyo kwenu; BALI MTU ATAKAYETAKA KUWA MKUBWA KWENU, ATAKUWA MTUMISHI WENU,
44 NA MTU ANAYETAKA KUWA WA KWANZA WENU, ATAKUWA MTUMWA WA WOTE.

45 Kwa maana Mwana wa Adamu naye hakuja kutumikiwa, bali kutumika, NA KUTOA NAFSI YAKE IWE FIDIA YA WENGI." 

Mahali pengine Bwana Yesu aliwaambia wanafunzi wake.

.Mathayo 11:11 " Amin, nawaambieni, Hajaondokea mtu katika wazao wa wanawake aliye mkuu kuliko Yohana Mbatizaji; walakini ALIYE MDOGO KATIKA UFALME WA MBINGUNI ni MKUU kuliko yeye. " Hii ikiwa na maana kuwa yule ANAYEJINYENYEKEZA (KWA MUNGU na KWA WANADAMU) na KUWA MDOGO, Huyo ndiye aliye MKUU kuliko Yohana mbatizaji,.Unaweza ukaona ni faida gani aliyonayo mtu yule ajishushaye kama mtoto mdogo halafu anakuwa mkubwa kuliko hata manabii mfano wa Yohana Mbatizaji na wote waliomtangulia kabla yake.

Katika utawala unaokuja huko mbele wa milele, Kristo akiwa kama MFALME WA WAFALME, atatwaa wafalme wengine hao ndio watakaoitawala dunia wakati huo milele, sasa hizi nafasi za wafalme hawatapewa wale MATAJIRI WA ROHO bali wale WAKUU WA ROHO. Hawa wakuu watakuwa na amri, na usemi kwa kila kitu na kila kiumbe duniani kitakuwa chini yao kwasababu watakuwa wamepewa hayo na MKUU WA WAKUU (YESU KRISTO), Biblia inasema wataichunga dunia kwa fimbo ya chuma,(Ufunuo 2:26 Na yeye ashindaye, na kuyatunza matendo yangu hata mwisho, nitampa mamlaka juu ya mataifa, naye atawachunga kwa fimbo ya chuma, kama vyombo vya mfinyanzi vipondwavyo, kama mimi nami nilivyopokea kwa Baba yangu. Nami nitampa ile nyota ya asubuhi. )... watakuwa wenye mataji mengi kama leo hii tu huwezi kuwakaribia hawa wafalme wa dunia ambao sio kitu itakuwaje kwa wale?? watakuwa ni miale ya moto kama BWANA MWENYEWE.


 Vivyo hivyo na MATAJIRI watapewa heshima yao, watamiliki hazina nyingi, watakuwa na HESHIMA katika ulimwengu kama tu vile matajiri wa ulimwengu huu wanavyoheshimika sasa, chochote watakachotaka watapata, kwasababu walijiwekea HAZINA nyingi mbinguni, kuna viwango vya umiliki watafikia wewe usiye na kitu hutaweza kufika. 


Bwana mwenye haki atamlipa kila mtu kwa kadri ya alichokipanda ulimwenguni. Kumbuka wapo pia watakaokuwa MATAJIRI NA WAKUU kwa pamoja. Hao ndio wale waliojinyenyekeza na kumtumikia Mungu kwa bidii na kwa moyo, waliitangaza injili, walikuwa watumishi kati ya ndugu, watakatifu, waaminifu katika karama walizopewa, walikuwa kama vitoto vidogo mbele za MUNGU, walikuwa na mapenzi yao wenyewe lakini wakayakataa na kuyakubali mapenzi ya MUNGU maishani mwao, katika mapito yao yote hawakumnung'unikia, walitii na kumwamini pasipo majadiliano kama tu mtoto na baba yake mfano wa BWANA WETU YESU KRISTO.


Kwahiyo ndugu tuutafute UKUU na UTAJIRI WA MBINGUNI. lakini zaidi UKUU ambao kwa huo tu ndio utakaokuleta karibu na Mungu.


Ufunuo 3:19 Wote niwapendao mimi nawakemea, na kuwarudi; basi uwe na bidii, ukatubu.
20 Tazama, nasimama mlangoni, nabisha; mtu akiisikia sauti yangu, na kuufungua mlango, nitaingia kwake, nami nitakula pamoja naye, na yeye pamoja nami.
21 Yeye ashindaye, nitampa kuketi pamoja nami katika kiti changu cha enzi, kama mimi nilivyoshinda nikaketi pamoja na Baba yangu katika kiti chake cha enzi. "

Mungu akubariki.

Saturday, July 8, 2017

DHAMBI YA MAUTI


1Yohana 5:16 "Mtu akimwona ndugu yake anatenda dhambi isiyo ya mauti, ataomba, na Mungu atampa uzima kwa ajili ya hao watendao dhambi isiyo ya mauti. IKO DHAMBI ILIYO YA MAUTI. Sisemi ya kwamba ataomba kwa ajili ya hiyo.Kila lisilo la haki ni dhambi, na dhambi iko isiyo ya mauti."


Biblia inaeleza wazi kuwa kuna DHAMBI ZA MAUTI na DHAMBI ZISIZO ZA MAUTI:




DHAMBI ISIYO YA MAUTI:

Hii ni dhambi ambayo mtu akiifanya anaweza akatubu na kusamehewa, na dhambi hii ni ile inayotokana na aidha kutenda pasipo kukusudia, au inatendeka kutokana na uchanga wa kiroho, au kwa kukosa maarifa  au jambo lingine lolote linaloweza kutendeka ambalo halijavuka mipaka ya neema. Dhambi  ya namna hii biblia inasema mtu anaweza akatubu au akamuungamania mwenzake na akasamehewa, akaendelea kuishi na asife. Lakini kuna dhambi mtu akiitenda hiyo hata huyo mtu aombeje, anaweza akasamehewa kosa tu lakini adhabu ya mauti ipo pale pale, je! hii dhambi inasababishwa na nini?



DHAMBI YA MAUTI:

Dhambi hii ipo kwa namna mbili, ya kwanza kwa wale watoto wa Mungu (watumishi wake) na ya pili ni kwa watu wengine ambao neema ya Mungu inalilia masikioni mwao lakini wanaichezea. Namna hizi mbili tunaweza tukaona zimefananishwa  na Musa na wana wa Israeli kule jangwani, Musa akiwa mfano wa "watumishi wa Mungu", pamoja na kwamba Mungu alitembea nae kwa namna ya tofauti hata kuliko manabii wote, lakini alitenda dhambi kwa kosa kutokutii maagizo ya Mungu na kuchukua utukufu wa Mungu, alifanya vile akijua kabisa kuwa ni kosa ikampelekea kutenda DHAMBI YA MAUTI, 


Musa kwa kweli alisamehewa lile kosa lakini adhabu ya mauti ilikuwa pale pale iliyomsababishia apoteze hata zile ahadi zote Mungu alizomuahidia za kuiona nchi ya Ahadi. Hata leo hii wapo watumishi wanatenda hii dhambi, wanachukua utukufu wa Mungu na kutokutii maagizo yake, inapelekea Mungu kuwaadhibu huduma zao zinakatishwa kama ilivyotokea kwa Anania na Safira walipomdanganya Roho Mtakatifu na kupokea adhabu ya kifo pale pale japo walikuwa ni watoto wa Mungu. Hizo zote ni DHAMBI ZA MAUTI.

Vivyo hivyo na wana wa israeli ni mfano kamili wa "wakristo vuguvugu" wa leo kumbuka wana wa israeli ijapokuwa waliuona utukufu wote wa Mungu, na maajabu yote na miujiza yote lakini mioyo yao haikuwa mikamilifu  ijapokuwa Mungu aliwavumilia kwa muda mrefu watubu lakini hawakutaka wakaanza kuabudu sanamu, wakafanya uasherati, wakawa wakimnung'unikia Mungu na kumjaribu ikafika wakati neema ya Mungu juu yao ikakoma Mungu akaapa kwamba wote wangekufa nyikani ijapokuwa walitubu kwa kulia na kuomboleza hata hivyo hakuna hata mmoja wao aliyeiona nchi ya ahadi isipokuwa wale wana wao tu!, unaona hiyo ndiyo DHAMBI YA MAUTI. unajisikiaje pale ambapo unaona ungestahili kupata baraka fulani halafu unazikosa, hautakaa uzipate tena milele? fikiri juu ya hilo, na ndio maana maandiko yafuatayo yanatuonya..tusome.


1 wakorintho 1 Kwa maana, ndugu zangu, sipendi mkose kufahamu ya kuwa baba zetu walikuwa wote chini ya wingu; wote wakapita kati ya bahari;
2 wote wakabatizwa wawe wa Musa katika wingu na katika bahari;
3 wote wakala chakula kile kile cha roho;
4 wote wakanywa kinywaji kile kile cha roho; kwa maana waliunywea mwamba wa roho uliowafuata; na mwamba ule ulikuwa ni Kristo.
5 Lakini wengi sana katika wao, Mungu hakupendezwa nao; maana waliangamizwa jangwani.
6 Basi mambo hayo yalikuwa mifano kwetu, kusudi sisi tusiwe watu wa kutamani mabaya, kama wale nao walivyotamani.
7 Wala msiwe waabudu sanamu, kama wengine wao walivyokuwa; kama ilivyoandikwa, Watu waliketi kula na kunywa, kisha wakasimama wacheze.
8 Wala msifanye uasherati, kama wengine wao walivyofanya, wakaanguka siku moja watu ishirini na tatu elfu.
9 Wala tusimjaribu Bwana, kama wengine wao walivyomjaribu, wakaharibiwa na nyoka.
10 Wala msinung'unike, kama wengine wao walivyonung'unika, wakaharibiwa na mharabu.
11 Basi mambo hayo yaliwapata wao kwa jinsi ya mifano, yakaandikwa ili kutuonya sisi, tuliofikiliwa na miisho ya zamani.
12 Kwa hiyo anayejidhania kuwa amesimama na aangalie asianguke. 

