"Tazama, naja kama mwivi. Heri akeshaye, na kuyatunza mavazi yake, asiende uchi hata watu wakaione aibu yake...ufunuo 16:15"

Monday, May 28, 2018

MASWALI NA MAJIBU: SEHEMU YA 24

SWALI 1: marko2:18"Nao wanafunzi wa Yohana na Mafarisayo walikuwa wakifunga; basi walikuja, wakamwambia, Kwani wanafunzi wa Yohana na wanafunzi wa Mafarisayo hufunga bali wanafunzi wako hawafungi? SASA BWANA ALIKUSUDIA Nini kuwajibu hivi?19"Yesu akawaambia, WALIOALIKWA HARUSINI WAZAJE KUFUNGA maadamu bwana-arusi yupo pamoja nao?(BWANA ALIKUWA ANAMAANISHA NINI KUSEMA HIVYO?
JIBU: shalom! Mfano huo sawa tu, na mwanafunzi aliye na mwalimu wake, pindi anapokuwa naye anao uwezo wa kumuuliza swali lolote na likajibiwa, au akampelekea mwalimu wake maswali yote magumu yanayomsumbua na yakatatuliwa pindi wakati yupo naye, lakini kikifika kipindi cha mitihani, labda mtihani wa NECTA, pale ambapo anawajibika kuketi mwenyewe kwenye chumba cha mtihani mahali ambapo mwalimu wake hawezi kuwepo tena hapo ndipo itampasa atumie nguvu na jitihada ya ziada kutatua maswali yote peke yake anayokutana nayo kwa maarifa aliyopewa na mwalimu wake, lakini hapo mwanzo angeweza kumpelekea tu kila swali linalokuja mbele yake na akasaidiwa pasipo hata kujishughulisha...

Na ndivyo ilivyokuwa kwa mitume wa BWANA wetu YESU KRISTO wao walipewa neema ya kipekee kutembea na Mungu( BWANA YESU) duniani tofauti na wanafunzi wa Yohana au masadukayo, sasa unategemea vipi watu kama hao wafunge, au kujisumbua kwa lolote, wakati wanayemwomba wapo naye hapo hapo...wakiwa wanahitaji ufunuo wa jambo fulani si wanamkimbilia BWANA  na kumuuliza kwasababu yupo nao hapo?!!!...Na ndio maana akasema wakati utafika Bwana arusi atakapoondolewa...hapo ndipo watalazimika kufunga kama wenzao. Wakitaka ufunuo wa jambo fulani sasa itawapasa wafunge, wakitaka kutatua au kujua jambo fulani itawapasa wafunge kwanza na kuomba,Kwahiyo kile kitendo cha wao kutembea, kula, kuishi na kufundishwa na BWANA ndio kualikwa kwenyewe Harusini.

SWALI 2: SASA BWANA ALIMAANISHA NINI MSTARI WA MARKO 2:21-22? 21"Hakuna mtu ashonaye kiraka cha nguo mpya katika vazi kukuu; ikiwa ashona, kile kipya kilichotiwa huliharibu lile vazi kukuu,na pale palipotatuka huzidi. 22"Wala hakuna mtu atiaye divai mpya katika viriba vikukuu;ikiwa atia, ile divai mpya itavipasua viriba vile, divai ikamwagika, vile viriba vikaharibika. BALI HUTIA DIVAI MPYA KATIKA VIRIBA VIPYA.



JIBU: Mfano huo..unawalenga watu wanaojiita wakristo..Viriba ni vyombo maalumu vilivyokuwa vinatumika kuwekea divai wakati wa zamani, vilikuwa ninatengenezwa kwa ngozi, sasa nadhani utakuwa unafahamu pombe huwa inafura wakati inapoanza kukaribia kuchacha, na pombe zote ndivyo zilivyo, sasa, kwa wayahudi walikuwa wanatumia viriba vya ngozi ambayo bado ni mbichi, hivyo wakiweka divai ambayo bado inaendelea kuchachuka wakati ikiendelea kuvimba basi ile ngozi kwasababu bado ni laini, na mbichi, hutanuka pamoja na divai, kama vile kiatu cha ngozi, unaweza ukanunua mwanzoni kikakubana lakini baadaye kikakuenea vizuri ni kwasababu ni ngozi ambayo haijakakamaa haijawa ngumu bado...vivyo hivyo na kwa divai pia,..kwahiyo mfano ile pombe ikiwekwa kwenye kiriba ambacho kimeshakauka au kukaa sana inamaanisha kuwa ile ngozi itakuwa ishakuwa ngumu, kwahiyo ukiweka pombe changa mule ndani ni lazima kipasuke kwasababu ile pombe itavimba na kwa vile hakiwezi kutanuka mwisho wa siku kitapasuka tu...kwahiyo kiriba kipya, ni kwa divai mpya, huwezi kuweka divai mpya kwenye kiriba cha kale.

