"Tazama, naja kama mwivi. Heri akeshaye, na kuyatunza mavazi yake, asiende uchi hata watu wakaione aibu yake...ufunuo 16:15"

Monday, October 22, 2018

UMEPATA UHAKIKA WA KUTOKUINGIA HUKUMUNI KATIKA SIKU ILE?

Jaribu kufikiria dikteta Adolf Hitler wa ujerumani Yule aliyesababisha vita ya pili ya dunia, na kuhusika kwa mauji ya mamilioni ya raia wasiokuwa na hatia ulimwenguni kote, mfano leo hii angekuwa hai, unadhani hatma ya maisha yake ingekuwa ni nini?, watu wa ulimwengu mzima wangetaka Yule mtu apewe adhabu gani?, Ni wazi kuwa kila mtu angetoa maoni ya adhabu yake ya kipekee ya mateso yasiyokuwa ya kawaida ambayo walau yangeweza kulipiza kisasi cha yale mabaya yote aliyowafanyia watu wasiokuwa na hatia, wale watu aliowachoma katika matarunu ya gesi na kuwaua kwa vifo vya kikatili na mateso na kusababisha vita ya pili ya dunia. Yeye naye angepewa adhabu mojawapo ya hizo watu wangeridhika kumuona analipa deni la alichokipanda.

Lakini pia jaribu kufikiria mfano amekamatwa na kwenda kuhifadhiwa mahali Fulani pa siri, kisha ukasikia baada ya siku chache kaachiwa huru, sasa ni raia wa kawaida kama raia mwingine ambaye hajafanya kosa lolote, na cha kushangaza zaidi sio tu kutokupewa adhabu yoyote bali hata MAHAKAMANI penyewe mahali ambapo ni pa haki hajapandishwa kushitakiwa. Badala yake kaachiwa yupo huru na anaendelea na maisha yake ya kawaida...

Kwa namna ya kawaida hilo ni jambo lisilokaa liwezekane, lakini kwa Mungu limewezekana..

Bwana Yesu anasema.. Yohana 5:24 "Amin, amin, nawaambia, Yeye alisikiaye neno langu na kumwamini yeye aliyenipeleka yuna uzima wa milele; WALA HAINGII HUKUMUNI, BALI AMEPITA KUTOKA MAUTINI KUINGIA UZIMANI".




Ndugu yangu mimi na wewe nafsi zetu zinatushuhudia kabisa sio wakamilifu kwa asilimia zote, na kama sio wakamilifu mbele za Mungu amri ni moja tu, ni lazima tukahukumiwe adhabu kwa kutokukamilika mbele zake, Na biblia ipo wazi juu ya hilo, Lakini ashukuruwe Kristo alisema amwaminiye yeye, yuna uzima wa milele, WALA HAINGII HUKUMUNI, BALI AMEPITA KUTOKA MAUTINI KUINGIA UZIMANI.

Ikiwa na maana kuwa siku ile Kristo atakaposimama kuyahukumu mataifa yote ulimwenguni katika kile kiti chake cheupe cha enzi wale wote waliomwamini yeye hawatakuwepo hapo, badala yake wao ndio watakaosimama na Kristo kuyahukumu mataifa yote.Tunasoma..
Ufunuo 20.11 "Kisha nikaona kiti cha enzi, kikubwa, cheupe, na yeye aketiye juu yake; ambaye nchi na mbingu zikakimbia uso wake, na mahali pao hapakuonekana. 12 Nikawaona wafu, wakubwa kwa wadogo, wamesimama mbele ya hicho kiti cha enzi; na vitabu vikafunguliwa; na kitabu kingine kikafunguliwa, ambacho ni cha uzima; na hao wafu wakahukumiwa katika mambo hayo yaliyoandikwa katika vile vitabu, sawasawa na matendo yao. 13 Bahari ikawatoa wafu waliokuwamo ndani yake; na Mauti na Kuzimu zikawatoa wafu waliokuwamo ndani yake. Wakahukumiwa kila mtu kwa kadiri ya matendo yake. 14 Mauti na Kuzimu zikatupwa katika lile ziwa la moto. Hii ndiyo mauti ya pili, yaani, hilo ziwa la moto. 15 Na iwapon mtu ye yote hakuonekana ameandikwa katika kitabu cha uzima, alitupwa katika lile ziwa la moto".

Unaona hapo? Leo hii wewe ni mlevi,mtazamaji wa pornography, mfanyaji wa mustarbation, msengenyaji, mwizi, mzinzi, maisha yako hayana matumaini, unaishi kwa hofu, kila siku unahisi kuhukumiwa ndani ya nafsi yako, kuwa njia unayoiendea ni ya mauti, na unafahamu kabisa kuwa hata ukifa leo utahukumiwa tu na kwenda katika ziwa la moto, kwanini unaendelea kuyahatarisha maisha yako, kwa kuishi maisha ya namna hiyo ya kutokujali?, kwanini unaipuuzia neema hii ya kipekee ya kuvukishwa toka mautini mpaka uzimani? Neema ya kutokuingizwa hukumuni? Bwana anasema NJOO! KWANGU unywe maji ukate hiyo kiu..Lakini bado upo vuguvugu, unadhani kwa matendo yako utaweza kusimama mbele zake siku ile? hii neema haitadumu milele..Ni neema ambayo mwanadamu yoyote asingestahili kupewa.

Ni maombi yangu, tusitamani KUSIMAMA MBELE YA KITI CHEUPE CHA HUKUMU CHA MUNGU siku ile kwasababu tukishajikuta tu tumesimama pale, habari yetu imekwisha hatutakuwa na cha kujitetea, kwa njia yoyote makosa ni lazima tu yaonekana ndani yetu. Na baada ya hapo ni safari ya moja kwa moja kwenda katika lile ziwa la moto.

Tuipishe hukumu ya Mungu hakuna anayependa kupandishwa mahakamu hata kwa katika mahakama za kibinadamu tu hakuna anayenda kufikishwa kule, itakuwaji siku ile kukutana uso kwa uso wa Mungu mwenyewe katika mahakama? Ni jambo la kutisha sana, tusitamani tuwepo.

Tubu sasa maadamu muda upo, salimisha maisha yako kwa Kristo leo, kesho haipo, kabatizwa katika ubatizo sahihi baada ya kuamini kwako kama haujafanya hivyo haraka iwezekanavyo ili upate ondoleo la dhambi zako, na ubatizo sahihi ni ule wa kuzamishwa kwenye maji mengi na uwe ni kwa jina la YESU KRISTO ubatizo mwingine nje ya huo ni batili, Kisha Bwana atakupa Roho wake mtakatifu na hapo utakuwa UMESHAZALIWA MARA YA PILI..Na kama hizo hatua hazijakamilika ndani yako, hapo bado hujazaliwa mara ya pili. Bado hujavuka toka mautini kwenda uzimani, bado hujaikwepa hukumu...


Fanya bidii kumtafuta YESU siku hizi ni za hatari.

Ubarikiwe sana.


Tafadhali “share” kwa wengine ujumbe huu, pia “LIKE” page hii uwe unapata machapisho mapya kila wakati.

Kwa mafundisho mengine mengi ya ziada tembelea website yetu >>> www.wingulamashahidi.org

No comments:

Post a Comment