Mfano kamili wa kanisa la leo lililo vuguvugu kupita kiasi" linaona utukufu wa Mungu karibu kila mtu anafahamu kabisa kuwa KRISTO ni mwokozi, mponyaji, na wengi wao wamebatizwa wanaenda kanisani, wanaujua ukweli wote lakini utakuta bado mtu ni mwasherati, mlevi, mtukanaji, anaenda disco, msengenyaji, anatazama pornography, anavuta sigara, anavaa mavazi ya kiasherati n.k. angali akifahamu Mungu hapendezwi na watu wa namna hiyo. Anaiona neema ya Mungu lakini bado anaidharau mfano ule ule wa wana wa Israeli, Lakini watu kama hawa hawajui kuwa wapo hatarini kutenda DHAMBI YA MAUTI. kama tu Mungu hakuweza kumwachilia mtumishi wake Musa kwa kosa dogo tu la kutokutii wewe unadhani utaponea wapi ikiendelea na maisha yako ya dhambi?..Ni kweli Musa alisamehema lakini adhabu ya kutokuiona nchi ya ahadi kwa njia ya Mauti ilikuwa pale pale.


Kwa namna hiyo hiyo unahubiriwa injili leo umgeukie Mungu, uache dhambi utubu usamehewe unasema hapana ngoja nile maisha nitakuja kutubu baadaye unaweza usiseme kwa mdomo lakini moyo wako unasema unaendelea kuwa mwasherati pale unapopata ugonjwa usiokuwa na matumaini mfano ukimwi unaona ndio sababu ya kumgeukia Mungu angali wakati ulipokuwa mzima hukufanya hivyo? Ni kweli ukitubu unaweza ukasemehewa lakini adhabu ya mauti ipo pale pale ndio maana utaona watu wa namna hiyo hata waombeweje hawaponi, sababu ni kwamba wameshatenda DHAMBI YA MAUTI. Sisemi hili kwa kukutisha lakini ndio ukweli tuyachunguze maisha yetu.


Mara nyingine sauti ya Mungu inakulilia uache dhambi ya ulevi na uvutaji sigara ili usafishwe maisha yako lakini unaziba masikio yako hutaki kusikia. Mungu anaruhusu pepo la Kansa linakuingia unapata kansa ya koo au mapafu au ini hapo ndipo unapoona sababu ya kumrudia Mungu ni kweli ukitubu Mungu anaweza kukusamehe lakini adhabu ya kifo ipo pale pale Kwasababu apandacho mtu ndicho atakachovuna. Mungu sio wa kumtegea kwamba niache nifanye mambo yangu kisha nikishafika mzee au wakati fulani ndipo nimgeukie, Mungu hadhihakiwi.


MADHARA YA DHAMBI YA MAUTI:

Madhara yake makubwa ni kwamba utapoteza thawabu yako katika ule ulimwengu ujao kwasababu umelikatisha kusudi la Mungu juu yako, ndio hapo kama Mungu alikupa huduma au anataka uwe na huduma haiwezekani tena kuendelea nayo kwasababu ulishatenda DHAMBI YA MAUTI, huna budi kuondoka nafasi yako anapewa mtu mwingine kama ilivyomtokea Yuda nafasi yake ilichukuliwa na mtu mwingine. wakati wengine wakipewa mataji yao mbinguni siku ile kwa kazi nzuri walizotaabika nazo duniani wewe utakuwa huna lolote, utabaki mtu wa kawaida milele.


Hivyo ndugu, biblia inasema 1petro 1:10 " KWAHIYO NDUGU, JITAHIDINI ZAIDI KUFANYA IMARA KUITWA KWENU NA UTEULE WENU; maana mkitenda hayo hamtajikwaa kamwe. " .


Itikia wito wa Mungu ulio ndani yako sasa kabla hazijaja siku zilizo mbaya utakazosema ee! Mungu wangu nisamehe nataka kuishi lakini usiweze kusikilizwa dua zako kwa upumbavu wako mwenyewe. Ndugu Tukisikia hili tuogope kwasababu imeandikwa..


Wafilipi 2:12 "Basi, wapendwa wangu, kama vile mlivyotii sikuzote, si wakati mimi nilipokuwapo tu, bali sasa zaidi sana mimi nisipokuwapo, UTIMIZENI WOKOVU WENU WENYEWE KWA KUOGOPA NA KUTETEMEKA.KWA MAANA NDIYE MUNGU ATENDAYE KAZI NDANI YENU, kutaka kwenu na kutenda kwenu, kwa kulitimiza kusudi lake jema. "

AMEN!


Friday, July 7, 2017

HISTORIA YA WILLIAM BRANHAM


 

Katika Biblia, Mungu daima aliuleta Ujumbe Wake kwa watu wa ulimwengu kupitia kwa nabii wa kizazi hicho. Yeye alisema na Musa kupitia kichaka kilichowaka moto na akampa agizo la kuwaongoza Waebrania kutoka Misri. Nguzo ya Moto iliyo dhahiri pamoja na ishara zingine zilitolewa kuthibitisha huduma yake. Yohana Mbatizaji alileta Ujumbe kuuandaa ulimwengu kwa ajili ya kule kuja kwa Masihi. Wakati akimbatiza Bwana Yesu katika Mto Yordani, Sauti kutoka Mbinguni ililithibitisha agizo la Yohana la kumtambulisha Mwana-Kondoo wa Mungu, “Huyu ni Mwanangu mpendwa, ninayependezwa kukaa ndani Yake.” Miaka kadhaa baadaye, Sauti ya Bwana ilisikika tena ikizungumza na nabii wakati Yeye aliponena na Paulo kwa Nuru ya kupofusha, na baadaye akampa agizo la kuyaweka makanisa katika utaratibu. Kote katika Agano Jipya na la Kale, Mungu kamwe hajapata kuzungumza na watu Wake kupitia mfumo wa kimadhehebu ama shirika la kidini. Yeye daima amesema na watu kupitia mtu mmoja: nabii Wake. Naye aliwathibitisha manabii hawa kwa ishara za kimbinguni.

LAKINI JE! NI VIPI SIKU HIZI? JE! MUNGU ANGALI ANALIFUNUA NENO LAKE KWA MANABII? JE! KUNGALI KUNA ISHARA ZA KIMBINGUNI? JE! MUNGU ANGEMTUMA NABII WA SIKU HIZI ULIMWENGUNI? JIBU LILILODHAHIRI KABISA NI, "NDIO!"


Manabii wa kale walikuwa ni watu jasiri wa Mungu, wala hawakuhofu kukabiliana na mashirika ya kimadhehebu. Kusema kweli, karibu kila wakati walishutumiwa na makasisi. Eliya aliyapa changamoto mashirika ya kidini ya siku zake, akiwauliza kama Mungu angeiheshimu sadaka yao, ama yake. Walipiga makelele. Walitabiri. Wakaruka-ruka juu ya madhabahu hayo. Wakajikata-kata kwa visu. Bali Mungu hakuwasikia. Eliya aliangalia juu Mbinguni na kusema, “Na ijulikane leo ya kuwa Wewe Ndiwe Mungu katika Israeli, na ya kuwa mimi ni mtumishi Wako, na ya kuwa nimefanya mambo haya yote kwa neno lako.” Ndipo basi akaagiza moto ushuke kutoka Mbinguni na kuiteketeza ile sadaka. Nabii Mikaya alishindana na Mfalme wa Israeli, na ukuhani wote, wakati alipomkemea Kuhani Mkuu Zedekia kwa kutabiri uongo. Huyo kuhani Mkuu alimchapa kofi usoni naye Mfalme akamfunga gerezani kwa kusema kweli. Hata Bwana Yesu alichukiwa sana na mashirika ya kidini ya siku Zake hata wakamsulibisha pamoja na wahalifu wabaya sana. Kama historia ikishikilia kuwa ni ya kweli, nabii angechukiwa na mfumo wa sasa wa kimadhehebu, naye angebandikwa jina la mzushi, nabii wa uongo, ama jina baya zaidi. Ila Mungu angemtetea mtumishi Wake.

KAMA KULIKUWAKO NA NABII KATIKA SIKU HIZI ZA KISASA, ANGEKUBALIKANAJE NA KANISA KATOLIKI? KANISA LA KIBAPTISTI? KANISA LA KILUTHERI, AU NA DHEHEBU LINGINE LOLOTE?

Bwana Yesu aliwaagiza wote wanaomwamini Yeye: “Na ishara hizi zitafuatana na hao waaminio; Kwa jina langu watatoa pepo; watasema kwa lugha mpya; Watashika nyoka; hata wakinywa kitu cha kufisha, hakitawadhuru kabisa; wataweka mikono yao juu ya wagonjwa, nao watapata afya.” (Marko 16:17-18). Je! Andiko hili ni la kweli leo? Ikiwa si la kweli, je! Maneno ya Bwana yalikoma kutumika lini? Kote katika Biblia, manabii waliweza kuwaponya wagonjwa, kutoa pepo, na kufanya miujiza. Musa alimweka yule nyoka wa shaba mbele za watu wa Israeli kuwaponya wakiumwa na nyoka wa sumu (Hesabu 21:9). Naamani, Mshami hodari, alimjia Elisha apate kuponywa ukoma (II Wafalme 5:9). Wakati kijana mwanamume mmoja alipoanguka kutoka kwenye dirisha la juu akafa, mtume Paulo alimkumbatia na kuurejesha uhai kwenye mwili uliokufa (Matendo 20:10). Tuna taarifa ya kama miaka 3½ pekee ya maisha ya Bwana wetu Yesu, bali katika miaka hiyo michache, Yeye aliendelea kuwaponya wagonjwa. Vipofu walifanywa kuona. Wenye ukoma waliponywa. Viziwi walipokea kusikia kwao. Viwete walitembea. Kila namna ya ugonjwa iliponywa (Mat. 4:23).