Hiyo inafunua tabia za wakristo wa leo, ambao roho zao zimegandishwa na mafundisho ya kale, wasiotaka kubadilika kwa kumruhusu Roho wa Mungu kutenda kazi ndani yao, hao ni sawa ni viriba vya kale visivyoweza kutanuka, Hivyo mfano ukija ufunuo wa kweli wa Roho Mtakatifu, ufunuo mpya mbele yao ambao hawajawahi kuusikia katika dini zao, au maisha yao, kwasababu ni viriba vya kale visivyotaka kutanuka basi vinapasuka..na ndio maana watu kama hao hawawezi kuupokea Ufunuo wa Roho wa Mungu hata kama ni kweli vipi au upo dhahiri kiasi gani, wanaishia kupinga tu kama mafarisayo kwasababu hawana uwezo wa kuchukuliana na ufunuo mpya wa Roho wa Mungu wao wataaishia kupinga tu, na kibakia katika dini zao, na ndivyo walivyokuwa mafarisayo na masadukayo wakati wa Bwana, Yeye alipowaletea kitu kipya hawakuweza kukipokea kwasababu roho zao zilikuwa zimegandishwa na mafundisho yao ya kale. Lakini wale wote waliokubali na kuilainisha mioyo yao kwa Bwana. Basi waliweza kuupokea ndio wale waliokuwa Mitume wa Bwana baadaye. Na ndio maana Bwana akawapa mifano hiyo....Hivyo ni vizuri kila siku kumruhusu Roho wa Mungu kututengeza kwa jinsi apendavyo ili kutambua ujumbe wa wakati tunaoishi...tusije tukawa tunaishi wakati wa ujumbe wa kanisa la kwanza wakati tupo katika kanisa la mwisho la Laodikia.

SWALI 3: Ndugu ninawaombeni msaada wenu mnieleewesheni ufunuo wa hivi vifungu? na unabii wake utatimia lini? Mathayo 24:29"Lakini mara, baada ya dhiki ya siku zile,jua litatiwa giza,na mwezi hautatoa mwangaza
wake,na nyota zitaanguka mbinguni,na nguvu za mbinguni zitatikisika;30"ndipo itakapoonekana ishara yake Mwana wa Adamu mbinguni; NDIPO MATAIFA(haya mataifa baada ya kumuona kwanini yaliomboleza? na baada ya kumuona yalikwenda na wapi?) YOTE YA ULIMWENGU* watakapoomboleza, nao watamwona Mwana wa Adamu akija juu ya mawingu ya mbinguni pamoja na nguvu na utukufu mwingi.31"Naye atawatuma "malaika" wake pamoja na SAUTI KUU YA PARAPANDA, NAO WATAWAKUSANYA WATEULE WAKE TOKA PEPO NNE,TOKA MWISHO HUU WA MBINGU MPAKA MWISHO HUU.

JIBU: Hiyo itakuwa ni mwisho kabisa, pale mataifa yote yatakapojikusanya katika vita ile kuu ya Har magedoni, wataomboleza kwasababu Bwana hatakuja kuwafariji, Bali Atakuja na  UPANGA kutoka kinywani mwake(ufunuo 19:11-16), watajutia maisha yao ya nyuma walioishi, watahuzunika pale watakapogundua kuwa wamedanganyika na huu ulimwengu, na dini za uwongo, na kamba za mpinga-kristo na kwamba KRISTO ndiye aliyekuwa njia pekee ya uzima na kwamba anakuja na hasira kali...Maana ukisoma pale kwenye ufunuo utaona anashuka akiwa amepanda farasi mweupe, ..sasa farasi anaashiria vita, hatakuja tena amepanda punda kama kile kipindi alichokuwa anaingia Yerusalemu kuashiria amani,..La! bali atakuja na upanga, kuteketeza mataifa yote, yaliyomkataa yeye, maelfu ya watu wataomboleza watakapogundua kuwa walikuwa wanapoteza muda maisha yao yote na kwamba hakuna tena maisha waliyoyazoelea, na wala hakuna nafasi ya pili,na Bwana ataleta utawala mpya wa Amani duniani...lakini watakaookoka ni wateule wachache sana watakaokuwa duniani wakati huo, ambao ni wayahudi na watu baadhi waliokuwa wanawasaidia wayahudi, tena ni wachache sana, hivyo, kutakuwa na maafa makubwa kutoka kwa Bwana sio kipindi cha kutamani kuwepo, na watu watu wote watamwona watakaokuwepo watamwona, na kuomboleza..

SWALI 4: Ufunuo 18:11"Nao wafanya biashara wa nchi walia na kuomboleza,kwasababu hapana mtu anunuaye bidhaa yao tena;..sasa hawa wafanya biashara waliolia kwa kuangamizwa kwa KANISA KATOLIKI NA MAKAO YAKE MAKUU VATIKANI kulingana na kile kitabu cha ufunuo 18 hii babeli ya kiroho inawasaidiaje sasa katika biashara zao ndugu? mpaka walie nakuomboleza? ebu nieleweni hapo ndugu?

JIBU: Hazina yote ya dunia leo hii inashikiliwa na Vatican,(fuatilia utajua hilo), ipo Vatican ambapo ndipo makao makuu ya kanisa katoliki utajiri wote upo kule, wala usifikirie ni Marekani, jaribu tu, kuangalia miradi mikubwa kama mahospitali, mashule, taasisi za kijamii, nk. zinafadhiliwa na kumilikiwa na nani?..au chunguza karibu kila kata utakuta kanisa kubwa la katoliki, chunguza hata hapo mahali unapoishi, utaona,na ndivyo ilivyo katika sehemu kubwa za dunia.. uchumi wote wa dunia unaongozwa na huo mfumo..Na sasa kanisa hilo linaongeza nguvu kuleta madhehebu yote pamoja na dini zote, kuiunda ile chapa ya mnyama, dini na serikali itakuwa ni kitu kimoja, Papa akisema ni sawa na serikali  imesema, itafika wakati kutakuwa hakuna kuuza wala kununua pasipo kuwa na utambulisho wa dhehebu fulani au dini iliyojiunga kwenye umoja huo wa dini na madhehebu.

Ubarikiwe sana.

Ukiwa na swali lolote lihusulo biblia ..tutumie  (kwa e-mail/whatsapp/namba za simu )na kwa neema za Bwana litajibiwa.

No comments:

Post a Comment