"Tazama, naja kama mwivi. Heri akeshaye, na kuyatunza mavazi yake, asiende uchi hata watu wakaione aibu yake...ufunuo 16:15"

Monday, September 26, 2016

MVUTO WA TATU!

Bwana  wetu Yesu Kristo alipokuwa hapa duniani, huduma yake iligawanyika katika sehemu kuu tatu.
ya kwanza:  huduma ya uponyaji, ishara na miujiza
ya pili: kueleza siri za mioyo ya watu, kama vile kwa yule mwanamke msamaria,
ya tatu: kuhubiri neno la Baba yake.

ndugu William Branham alifundishwa na malaika wa Bwana jinsi ya kuvua samaki WAKUBWA kutoka kwenye maji, na yule malaika alimwambia ni kwa namna hiyo hiyo Bwana Yesu Kristo aliitumia kuwavuta watu wake kwake kutoka kwenye dhambi alipokuwa hapa duniani

MVUTO WA KWANZA:
alielezwa kuwa baada ya kuweka mnofu wa kuwavutia samaki kwenye ndoano na kuitupa ndoano  majini baada ya muda kidogo utaivuta juu, wale samaki wadogo wataiona na kuifuata na kuizingira ila wale wakubwa watasogea tu karibu na tukio kuhakikisha kama ni chakula halisi, huo ndio mvuto wa kwanza.

MVUTO WA PILI:
baada ya muda tena kidogo utaivuta ndoano juu tena ila isitoke yote, na wale samaki wadogo waliokuwa wameizunguka ndoano, watakimbia lakini wale samaki wakubwa, watakikaribia na kukila na kunaswa,

MVUTO WA TATU:
baada ya wale samaki wakubwa kunaswa katika mvuto wa pili sasa ni wakati wa kumalizia mvuto wa mwisho.na huu ndio wa kumtoa samaki nje ya maji.

sasa kanisa la Mungu lipo katika mvuto wa tatu ambao ni NENO LA MUNGU, kuandaliwa kwenda kwenye unyakuo, ishara na miujiza haviwezi kutukamilisha hivyo vyote vilikuwa vinatuandaa kwa ajili ya mvuto wa tatu, ambao ni kusikia neno la Mungu,
 tunawashauri wakristo wayatazame mafundisho haya, yameelezea vizuri zaidi kuhusu MVUTO WA TATU,



MUNGU AKUBARIKI





1 comment:

  1. Really appreciate this wonderful post that you have provided for us.Great site and a great topic as well i really get amazed to read this. Its really good. Tattoo artists near you

    ReplyDelete