Mungu pia aliwathibitisha manabii wake kwa njia zingine mbali na uponyaji. Hata siri zilizofichwa sana za moyo zilijulishwa watu hawa wa Mungu. Mfalme Nebukadreza alikuwa na ndoto iliyomsumbua, lakini asingeweza kukumbuka ilikuwa inahusu nini. Nabii Danieli alimfumbulia mfalme huyo ndoto hiyo pamoja na unabii uliofuata (Dan 2:28). Hakuna kitu alichofichwa Sulemani wakati Malkia wa Sheba alipokuja mbele zake. Yeye alikuwa amejazwa sana na Roho hata yeye alimpambanulia maswali ya moyoni mwake kabla hajayauliza (I Wafalme 10:3). Elisha alimfichulia Mfalme wa Israeli mipango yote ya Mfalme wa Shamu, hata maneno ya binafsi aliyonena katika chumba chake cha kulala (II Wafalme 6:12).

Kupitia matendo Yake mwenyewe, Bwana Yesu mara nyingi alionyesha ya kwamba Roho huyu wa utambuzi ni Roho wa Kristo. Yeye aliitambua tabia ya Nathanaeli wakati aliposema, “Tazama, Mwisraeli kweli kweli, hamna hila ndani yake!” Ndipo Yesu akaendelea kumwambia Nathanaeli mahali alipokuwa wakati Filipo alipomwambia kuhusu Masihi (Yohana 1:48). Wakati Nathanaeli alipoona ya kwamba Yesu aliujua moyo wake, papo hapo alimtambua kuwa Ndiye Kristo. Mara ya kwanza Yesu alipomwona Petro, alimwambia jina la baba yake, Yona (Yohana 1:42). Ndipo Petro alipoacha mambo yote na kumfuata Yesu maishani mwake mwote. Yesu alikutana na yule mwanamke Msamaria kisimani na kumwambia dhambi zake za wakati uliopita. Maneno yake ya kwanza yalikuwa, “Bwana, naona kwamba wewe u nabii” (Yohana 4:19). Watu wote hawa watatu walikuwa wametoka katika tabaka mbali mbali za maisha, hata hivyo walimtambua Yesu mara moja wakati alipoonyesha karama ya utambuzi.

Je! karama hii ilitoweka wakati ukurasa wa mwisho wa Biblia ulipoandikwa? Iwapo miujiza hii imeandikwa dhahiri jinsi hii katika Biblia, iko wapi siku hizi? Nabii wa siku hizi hakika angethibitishwa kwa miujiza.

Je! Mungu amewasahau watu Wake? Je! angali anaweza kuponya wagonjwa? Je! angali ananena nasi kupitia manabii Wake? Je! yeyote wa manabii hao alitangulia kuiona siku hii?

JE! KUNA NABII AMBAZO HAZIJATIMIZWA BADO?



1) AHADI YA NABII KATIKA SIKU ZA MWISHO 


"


Maneno ya mwisho kabisa yaliyoandikwa katika Agano la Kale yanatoa ahadi hii: “Angalieni, nitawapelekea Eliya nabii, kabla haijaja siku ile ya BWANA, iliyo kuu na ya kuogofya. Naye ataigeuza mioyo ya baba iwaelekee watoto wao, na mioyo ya watoto iwaelekee baba zao, ili nisije nikaipiga dunia kwa laana.” (Mal 4:5-6)
Siku ya Bwana iliyo kuu na ya kuogofya haijakuja bado, kwa hiyo inatupasa kumtazamia nabii Eliya kwa moyo. Katika Biblia, manabii hawakuyajilia madhehebu makubwa ya kidini. Waliwajilia wachache waliochaguliwa. Wazia kama yule nabii wa Malaki 4 angelikuja, asitambulikane. Vipi kama yeye ni kama wale manabii wa kale, na ni watu wachache tu wanaomtambua? Kama nabii huyu atarudi katika siku za mwisho, tutamjuaje? Jibu lake linaonekana dhahiri katika Maandiko. Yeye atakuwa na tabia ya nabii. Atazijua siri za moyo. Atafanya miujiza. Madhehebu ya kidini yatajaribu kumkosoa. Bali kutakuwako na wachache waliochaguliwa ambao watamtambua kama mjumbe aliyeahidiwa kwa ajili ya siku hizi.

TUTAJUAJE WAKATI ELIYA ATAKAPORUDI? YEYE ATAONYESHA TABIA ZIPI KUSUDI TUWEZE KUMTAMBUA?
Eliya alikuwa ni mtu wa nyikani. Ishara kuu na maajabu yaliifuata huduma yake. Alihubiri dhidi ya maovu ya siku zake. Zaidi sana alihubiri dhidi ya utovu wa uadilifu wa Malkia Yezebeli. Wakati Eliya alipotwaliwa juu Mbinguni katika gari la moto, roho yake ilishuka juu ya Elisha. Ndipo ishara kuu na maajabu yakaifuata huduma ya Elisha, naye pia alihubiri dhidi ya dhambi za ulimwengu. Manabii hao wote wawili walisimama peke yao dhidi ya mashirika ya kidini ya siku hizo. Mamia ya miaka baadaye, roho yule yule alirudi duniani katika Yohana Mbatizaji. Nabii Malaki alibashiri ya kwamba Eliya angerudi kumtambulisha Bwana: “Angalieni, namtuma mjumbe wangu, naye ataitengeneza njia mbele yangu...” (Malaki 3:1). Yohana Mbatizaji alitimiza hayo wakati akihubiri toba miongoni mwa watoto wa Mungu. Kama vile Eliya, yeye alihubiri dhidi ya mfalme na madhehebu ya kidini ya siku hizo. Bwana Yesu alithibitisha ya kwamba Yohana Mbatizaji alikuwa ndiye nabii wa Malaki 3 katika Kitabu cha Mathayo (11:10): “Huyu ndiye aliyeandikiwa haya, Tazama, mimi namtuma mjumbe wangu mbele ya uso wako, atakayeitengeneza njia yako mbele yako.” Luka 1:17 inasema ya kwamba roho ya Eliya (Elias) ilikuwa iwe katika Yohana Mbatizaji, “Naye atatangulia mbele zake katika roho ya Eliya, na nguvu zake, ili kuigeuza mioyo ya baba iwaelekee watoto.” Lakini angalia kwamba sehemu ya pili ya Malaki 4 ilikuwa bado haijatimizwa: “…na mioyo ya watoto iwaelekee baba zao, ili nisije nikaipiga dunia kwa laana.” Sehemu hiyo ya Maandiko itatimia kabla ya kuja kwa Kristo Mara ya Pili.

MIAKA ELFU MBILI BAADA YA YOHANA MBATIZAJE, WAKATI UMEWADIA TENA KWA ROHO YA ELIYA KURUDI DUNIANI.


Siku hiyo imewadia! Katika wakati huu, tumeiona roho ya Eliya ikirudi. Yeye aliupinga mfumo wa madhehebu ya kisasa. Alizikemea dhambi za ulimwengu. Alionyesha ishara na maajabu yasiyohesabika. Aliihubiri Biblia neno-kwa-neno kutoka Mwanzo hadi Ufunuo. Nabii wa Malaki 4 alikuja kama ilivyoahidiwa, naye akaleta Ujumbe kutoka kwenye Kiti cha Enzi cha Mwenyezi Mungu. Jina la nabii huyo ni William Marrion Branham. Sisi tunamwita “Ndugu Branham.”


  •     Oral Roberts, mwinjilisti anayejulikana sana ulimwenguni na mwanzilishi wa Chuo Kikuu cha Oral Roberts.
    “William Branham, niliyempenda na kuamini yeye ni nabii wa Mungu.”

  
  •     Dr. T.L. Osborn, mwinjilisti wa Kipentekoste na mwandishi hodari.
“William Branham alikuja kwetu kama nabii wa Mungu na akatuonyesha katika karne ya ishirini vitu vile vile dhahiri ambavyo vilionyeshwa katika Injili…Mungu amewatembelea watu Wake, kwa kuwa nabii mkuu ameinuka miongoni mwetu.”


  •     Ern Baxter, mwinjilisti, meneja wa Miamsho ya Branham kwa muda wa miaka saba, pia mmoja wa viongozi wa mwanzoni wa Huduma Mpya ya Kanisa la Kiingereza.  
    “Kabla ya kumwombea mtu, angetoa utondoti sahihi kuhusu maradhi ya mtu huyo, na pia utondoti wa maisha yao - mji wanamoishi, kazi, matendo-hata huko nyuma kabisa utotoni mwao. Branham kamwe hakufanya makosa hata mara moja akiwa na neno la maarifa katika miaka yote niliyokuwa pamoja naye. Hiyo inajumuisha, kwangu mimi, maelfu ya visa.”


