"Tazama, naja kama mwivi. Heri akeshaye, na kuyatunza mavazi yake, asiende uchi hata watu wakaione aibu yake...ufunuo 16:15"

Sunday, April 9, 2017

MASWALI NA MAJIBU: SEHEMU YA 11


SWALI: Ufunuo 20:7  "Na hiyo miaka elfu itakapokwisha, Shetani atafunguliwa, atoke kifungoni mwake;
8 naye atatoka kuwadanganya mataifa walio katika pembe nne za nchi, Gogu na Magogu, kuwakusanya kwa vita, ambao hesabu yao ni kama mchanga wa bahari.
9 Wakapanda juu ya upana wa nchi, wakaizingira kambi ya watakatifu, na mji huo uliopendwa. Moto ukashuka kutoka mbinguni, ukawala."
 Je!, hawa watu ambao shetani atawashawishi kuishambulia kambi ya watakatifu watatoka wapi wakati katika ule utawala wa miaka 1000 hakukuwa na waovu?
JIBU: Katika utawala wa miaka 1000 biblia inarekodi kuwa wenye dhambi watakuwepo, lakini dhambi  haitatawala dunia kwasababu mkuu wa ulimwengu ule atakuwa ni MFALME WA AMANI yaani Yesu Kristo, tofauti na dunia ya sasa ambayo mkuu wa ulimwengu huu ni shetani. Dhambi na wenye dhambi watakuja kuondolewa wote mara tu baada hukumu ya kile kiti cheupe cha Mungu ambayo itakuja baada ya utawala wa miaka 1000 kuisha. Kwahiyo kama vile biblia inavyosema Kristo atatawala kwa fimbo ya chuma pamoja na sisi  ukisoma..
ufunuo 2:26-27" Na yeye ashindaye, na kuyatunza matendo yangu hata mwisho, nitampa mamlaka juu ya mataifa,
27 naye atawachunga kwa fimbo ya chuma, kama vyombo vya mfinyanzi vipondwavyo, kama mimi nami nilivyopokea kwa Baba yangu. "
(fimbo ya chuma inamaana >> ni utii chini ya kila kitakachoamriwa pasipo majadiliano wala mahojiano, kwa atakayekaidi atalazimika kutumikia adhabu kali ). Hautakuwa utawala wa kimabavu bali ni wa amani na utaratibu lakini kwa watakaokuwa wanaenda kinyume na sheria ya Mfalme na watakatifu wake wataangukia laana, soma zekaria 14 yote inaelezea adhabu zitakazowakuta mataifa wasiokwenda kumwabudu mfalme mwaka kwa mwaka Yerusalemu,
  pia isaya 65:17-20" 17 Maana, tazama, mimi naumba mbingu mpya na nchi mpya, na mambo ya kwanza hayatakumbukwa, wala hayataingia moyoni.
18 Lakini furahini, mkashangilie daima, kwa ajili ya hivi niviumbavyo; maana, tazama, naumba Yerusalemu uwe shangwe, na watu wake wawe furaha.
19 Nami nitaufurahia Yerusalemu, nitawaonea shangwe watu wangu; sauti ya kulia haitasikiwa ndani yake tena, wala sauti ya kuomboleza.
20 Hatakuwapo tena mtoto wa siku chache, wala mzee asiyetimia siku zake; kwa maana mtoto atakufa mwenye umri wa miaka mia; bali mtenda dhambi mwenye umri wa miaka mia atalaaniwa. "
Hivyo tunaona atakayetawaliwa hapo kwa fimbo ya chuma sio mkristo bali watakuwa ni watu wengine watakaokuja kuzaliwa ndani ya huo utawala wa miaka 1000. Maana ile siku ya mwisho ya Bwana atakayokuja pamoja na sisi kuuharibu ulimwengu wa sasa haitamaliza watu wote bali kuna watu wachache watakaosalia,soma
 Isaya 13:9-13"  Tazama, siku ya Bwana inakuja, siku kali, ya hasira na ghadhabu kuu, ili iifanye nchi kuwa ukiwa, na kuwaharibu watu wake, wenye dhambi, wasikae ndani yake.
10 Maana nyota za mbinguni na matangamano havitatoa nuru yake; jua litatiwa giza wakati wa kucha kwake, na mwezi utaacha nuru yake isiangaze.
11 Nami nitaadhibu ulimwengu kwa sababu ya ubaya wake, na wenye dhambi kwa sababu ya hatia yao; nami nitaikomesha fahari yao wenye kiburi; nami nitayaangusha chini majivuno yao walio wakali;
12 nitafanya wanadamu kuadimika kuliko dhahabu safi, na watu kuliko dhahabu ya Ofiri.
13 Kwa hiyo nitazitetemesha mbingu, na dunia itatikiswa itoke katika mahali pake, kwa sababu ya ghadhabu ya Bwana wa majeshi, na kwa sababu ya siku ya hasira yake kali. "
hao ndio watakaopata neema ya kuingia katika utawala wa miaka 1000 katika miili yao ya asili(hawa ndio watakaokuwa wakizaa na kuzaliana) lakini sisi tutakao kuja na Kristo kutakuwa hakuna kuzaa wala kuzaliana kwa sababu tutakuwa na ile miili ya utukufu iliyotoka mbinguni,
 Na baadhi ya hawa watu  baadaye shetani atakapokuja kufunguliwa kuwajaribu ndio watakaotaka kufanya vita dhidi ya watakatifu, kama biblia inavyosema moto utashuka kutoka mbinguni na kuwameza wote. ndipo hukumu ya kiti cheupe itafuata ambapo waovu wote watahukumiwa na kutupwa katika ziwa la moto pamoja na shetani na kisha tutaingia katika umilele ambapo dhambi haitakuwepo wala waovu.

No comments:

Post a Comment