Hakuna mtu ambaye ameugusa ulimwengu kwa undani hivyo tangu Bwana Yesu Kristo alipotembea duniani. Kutoka kwenye asili duni katika kibanda cha chumba kimoja kwenye milima ya Kentucky, hadi Amarillo Texas ambako Bwana alimchukua Nyumbani, maisha yake daima yalijaa matukio ya mambo ya kimbinguni. Kwa kuongozwa na Malaika wa Bwana katika mwaka wa 1946, huduma ya Ndugu Branham ilitoa cheche iliyowasha kipindi cha ufufuo mkuu wa uponyaji ulioenea Marekani upesi na kote ulimwenguni. Hata siku ya leo, yeye anatambuliwa na wanahistoria Wakristo kama “baba” na “kiongozi” wa ufufuo wa uponyaji wa miaka ya 1950 ambao ulilibadilisha Kanisa la Kipentekoste na hatimaye ukaizaa huduma ya Karisma, ambayo siku hizi inashawishi karibu kila dhehebu la Kiprotestanti. Hata hivyo, kama ilivyo kawaida yao, madhehebu yanayapuuza mafundisho yake na kulikana agizo lake.

Popote alipoenda, Mungu alithibitisha ya kwamba Ndugu Branham ndiye nabii wa kizazi hiki. Kama vile Ayubu, Bwana alisema naye katika upepo wa kisulisuli. Kama vile Musa, Nguzo ya Moto ilionekana ikimwongoza. Kama vile Mikaya, alishutumiwa na makasisi. Kama vile Eliya, yeye alikuwa ni mtu wa nyikani. Kama Yeremia, aliagizwa na Malaika. Kama Danieli, yeye aliona maono ya usoni. Kama Bwana Yesu, alijua siri za moyo. Na kama vile Paulo, yeye aliwaponya wagonjwa.

Bwana amewatembelea watu Wake tena kupitia nabii. Katika wakati wenye giza sana wa historia, ambapo uadilifu umezama kwenye viwango ambavyo kamwe havijaonekana katika siku za nyuma na silaha za maangamizi ya hadhara zikitishia kwenye upeo wa macho, mtu mnyenyekevu alitumwa kutoka kwenye uwepo wa Mungu kuialika jamii inayokufa ipate kutubu.

Mwanafunzi mpendwa Yohana aliandika kuhusu Bwana Yesu:

Kuna na mambo mengi aliyoyafanya Yesu; ambayo yakiandikwa moja moja, nadhani hata ulimwengu usingetosha kwa vile vitabu vitakavyoandikwa. Amina. (Yohana 21:25).

Jambo lilo hilo linaweza kusemwa kuhusu maisha ya Ndugu Branham. Kuna zaidi ya jumbe 1,200 zilizorekodiwa pamoja na maelfu ya hadithi zinazohusu maisha ya mtu huyu hodari. Hata sasa tunaendelea kusikia shuhuda mpya za ushawishi wake juu ya maisha ya mamilioni ya watu. Kijitabu hiki kisingeweza kubabia ushawishi ambao mtu huyu wa Mungu alikuwa nao juu ya ulimwengu.





2) MWANZO WA MAISHA YANGU (WILLIAM BRANHAM)

 


“Nilipozaliwa katika kibanda kidogo cha Kentucky kule juu, Malaika wa Bwana aliingilia dirishani na kusimama pale. Kulikuwako na Nguzo ya Moto.”

Mapambazuko yalikuwa tu ndiyo kwanza yaanze kupenya giza la mbingu baridi za Aprili. Lile dirisha moja la mbao lilifunguliwa lipate kuiachilia nuru ya asubuhi iingie kwenye chumba hicho kidogo sana cha kibanda. Robini aliyesimama karibu na hilo dirisha alionekana amechangamka sana asubuhi hii na alikuwa akiimba kwa mapafu yake yote. Ndani ya kibanda hicho, kijana Charles Branham aliitia mikono yake kwenye ovaroli yake mpya kabisa na kuinama akimwangalia mke wake mwenye umri wa miaka 15. “Tutamwita jina lake William,” akasema baba yake.

Ndani ya hilo dirisha ikaja Nuru ya kimbinguni. Hiyo nuru ilijongea humo chumbani na kuning’inia juu ya kitanda ambapo huyo mtoto ndiyo kwanza azaliwe. Hii ilikuwa ni Nuru ile ile iliyowaleta wana wa Kiebrania kutoka Misri. Ilikuwa ni Nuru ile ile iliyokutana na Paulo akienda zake Dameski. Nayo itaenda kumwongoza mtoto huyu mdogo apate kumwita Bibi-arusi wa Kristo kutoka ulimwenguni. Hiyo Nuru haikuwa ni mwingine ila ni huyo Malaika wa Bwana, ile Nguzo ya Moto; na kwa mara nyingine tena ilikuwa imemtokea mwanadamu.

    Na mle ndani, katika kibanda hiki kidogo cha mbao, asubuhi hiyo tarehe 6 Aprili, mkunga alifungua dirisha kusudi nuru iweze kuangazia ndani ili Mama na Baba waione sura yangu. Ndipo Nuru ya karibu ukubwa wa mto iliingia ikizungukazunguka upesi kupitia dirishani. Ilizungukazunguka mahali nilipokuwa, kisha ikashuka kitandani. Watu kadhaa wa mlimani walikuwa wamesimama pale. Walikuwa wakilia.

Makazi hayo duni yalikuwa katika milima ya Kentucky kusini, karibu na mji mdogo wa Burkesville. Ilikuwa ni tarehe 6 Aprili, 1909. Mtoto huyo mchanga alikuwa ndiye wa kwanza kati ya watoto kumi ambao wangezaliwa na Charles na Ella Branham.

Haikuchukua muda mrefu kabla ya Malaika wa Bwana kumtembelea mtoto William Branham tena.

Wakati alipokuwa mtoto mchanga, Malaika wa Bwana kwanza alisema naye, akisema ya kwamba angeyaishi maisha yake karibu na mji unaoitwa New Albany. Aliingia nyumbani na kumwambia mama yake yaliyokuwa yametukia tu. Kama mama yeyote, hakuitilia maanani hadithi hiyo naye akamweka kitandani apate kutuliza neva zake changa. Miaka miwili baadaye, familia yake ilihamia Jeffersonville Indiana, maili chache tu kutoka mji wa New Albany ulio kusini mwa Indiana.

Malaika alisema tena na huyo nabii kijana miaka michache baadaye. Ilikuwa ni siku tulivu ya Septemba huku jua lenye joto likiwaka kupitia kwenye matawi ya majira ya kupukutika. Mtoto huyo alikuwa akichechemea huku amebeba ndoo mbili za maji kupitia kwenye ujia. Gunzi la hindi lilikuwa limefungiwa chini ya kidole chake cha mguu kilichojeruhiwa kisije kikaingia uchafu. Aliketi chini ya mti mrefu wa mpopla apate kupumzika. Machozi yalikuwa yakitiririka kutoka machoni mwake huku akilia juu ya msiba wake: marafiki zake walikuwa wakijifurahisha kwenye shimo la mahali hapo la kuvulia samaki, naye alikuwa amekwama akimchotea baba yake maji. Mara, upepo ukaanza kuzungukazunguka juu yake mtini. Akapangusa macho yake na kusimama kwa miguu yake. Akasikia sauti ya majani yakichakarisha katika upepo…bali hakukuwa na upepo. Akaangalia juu, na yapata nusu ya urefu wa kwenda juu wa huo mpopla, kitu fulani kilikuwa kikizungushazungusha hayo majani yaliyokauka.

Mara Sauti ikanena, “Usinywe pombe wala kuvuta sigara wala kuuchafua mwili wako kwa njia yoyote, kutakuwako na kazi utakayofanya utakapokuwa mtu mzima.” Mvulana huyo aliyeingiwa na hofu mwenye umri wa miaka saba aliangusha ndoo zake akakimbilia kwa mamaye.

Majuma machache baadaye, alikuwa akicheza gololi na ndugu yake mdogo. Hisi ya ajabu ilimjia. Akaangalia huko kwenye Mto Ohio na kuona daraja zuri. Watu kumi na sita walianguka wakafa wakati hilo daraja lilipokuwa likivuka mto. Nabii kijana alikuwa ameona ono lake la kwanza. Alimwambia mama yake, naye akaandika simulizi lake. Miaka kadhaa baadaye, watu 16 walianguka wakafa wakati daraja la Mtaa wa Pili huko Louisville, Kentucky lilipokuwa likijengwa juu ya Mto Ohio.
Bwana alikuwa akimwonyesha maono ya usoni. Na kama vile manabii waliomtangulia, maono hayo hayakukosea kamwe.





3) MIAKA YA UJANA

" 



Kote katika maisha yake, Ndugu Branham alitamani kuwa nyikani. Kwenye umri wa miaka 18, aliondoka Indiana kwenda kwenye milima ya magengemagenge ya magharibi. Kukaa kwake Arizona hakukuchukua muda mrefu kabla ya kulazimika kurudi.

    Siku moja niliamua ya kwamba nilikuwa nimepata njia ya kuondolea mbali wito huo. Nilikuwa ninakwenda magharibi kufanya kazi kwenye ranchi. Ewe rafiki, Mungu ni mkuu tu huko nje kama alivyo mahali popote. Naomba ufaidike na uzoefu wa maisha yangu. Anapokuita, mjibu.

    Asubuhi moja ya Septemba katika mwaka wa 1927, nilimwambia mama yangu ya kwamba nilikuwa ninaenda kwenye ziara ya kupiga kambi huko Tunnel Mill, ambako ni kama maili kumi na nne kutoka Jeffersonville tulikoishi wakati huo. Nilikuwa tayari nimepanga safari ya Arizona pamoja na marafiki fulani. Wakati mama aliposikia kutoka kwangu tena, sikuwa Tunnel Mill bali Phoenix, Arizona, nikimkimbia Mungu wa Upendo. Maisha ya ranchi yalikuwa ni mazuri sana kwa muda, lakini mara yalichujuka, kama ilivyo kwa anasa nyingine yoyote ya ulimwenguni. Ila hebu niseme hapa, Mungu Asifiwe, ya kwamba uhusiano wa maisha na Yesu unazidi kuwa mtamu na mtamu wakati wote wala hauchujuki. Yesu huleta amani kamilifu na faraja siku zote.

    Mara nyingi nimesikia upepo ukivuma katika misonobari mirefu. Ilionekana kana kwamba ningeweza kusikia sauti Yake ikiita huko mwituni, ikisema, “Adamu, uko wapi?” Nyota zilionekana zikiwa karibu sana mtu ungaliweza kuzichuma kwa mikono yako. Mungu alionekana kuwa yuko karibu sana.


    Jambo moja kuhusu nchi hiyo ni zile barabara jangwani. Mtu ukitoka kwenye barabara, unapotea kwa urahisi. Mara nyingi sana watalii wanaona maua madogo ya jangwani na wanaondoka kwenye barabara kuu kwenda kuyachuma. Wanazurura jangwani na wanapotea na mara nyingine wanakufa kwa kiu. Ndivyo ilivyo katika njia ya Mkristo — Mungu ana njia kuu. Anazungumza juu yake katika Isaya, mlango wa 35. Inaitwa “Njia Kuu ya Utakatifu.” Mara nyingi anasa ndogo za ulimwengu zinakuvuta kukutoa kwenye njia kuu. Ndipo umepoteza mawasiliano yako na Mungu. Jangwani wakati mtu umepotea, mara nyingine kunatokea mazigazi. Kwa wale watu wanaokufa kwa kiu, mazigazi hayo yatakuwa ni mto ama ziwa. Mara nyingi watu huyakimbilia na kutumbukia ndani yao ndipo tu wanakuta kwamba wanaogelea tu kwenye mchanga wenye joto. Wakati mwingine ibilisi anakuonyesha jambo fulani ambalo anasema ni wakati wa kujifurahisha. Hayo ni mazigazi tu, ni kitu ambacho si halisi. Ukisikiliza utajikuta tu ukijilundikia huzuni nyingi kichwani mwako. Usimsikilize, mpendwa msomaji. Mwamini Yesu awapaye maji yaliyo hai hao wenye njaa na kiu.

    Siku moja nilipata barua kutoka nyumbani ikisema ya kwamba mmoja wa ndugu zangu alikuwa ni mgonjwa sana. Ilikuwa ni Edward, aliyenifuata kwa umri. Hakika nilifikiri haukuwa mbaya sana, kwa hiyo niliamini atapona. Walakini, jioni moja siku chache baadaye nilipokuwa nikirudi kutoka mjini kupitia kwenye bwalo la chakula kwenye ranchi, niliona karatasi mezani. Nikaichukua. Ilisema, “Bill, njoo huku kwenye malisho ya kaskazini. Muhimu sana.” Baada ya kuisoma mimi pamoja na rafiki yangu tulienda kwenye malisho hayo. Mtu wa kwanza niliyekutana naye alikuwa ni maskini Mteksasi aliyefanya kazi kwenye ranchi hiyo. Jina lake lilikuwa ni Durfy, bali tulimwita “Pop.” Alikuwa na uso wenye huzuni aliposema, “Billy, jamani, nina habari za kuhuzunisha kwako.” Wakati uo huo mnyapara akaja akitembea. Wakaniambia ya kwamba barua ya simu ilikuwa ndiyo kwanza ifike, ikiniambia kuhusu kifo cha ndugu yangu.

    Rafiki mpendwa, kwa muda kidogo nisingeweza kusogea. Yalikuwa ndiyo mauti ya kwanza nyumbani mwetu. Ila ninataka kusema ya kwamba jambo la kwanza nililowazia lilikuwa kama alikuwa tayari kufa. Nilipogeuka na kuangalia mbuga hiyo pana ya majani ya manjano, machozi yalitiririka mashavuni mwangu. Jinsi nilikumbuka vile tulivyopambana kwa pamoja tulipokuwa watoto wadogo na jinsi tulivyopata shida nyingi.

    Tulienda shuleni bila chakula cha kutosha. Vidole vya miguu vilikuwa vimetokeza kwenye viatu vyetu na ilitulazimu kuvaa makoti yaliyochakaa yaliyofungwa shingoni kwa pini kwa kuwa hatukuwa na mashati. Jinsi nilivyokumbuka pia ya kwamba siku moja mama alikuwa ameweka bisi kidogo katika ndoo ndogo kwa ajili ya chakula chetu cha mchana. Hatukula pamoja na watoto wengine. Tusingeweza kupata chakula kama walichokuwa nacho. Daima tungechurupukia kilimani tupate kula. Ninakumbuka hiyo siku tulipokuwa na bisi, tulifikiri ilikuwa ni tafrija hasa. Kwa hiyo ili kuhakikisha nilipata fungu langu la hizo, nilitoka kabla ya adhuhuri na kuchota konzi nzima kabla ndugu yangu hajapata fungu lake.

    Basi nikisimama hapo nikiangalia mbuga pana iliyokaushwa na jua niliwazia juu ya mambo hayo yote na kujiuliza iwapo Mungu alikuwa amempeleka mahali bora zaidi. Ndipo tena Mungu aliniita, lakini kama kawaida, nilijaribu kuupiga vita.

    Nilijiandaa kuja nyumbani kwa ajili ya mazishi. Wakati Kasisi McKinney wa Kanisa la Port Fulton, mtu ambaye ni kama tu baba kwangu mimi, alipohubiri mazishi yake, alitamka ya kwamba “Huenda ikawa kuna wengine hapa wasiomjua Mungu, kama wapo, mkubalini sasa.” Loo, jinsi nilivyoshikilia kiti changu. Mungu alikuwa akinishughulikia tena. Msomaji mpendwa, Yeye anapoita, mwitikie.

    Sitasahau kamwe jinsi ambavyo maskini Baba yangu na Mama walivyolia baada ya yale mazishi. Nilitaka kurudi Magharibi bali Mama alinisihi sana nikae hata hatimaye nikakubali kukaa kama ningaliweza kupata ajira. Mara nikapata ajira kwenye Kampuni ya Utumishi wa Umma ya Indiana.

    Yapata miaka miwili baadaye nilipokuwa nikipima mita katika duka la mita kwenye Mtambo wa Gesi huko New Albany, nililemewa na gesi na kwa majuma kadhaa niliteseka kutokana nayo. Niliwaendea madaktari wote niliowajua. Sikuweza kupata nafuu. Niliumwa na tumbo lenye asidi, iliyosababishwa na athari ya gesi. Hali ilizidi kuwa mbaya wakati wote. Nilipelekwa kwa wataalamu huko Louisville, Kentucky. Hatimaye walisema ni kidole tumbo changu na wakasema ilibidi nifanyiwe upasuaji. Sikuweza kuamini jambo hilo kwa kuwa kamwe sikuwa na maumivu ndani ya ubavu wangu. Madaktari walisema wasingeweza kunifanyia jambo lingine lolote mpaka nifanyiwe upasuaji. Hatimaye nilikubali ufanywe bali nilisisitiza ya kwamba watumie nusukaputi ya kawaida ili kwamba niweze kuufuatilia huo upasuaji.

    Loo, nilitaka mtu fulani asimame kando yangu ambaye alimjua Mungu. Niliamini katika maombi bali sikuweza kuomba. Kwa hiyo mhudumu kutoka kwenye Kanisa la Kwanza la Kibaptisti aliambatana nami kwenye chumba cha kufanyiwa upasuaji.

    Waliponichukua kutoka mezani wakanipeleka kwenye kitanda changu, nilijisikia nikiendelea kuwa dhaifu zaidi na zaidi wakati wote. Moyo wangu ulikuwa ukidunda kwa shida. Nilihisi kifo kikiwa juu yangu. Kupumua kwangu kulikuwa kukipungua wakati wote. Nilijua nilikuwa nimefikia mwisho wa safari yangu. Ewe rafiki, ngoja mpaka utakapofika hapo wakati mmoja, ndipo utakapofikiria juu ya mambo mengi uliyofanya. Nilijua kamwe sikuwahi kuvuta sigara, kunywa pombe, wala kuwa na tabia zozote chafu bali nilijua sikuwa tayari kukutana na Mungu wangu.

    Ewe rafiki yangu, kama wewe ni mfuasi baridi na wa kawaida tu wa kanisa, utajua wakati utakapofika mwisho ya kwamba huko tayari. Kwa hiyo kama hayo tu ndiyo unayojua kumhusu Mungu wangu, ninakuomba papa hapa upige magoti na kumwomba Yesu akupe tukio lile la kuzaliwa mara ya pili, kama vile alivyomwambia Nikodemo katika Yohana mlango wa 3, na loo, jinsi ambavyo kengele za furaha zitakavyolia. Jina Lake na lisifiwe.



4) MIAKA YA UJANA - INAENDELEA





    Kulianza kuingia giza zaidi kwenye chumba hicho cha hospitali, kana kwamba kilikuwa ni kwenye msitu mkubwa. Niliweza kusikia upepo ukivuma kupitia kwenye majani, hata hivyo ilionekana ni huko mbali sana mwituni. Huenda umesikia kishindo cha upepo ukivuma kwenye majani, ukizidi kukukaribia. Niliwaza, “Vema, hiki ni kifo kikija kunichukua.” Loo! nafsi yangu ilikuwa ikutane na Mungu, nilijaribu kuomba bali sikuweza.

    Kadiri upepo ulivyosogea karibu, ndivyo ulivyozidi kutoa sauti kubwa. Majani yakatatarika na kwa ghafla, nikazimia.

    IIlionekana basi kana kwamba nilirudia tena kuwa mvulana mdogo pekupeku, nimesimama kwenye ule ujia chini ya mti ule ule. Nikasikia sauti ile ile iliyosema, “Usinywe pombe kamwe wala kuvuta sigara.” Na majani niliyosikia yalikuwa ni yale yale yaliyovuma katika ule mti siku ile.

    Lakini wakati huu ile Sauti ilisema, “Nilikuita nawe hukukubali kwenda.” Ikarudia kwa mara ya tatu.

    Ndipo nikasema, “Bwana, kama huyo ni Wewe, nijalie nirudi tena duniani nami nitaihubiri Injili Yako hadharani na pembeni mwa barabara. Nitamwambia kila mtu habari zake!”

    Wakati ono hili lilipopita, nilikuta ya kwamba sikuwa nimepata kujisikia vizuri zaidi. Daktari wangu mpasuaji alikuwa angali yumo humo jengoni. Alikuja na akaniangalia na akashangaa. Alionekana kana kwamba alifikiri ningekuwa nimekufa, ndipo akasema, “Mimi si mtu anayeenda kanisani, kazi yangu ni kubwa mno, bali ninajua Mungu amemzuru mvulana huyu.” Kwamba ni kwa nini yeye alisema hivyo, sijui mimi. Hakuna mtu aliyekuwa amesema jambo lolote kuhusu jambo hilo. Kama ningalikuwa nimejua wakati huo ninachojua sasa, ningalitoka kwenye kitanda hicho nikipaza sauti Sifa kwa Jina Lake.

    Baada ya siku chache niliruhusiwa kurudi nyumbani, bali nilikuwa ningali mgonjwa na nililazimika kuvaa miwani machoni mwangu kwa sababu ya dosari katika jicho. Kichwa changu kilitikisika nilipoangalia kitu chochote kwa kitambo kidogo.

    Nilianza kumwomba na kumtafuta Mungu. Nilienda toka kanisa moja hadi lingine, nikijaribu kupata mahali fulani ambapo palikuwa na wito wa madhabahuni wa mtindo wa kale. Jambo la kuhuzunisha lilikuwa kwamba sikuweza kupata popote.

    Nilisema ya kwamba kama ningejaliwa kuwa Mkristo, kweli ningekuwa Mkristo hasa. Mhudumu aliyenisikia nikitoa tamshi hilo alisema, “Sasa Billy jamani, unaelekea kwenye ulokole.” Nikasema ya kwamba kama kamwe nikipata dini, nilitaka kuisikia wakati ikija, kama tu vile wanafunzi walivyofanya.

    Loo Jina Lake lisifiwe. Nilipata dini baadaye kidogo na ningali ninayo, na kwa msaada Wake, nitaidumisha daima.

    Usiku mmoja nilimwonea Mungu njaa sana na kuonea njaa tukio halisi hata nilitoka nikaenda nje nyuma ya nyumba kwenye kibanda cha zamani na kujaribu kuomba. Sikujua jinsi ya kuomba wakati huo kwa hiyo nilianza tu kuongea Naye kama vile ambavyo ningeongea na mtu yeyote yule. Mara kukatokea Nuru huko bandani na ikafanya msalaba na Sauti iliyotoka msalabani ikasema nami katika lugha ambayo sikuweza kuifahamu. Kisha ikaondoka ikaenda zake. Nilipigwa na bumbuazi. Nilipojirudia tena niliomba, “Bwana, kama huyo ni Wewe, naomba uje uzungumze nami tena.” Nilikuwa nikisoma Biblia yangu tangu niliporudi nyumbani toka hospitalini na nilikuwa nimesoma katika I Yohana 4, “Wapenzi, msiiamini kila roho, bali zijaribuni hizo roho, kwamba zimetokana na Mungu.”

    Nilijua ya kwamba roho fulani alikuwa amenitokea, na nilipoomba alitokea tena. Ndipo ilionekana kana kwamba kulikuwako na ratili elfu moja zilizonyanyuliwa toka kwenye nafsi yangu. Niliruka juu na kukimbilia nyumbani na ilionekana kana kwamba nilikuwa nikikimbia hewani.

    Mama akauliza, “Bill, umepatwa na kitu gani?” Nikajibu, “Sijui bali kwa kweli ninajisikia vizuri na mwepesi.” Singeweza kukaa hapo nyumbani tena. Ilibidi nitoke nje na kutimua mbio.

    Nilijua basi ya kwamba kama Mungu alinitaka nihubiri, angeniponya. Kwa hiyo nilienda kwenye kanisa lililoamini katika kupaka mafuta, nami nikaponywa papo hapo. Niliona basi ya kwamba wale wanafunzi walikuwa na kitu fulani ambacho wahudumu wengi sana siku hizi hawanacho. Wanafunzi walibatizwa na Roho Mtakatifu na kwa hiyo waliweza kuponya wagonjwa na kufanya miujiza mikuu katika Jina Lake. Kwa hiyo nikaanza kuomba kwa ajili ya ubatizo wa Roho Mtakatifu na nikaupata.

    Siku moja yapata miezi sita baadaye, Mungu alinipa shauku ya moyo wangu. Alisema nami katika Nuru kuu, akiniambia niende nikahubiri na kuwaombea wagonjwa Naye angewaponya haidhuru walikuwa na ugonjwa wa namna gani. Nikaanza kuhubiri na kufanya yale ambayo aliniambia nifanye. Ee rafiki, siwezi kuanza kukwambia yale yote yaliyotendeka: Macho mapofu yalifumbuliwa. Viwete walitembea. Kansa zimeponywa, na kila namna ya miujiza imetendwa.

    Siku moja mwishoni mwa Barabara ya Spring, Jeffersonville, Indiana, baada ya uamsho wa majuma mawili, nilikuwa nikibatiza watu 130. Ilikuwa ni siku yenye joto ya Agosti na kulikuwako na watu kama 3,000. Nilikuwa karibu na kumbatiza mtu wa 17 wakati mara moja niliisikia ile Sauti ndogo, tulivu tena na ikasema, “Angalia juu.” Mbingu zilikuwa kama shaba kwenye siku hiyo yenye joto ya Agosti. Hatukuwa na mvua kwa yapata majuma matatu. Niliisikia Sauti hiyo tena, na halafu tena mara ya tatu ikasema, “Angalia juu.”

    Nikaangalia juu na nyota kubwa inayoangaza ikashuka kutoka mbinguni, ambayo nilikuwa nimeiona mara nyingi hapo kabla bali sikuwa nimewaambia habari zake. Mara nyingi nimewaambia watu juu ya kuonekana kwake nao wangecheka tu na kusema, “Bill, unawazia tu hayo. Ama labda ulikuwa unaota.” Lakini Mungu asifiwe, wakati huu alikuwa amejionyesha wazi kwa wote, kwa sababu ilikuja karibu sana nami hata sikuweza kuzungumza. Baada ya sekunde chache kupita nilipaza sauti na watu wengi wakaangalia juu na kuiona hiyo nyota juu yangu kabisa. Wengine walizimia wakati wengine wakipiga makelele na wengine wakakimbia. Ndipo hiyo nyota ikarudi mbinguni na mahali ilipokuwa imeondoka palikuwa ni futi kumi na tano mraba na mahali hapa pakaendelea kusogea na kuvurugika ama kana kwamba mawimbi yalikuwa yakifingirika. Mahali hapa palikuwa pamefanya wingu dogo jeupe na hiyo nyota ilitwaliwa juu katika wingu hili dogo.

Kama vile Yohana Mbatizaji, nabii huyu alithibitishwa kwenye maji ya Ubatizo.



5) KUZURIWA NA MALAIKA

" 


Maono yaliendelea. Aliambiwa na makasisi wenzake ya kwamba maono yake hayakutoka kwa Mungu. Aliambiwa alikuwa amepagawa na roho mchafu. Hili lilimsumbua sana. Mzigo huo ukawa mzito sana asingeweza kuubeba, kwa hiyo akaenda nyikani akayatafute Mapenzi ya Mungu. Alikuwa amejitolea sana hivi kwamba aliapa kutorudi bila jibu. Ilikuwa ni kule, kwenye kibanda cha kale cha kutega wanyama, ndipo Malaika wa Bwana alipompa agizo lake. Miongoni mwa mambo mengine, Malaika huyo alimwambia hivi: “Ukiwafanya watu wakuamini wewe, na uwe mwaminifu unapoomba, hakuna kitakachosimama mbele ya maombi yako, si hata kansa.”

Tashwishi zote ziliondoka. Sasa alikuwa na agizo na kwa ujasiri akajitokeza. Uamsho wa uponyaji ulikuwa umeanza.

Mamia ya maelfu walihudhuria miamsho ya Branham. Maelfu waliponywa katika Jina la Bwana Yesu Kristo. Wainjilisti wengine kama vile Oral Roberts, T.L. Osborn, na A.A. Allen mara wakamfuata Ndugu Branham na kuanzisha miamsho yao wenyewe ya uponyaji. Bwana alizimimina baraka Zake kuliko hapo awali. Mkono wa uponyaji wa Yesu Kristo mara nyingine tena ulikuwa umewagusa watu Wake.

  • Kasisi F.F. Bosworth, mwinjilisti anayejulikana ulimwenguni kote na mmoja wa wazee waanzilishi wa dhehebu la Assemblies of God pamoja na mfumo wa siku hizi wa Upentekoste.

    “Mara nyingi nimelia kwa furaha kuhusu karama ya hivi karibuni ya Mungu kwa kanisa la ndugu yetu mpendwa, William Branham, pamoja na karama yake ya ajabu sana ya uponyaji. Hili ni jambo la Mungu kufanya mambo ya ajabu mno kuliko yote tuyaombayo au tuyawazayo (Efe. 3:20), kwa maana kamwe sijapata kuona wala kusoma juu ya chochote kinachofanana na huduma ya uponyaji ya William Branham.”


  •    Kasisi Gordon Lindsay, mwandishi hodari, mhudumu, na mwanzilishi wa Chuo cha Kristo kwa Mataifa Yote.
    “Katika tukio moja, tuliangalia wakati akizungumza na mtu fulani aliyelala kwenye machela. Mwanzoni hakukuwako na ishara yoyote ya jibu la kueleweka kutoka kwa mtu huyo. Baadaye maelezo yalitoka kwa mkewe aliyekuwa amesimama hapo karibu, ya kwamba mtu huyo hakuwa tu akifa kwa kansa, bali alikuwa ni kiziwi wala asingeweza kusikia yaliyokuwa yakisemwa.

    Ndugu Branham basi akasema ya kwamba ingefaa mtu huyo kupokea kusikia kwake ili kwamba aweze kumwelezea kuhusu kuponywa kwa kansa yake. Kulikuwa na muda mfupi wa maombi. Mara moja mtu huyo aliweza kusikia! Machozi makubwa makubwa yalitiririka mashavuni mwa mtu huyo ambaye uso wake jioni nzima ulikuwa haushiriki kitu kabisa na haukuonyesha hisia yoyote. Alisikiliza kwa shauku kuu alipokuwa akiambiwa juu ya ukombozi wake kutokana na kansa.”


  
  •     William D. Upshaw, Mbunge wa Marekani (1919-1927), alipigania Urais wa Marekani katika mwaka wa 1932. Alikuwa ni kiwete tangu alipoanguka akavunja mgongo wake akiwa mtoto. Alikuwa na umri wa miaka 84 wakati alipoponywa kabisa kutokana na maombi ya Ndugu Branham, baada ya kuwa kiwete kwa muda wa miaka 66. Kamwe hakuhitaji tena kiti cha magurudumu ama mikongojo hata mwisho wa maisha yake.
    “Ndugu Branham akasema, ‘Huyo Mbunge ameponywa.’ Moyo wangu ukaruka. Nikapiga hatua nikatoka na kumkubali Bwana kama Mponyaji wangu. Nikaweka kando mikongojo yangu…ndipo upande wa chini wa Mbinguni ukaanguka!”

  • Georgia Carter, Milltown Indiana, aliponywa ugonjwa wa kufisha wa T.B. mwaka wa 1940 wala kamwe hakuugua ugonjwa huo hata wakati mmoja tena maishani mwake. Anawakilisha makumi elfu ya watu ambao wameponywa kupitia kwa huduma yake na wangali wanaponywa leo.
    “Nilikuwa nimelala chali kwa muda wa miaka minane na miezi tisa nikiwa na T.B. na madaktari walikwishanikatia tamaa. Hata sikuwa nimefikisha uzito wa ratili 50 na ilionekana kana kwamba matumaini yote yalikuwa yamekwisha. Ndipo kutoka Jeffersonville, Indiana, alikuja Kasisi WM Branham katika ono alilokuwa ameona la mwana-kondoo akiwa ameshikwa kichakani na alikuwa akilia ‘Milltown’, ambako ndiko ninakoishi. Ndugu Branham hakuwa amewahi kuja huku wala kujua mtu yeyote aliyetoka huku. Akiingia, aliweka mikono juu yangu na akaomba, akiliitia juu yangu Jina la Bwana wetu mpenzi Yesu. Kitu fulani kilionekana kunishika na kwa ghafla nilikuwa nimeamka na kumshukuru Mungu kwa nguvu Zake za kuponya. Sasa mimi ni mpiga piano kwenye kanisa la Kibaptisti hapa.”

  

6) ILE NGUZO YA MOTO

" 


Mara nyingi Ndugu Branham hutoa sifa za Nguzo ya Moto iliyoithibitisha huduma yake. Ilikuwako alipozaliwa, ilionekana na maelfu ukingoni mwa Mto Ohio, na ilionekana kumfuata kokote alikoenda. Ilikuwa ni mwaka wa 1950 ambapo Bwana aliwapa waaminio na wasioamini vile vile thibitisho lisilokanushika ya kwamba Nguzo hii ya Moto ilikuwa pamoja na nabii huyu.

Usiku huo ulikuwa umegubikwa na ubishi kwenye Jumba Kubwa la Mikutano la Sam Houston. Ndugu Branham alikuwa akiongoza uamsho wa uponyaji uliokuwa ukienea nchini. Baraka za Bwana Yesu zilikuwa zikimiminika kama mvua kwenye mashamba ya ngano ya kiroho. Bali hizo ishara kuu na maajabu hazikutokea bila upinzani. Kama ilivyo kawaida siku zote, adui alimwinua mshindani. Vikosi hivyo viwili vilikutana Houston, Texas, Naye Malaika wa Bwana Mwenyewe akashuka kupiga vita.

Maelfu tayari walikuwako kushuhudia miujiza isiyohesabika iliyomfuata mtu huyu wa Mungu. Siku moja kabla, kundi la wahudumu walimpa changamoto nabii kufanya mjadala juu ya uponyaji wa Kiungu, bali changamoto hiyo ilimwangukia rafiki mzee mwaminifu wa nabii, Kasisi F.F. Bosworth. Hao wenye kushuku wengi waliongozwa na mhudumu wa mahali hapo wa Kibaptisti na ambaye ni mnenaji mkosoaji wa uponyaji wa kiungu. Mjadala huo uliokuwa unakuja ulifichuliwa kwa magazeti, ambayo upesi yalichapisha vichwa vya habari, “Manyoya ya Kitheolojia Yatapeperushwa Saa 1 usiku Wa Leo Katika Jumba Kubwa la Mikutano La Sam Houston.”

Mpinzani alimkodisha mpiga picha mweledi, Ted Kipperman wa Studio za Douglas, apate kunakili mjadala huo kwa picha. Jioni hiyo, picha zilipigwa za Ndugu Bosworth akiwa amesimama kwa ustaha huku huyo mwenye kushuku akiwa katika mikao ya kumtishia; wakati mmoja kidole chake kimekitwa kwenye uso wa mzee huyo mnyenyekevu.

Mjadala huo ulipoanza, Kasisi Bosworth upesi alithibitisha uhakika wa uponyaji wa Kiungu kwa ushuhuda wa Maandiko na halafu, kusudi asiliache swali lo lote, akawaomba wote waliokuwa wameponywa maradhi yao kusimama. Maelfu wakasimama kwa miguu yao. Baada ya hao walioponywa kuketi chini, aliwaomba wale wote waliokuwa wameponywa kwa uponyaji wa Kiungu waliokuwa ni wafuasi wenye sifa njema wa dhehebu la mtu huyu wangesimama. Wafuasi mia tatu wa kanisa hilo wakasimama na kwa fahari wakaonyesha rehema ambayo Bwana Yesu alikuwa amewaonyesha.

Changamoto basi ikatokea kwa huyo mwenye kushuku. “Hebu huyo mponyaji wa Kiungu ajitokeze. Hebu atende kazi.” Ndugu Bosworth akasema wazi ya kwamba Yesu alikuwa Ndiye Mponyaji pekee wa Kiungu, bali kelele za majigambo ya mkosoaji yakaendelea. Hatimaye, Ndugu Bosworth akamwalika Ndugu Branham jukwaani. Akakubali mwaliko huo huku kukiwako na makelele ya shangwe ya kumuunga mkono.

Nabii, huku amejazwa na Roho Mtakatifu, alitoa jibu hili:


    Siwezi kumponya mtu yeyote. Nasema jambo hili. Wakati nilipokuwa mtoto mchanga aliyezaliwa katika Mkoa wa Kentucky, kulingana na mama yangu mpendwa, na jambo ambalo limethibitishwa maishani mwangu mwote, kuna Nuru iliyoingia kwenye chumba cha kibanda maskini kile kilichosongamana vitu kule, mahali kilipokuwa, hakijasakafiwa, hata hakikuwa na dirisha, walikuwa tu na maskini kitu fulani cha kale kama dirisha pale, kama kijilango, nao wakakisukuma wakakifungua yapata saa kumi na moja alfajiri, na Nuru hii ikazunguka ikaingia kama wakati tu kukipambazuka. Tangu wakati huo, imekuwa pamoja nami. Ni Malaika wa Mungu. Alikutana nami uso kwa uso miaka michache iliyopita. Kote katika maisha yangu, Yeye aliniambia mambo ambayo yametukia, nami nimeyasimulia tu kama vile alivyoniambia. Nami ninampa changamoto mtu yeyote mahali popote, aende kwenye mji niliolelewa, ama popote pale, ambapo tamshi limepata kutolewa katika Jina la Bwana, ila lile lililotimia vile vile hasa jinsi lilivyosemwa lingekuwa.

Baada ya kusema maneno hayo, Roho Mtakatifu alishuka hapo jukwaani, naye mpiga picha mwenye kusisimkwa akapiga picha. Ndugu Branham aliondoka jukwaani kwa tamshi rahisi, hata hivyo la kinabii: “Mungu atashuhudia. Sitasema zaidi.”

Mwenziwe Bw. Kipperman upesi alienda kuzisafisha picha hizo kwa ajili ya taarifa za habari za kesho yake asubuhi. Aliona kitu cha ajabu alipokuwa akiitoa picha ya kwanza kutoka kwenye mmumunyo wa kusafishia. Hiyo, kama picha zingine tano zilizofuata, ilikuwa ni tupu. Aliushika moyo wake akaanguka kufudifudi wakati alipotoa picha ya mwisho kutoka kwenye mmumunyo huo. Hapo, kwenye picha hiyo ya mwisho, kulikuwako na ile Nguzo ya Moto katika umbo linaloonekana imetulia juu ya kichwa cha nabii wa Mungu, William Marrion Branham.

Wana wa Israeli waliishuhudia ile Nguzo ya Moto ikimwongoza Musa, nao watu wa siku hizi wameishuhudia Nguzo ile ile ya Moto ikimwongoza nabii mwingine.
Picha hiyo upesi ilipelekewa George J. Lacy, Mchunguzi Mweledi wa Hati Zinazoshukiwa wa F.B.I. ya Marekani, ambaye aliihakiki picha hiyo kwa maoni yake ya kitaalamu. Hati rasmi iliyotolewa na Bw. Lacy iko kwenye ukurasa unaofuata. 

Hii ilikuwa ni mapema zaidi kabla ya makompyuta na kamera za tarakimu, wala haingeweza kuelezewa kwa njia zozote zinazojulikana na sayansi, mbali na kwamba kulikuwa na Nuru halisi juu ya kichwa cha William Branham. Leo hii picha hiyo hiyo inaweza kuonekana kwenye Maktaba ya Bunge la Marekani, katika makao makuu ya taifa, Washington DC.





7) SIRI ZIMEFUNULIWA

" 


Mapema katika huduma ya Ndugu Branham ilikuwa wazi kwamba mfumo wa kimadhehebu uliundwa kuyaendeleza madhehebu ya kidini, wala si Injili ya kweli. Ndugu Branham aliiamini Biblia Neno kwa Neno, wala asingepatana, hata kama ilimaanisha kutengwa na wenzake, marafiki, ama familia.

Wakati angali akiwa ni mfuasi wa Kanisa la Kimishenari la Baptisti, aliombwa kuwaweka wakfu wahudumu wanawake. Hata hivyo, yeye alijua Maandiko vizuri sana. I Timotheo 2:12 inasema dhahiri, “Simpi mwanamke ruhusa ya kufundisha, wala kumtawala mwanamume; bali awe katika utulivu,” na I Wakorintho 14:34 inasema, “Wanawake na wanyamaze katika makanisa, maana hawana ruhusa kunena…” Hii haikuwa ni kuwapinga wanawake, bali Biblia ilikuwa imeliandika dhahiri jambo hilo. Wakati mkataa ulipotolewa, yeye asingepatana kwa hiyo akaliacha kanisa hilo.

Hilo halikuwa ndilo Andiko la pekee lililopuuzwa na madhehebu. Bwana alimfunulia Ndugu Branham ukweli juu ya ubatizo. Yesu angewezaje kuagiza, “Basi enendeni, mkawafanye mataifa yote kuwa wanafunzi, mkiwabatiza kwa jina la Baba, na la Mwana, na la Roho Mtakatifu,” hata hivyo kila ubatizo uliorekodiwa katika Biblia ulikuwa ni katika Jina la Yesu? Mtume Petro aliagiza katika Matendo 2:38 kutubu na kubatizwa katika Jina la Yesu Kristo. Maandiko hutenda kazi katika umoja mkamilifu, bali ilihitaji nabii kuifunua siri hii: “Baba” si jina, “Mwana” si jina, na “Roho Mtakatifu” si jina. Ni kama tu vile mtu mmoja ni baba kwa watoto wake, mwana wa wazazi wake, na ndugu wa ndugu zake, hata hivyo jina lake si “baba,” “mwana,” wala “ndugu.” Baba, Mwana, na Roho Mtakatifu ni sifa za Jina Lake Yesu Kristo. Mathayo 28:19 na Matendo 2:38 yamekuja kulingana kikamilifu.

Hata ile dhambi ya asili katika Bustani ya Edeni ilifunuliwa, sio kama kula tunda, bali ni jambo ovu zaidi. Je! kula kipande cha tunda kungewezaje kuwafunulia Adamu na Hawa mara moja kwamba walikuwa uchi? Kwa kweli haileti maana. Tofaa lina uhusiano gani na uchi? Nabii wa Mungu aliifunua siri hii wazi wazi.

Malaika walionenwa habari zao katika Ufunuo mlango wa 2 na wa 3 ni akina nani? Huenda majina yao yakasikika yanafahamika.

Wale wapanda farasi wa kisiri wa Ufunuo mlango wa 6 ni akina nani? Wana jambo moja shirika lililo muhimu sana.

Je! Marekani imetajwa katika Kitabu cha Ufunuo?

Wale 144,000 waliookolewa katika mlango wa 7 ni akina nani?

Yule kahaba mkuu wa mlango wa 17 ni nani? Utambulisho wake na siri hizi zote zilifunuliwa katika Ujumbe wa nabii huyu mkuu aliyetumwa kutoka kwa Mungu.

Si kwamba tu miujiza isiyohesabika ilimfuata mtu huyu, bali siri zilizofichwa katika Biblia katika nyakati zote pia zilifunuliwa katika huduma yake. Ilionekana wazi kwamba nabii huyu alitimiza Maandiko mengi zaidi mbali na Malaki 4.

Ufunuo 10:7: Isipokuwa katika siku za sauti ya malaika wa saba atakapokuwa tayari kupiga baragumu; hapo ndipo siri ya Mungu itakapotimizwa, kama alivyowahubiri watumishi wake hao manabii.

Sauti inawalilia walimwengu watoke kwenye madhehebu na walirudie Neno asili la Mungu. Kila mmoja wetu ana nafasi ile ile waliyokuwa nayo Petro, Yakobo, na Yohana. Tuna nafasi ya kuhesabiwa pamoja na wachache wa Mungu walioteuliwa ambao wasingeyasujudia madhehebu ya kidini ya siku hizi.

Maandiko matakatifu yamenakili maisha na matendo ya watu waliotembea pamoja na Mungu na walikuwa wametiwa mafuta sana na Roho hata walitangaza BWANA ASEMA HIVI, nayo maneno yao yakathibitishwa kwa ishara na maajabu yasiyoweza kukosea. Walikuwa ni manabii wa Mungu, na Sauti ya Mungu kwa kizazi chao.

Je! nyakati ziko tofauti sasa na vile zilivyokuwa wakati Yesu alipokuwa hapa? Viongozi wa dini ndio waliomsulibisha. Wanafunzi walikuwa wachache mno miongoni mwa mfumo mkubwa sana wa kidini. Walitengwa, wakadhihakiwa, na hatimaye wakauawa kwa kuchukua msimamo dhidi ya mfumo wa madhehebu makubwa. Huenda tusiuawe kwa ajili ya imani zetu siku hizi, bali hakika tunateswa. Kama vile Mafarisayo na Masadukayo, wao hawawezi kuikana miujiza iliyoifuata huduma ya Ndugu Branham kwa hiyo wanakimbilia kufanya mashambulizi ya namna nyingine. Huenda ukasikia ya kwamba yeye alikuwa ni nabii wa uongo, kiongozi wa kundi lililojitenga, ama mabaya zaidi. Kwa kweli, yeye alikuwa ni mtu mnyenyekevu wa Mungu ambaye alisimama imara dhidi ya utawala wa kimabavu ambao madhehebu na vikundi vya dini yanao juu ya watu wa Mungu. Walimshambulia Yesu jinsi hiyo hiyo wakati Yeye alipopinga mafundisho yao ya sharti na mapokeo.

Mungu aliuheshimu msimamo wa Ndugu Branham wa kuamini kila Neno katika Biblia, Naye anaitumia huduma yake kuwaongoza mamilioni ya watu kwa Yesu Kristo. Leo hii, Sauti ya Malaika wa Saba inapiga baragumu kwa nguvu vile vile ilivyopata kuipiga. Kadiri ya watu milioni mbili ulimwenguni kote wanauamini Ujumbe wa Ndugu Branham. Huenda hii ikawa ni uchache mdogo sana wa watu bilioni mbili wanaokiri Ukristo, lakini je! ni wakati gani ambapo watu wa Mungu hawakuwa katika uchache?

Tuna zaidi ya jumbe 1,200 zilizorekodiwa zilizo na Sauti ambayo ilitabiriwa ingekuja katika Ufunuo 10:7. Kila moja ya jumbe hizi inafungua siri zaidi za Mungu. Sauti hiyo inapatikana kwa ajili yako kama unapenda kuisikia.


CHAGUO NI LAKO


Rev. William Marrion Branham;
"Kamwe siwaletei watu ujumbe kusudi wanifuate, ama wajiunge na kanisa langu, ama waanzishe shirika na dhehebu fulani. Sijafanya hivyo kamwe wala sitafanya hivyo sasa. Sina haja ya mambo hayo, bali nina haja ya mambo ya Mungu pamoja na watu, na kama naweza kulitimiza jambo moja tu nitaridhika. Jambo hilo moja ni kuona uhusiano wa kweli wa kiroho baina ya Mungu na watu umeimarishwa, ambapo watu wanakuwa viumbe vipya katika Kristo, wamejazwa na Roho Wake na wanaishi kulingana na Neno Lake. Ningewaalika, ningewasihi na kuwaonya watu wote waisikie sauti Yake wakati huu, na kuyatoa maisha yenu kabisa Kwake, hata kama vile ninavyoamini moyoni mwangu kwamba nimeyatoa yangu yote Kwake. Mungu awabariki, na hebu kuja Kwake na kuifurahishe mioyo yenu."

(CHANZO)

http://themessage.com/sw/home

THEMESSAGE.COM
P.O. Box 950
Jeffersonville, IN 47131, USA
812-256-1177



https://rejeabiblia.com/je-dhambi-ya-mauti-ni-ipi-1yohana-516-17/