"Tazama, naja kama mwivi. Heri akeshaye, na kuyatunza mavazi yake, asiende uchi hata watu wakaione aibu yake...ufunuo 16:15"

Monday, January 21, 2019

USHUHUDA WA RICKY:


Ushuhuda huu utakutoa sehemAu moja kiimani hadi nyingine.
 
Mwinjilisti mmoja wa kimarekani aAjulikanaye kama Rick Jonyer alikuwa akiomba kwa muda wa miaka 26 Mungu amnyakue mpaka mbingu ya tatu kama Bwana alivyofanya kwa mtume Paulo. Na siku moja ilipofika Mungu kusikia maombAi yake alimchukua katika maono mbinguni kama tunavyosoma katika kitabu chake alichokiandika kijulikanacho kama THE FINAL QUEST,Kilichopata umaarufu mkubwa sana  duniani kote. akieleza humo jinsi alivyoonyeshwa mambo mengi yahusuo hali za wakristo wa sasa kwa ujumla, Lakini hasa kwa wakati huu ningependa tujifunze kipengele kifupi cha maono hayo aliyoonyeshwa naamini  lipo jambo kubwa sana la kujifunza .
 

Rick anasema alipofika wakati wa kupitishwa na Bwana  mbele ya viti vya enzi vilivyopo mbinguni, aliona kiti kimoja kilichokuwa na utofauti kidogo, malaika wamekipamba na kukizunguka pande zote, na juu yake aliketi mfalme mkuu sana, na malaika walisimama pembeni yake wakisubiri maagizo kutoka kwake ya kufanya. Rick anasema alipokitazama kile kiti kwa ukaribu aliona sura ya mtu ambaye alishawahi kumwona mahali, ndipo alipomwomba Bwana amsogelee aongee naye naye alipofika alimwambia: naona kama  sura yako si ngeni machoni pangu, kama nilishawahi kukuona mahali ila sikumbuki ni wapi.


 Lakini yule mtu ambaye jina lake ni Angelo akamwambia ulishawahi kuniona katika maono wakati fulani zamani. Ndipo Rick haraka akajaribu kukumbuka ni wapi ndipo kumbukumbu zake zikamjua kuhusu tukio hilo akasema: siku moja alivyokuwa kijana alitoka ndani na kwenda kukaa nje ya nyuma mbali kidogo na anapoishi sehemu ya utulivu akimsubiria Bwana azungumze naye huku akiwa anasoma biblia yake, anasema maono  yalimjia saa ile ile na katika maono hayo aliona mtu mmoja mkristo mwenye bidii sana katika kumtumikia Mungu, alikuwa anashuhudia watu sehemu nyingi na kufundisha biblia mara kwa mara na kwenda kuwaombea wagonjwa kila mahali. Na muda huo huo akamwona na mtu mwingine tena aliyekuwa wa mtaani asiyekuwa na makazi ya kuishi anazurura tu huku na huko, ni mtu ambaye alikuwa hata akipita njia na kukutana na kitu chochote hata kitoto cha paka alikipiga kwa teke kitoke mbele yake.


Na ndipo Bwana akamuuliza , je kati ya hawa wawili ni yupi anayenipendeza zaidi?

Ni yule wa kwanza!: Rick akajibu kwa ujasiri wote.


Hapana! Ni wa pili. Ndipo Bwana akaanza kumweleza Rick habari zao wote wawili na maisha yao jinsi yalivyokuwa.


Yule wa kwanza alililewa katika familia nzuri, inayomjua sana Mungu na kumcha Mungu daima alililewa katika kanisa nzuri na hata alipata nafasi ya kwenda kujifunza masomo ya biblia katika vyuo. Alipewa asilimia 100 ya neema yangu lakini yeye aliweza kutumia asilimia 75 tu ya neema hiyo.


Lakini yule wa pili alizaliwa kiziwi, alikuwa ni mtu wa kunyanyapaliwa na hivyo alitelekezwa kwenye nyumba za kale sehemu za baridi mpaka siku alipokuja kukutwa na serikali ya nchi yao na kupelekwa katika vituo vya watu wasiojiweza, alihamishwa kituo kimoja hadi kingine, kutokana na kunyanyapaliwa na watu, lakini haikusaidia  mpaka alipojikuta tena yupo mitaani alipokuwepo mwanzo. Hivyo Mungu akamuhurumia na kumpa sehemu tatu za neema yake, lakini alizishinda zote aliacha kuwapiga mapaka barabarani.. 


Pindi Bwana alipokuwa akisema nami niligeuka kumtazama tena huyo mfalme mkuu jinsi alivyoketi kwenye enzi kuu namna ile, mwenye utukufu mwingi kushinda hata wa Sulemani, malaika wamemzunguka kila mahali wakisubiria maagizo kutoka kwake. Ndipo nilipomgeukia tena Bwana na kumsihi BWANA azidi kunielezea juu ya habari ya huyu mtu.


Bwana akasema Angelo alikuwa mwaminifu kwa kila neema niliyompa, Nilimwongezea sehemu nyingine tatu za neema yangu na zote akazitenda kiuaminifu. Akaacha kuiba, hata wakati alipopitia katika mazingira magumu nusu ya kufa kwa njaa lakini hakutaka kuiba mali ambayo haikuwa ya kwake kwa ajili ya kwenda kujishibisha. Alijinunulia chakula chake kwa pesa yake mwenyewe aliyoipata katika kukusanya makopo barabarani  aliyoyauza. Na mara chache  akipata kazi za kusafisha uani katika majimba ya watu.


Angelo alikuwa ni kiziwi lakini alijifunza kusoma. Hivyo nilimpelekea nakala za vipeperushi cha Injili. Na Alipovisoma  Roho wangu alimfungua macho yake na ndipo akayakabidhi maisha  yake kwangu. Nikamwongozea tena sehemu ya neema yangu, na zote hizo alizitumia kuaminifu. Alitamani sana kushuhudia habari zangu kwa watu wengine lakini hakuweza kuongea, lakini japo kuwa alikuwa katika hali ile hakutana habari zangu zisiwafikie wengine.  Alianza kutumia zaidi ya nusu ya alichokipata kusambaza kipeperushi vya injili mabarabarani.


Ndipo nikamuuliza Bwana, Ni watu wangapi aliowavuta kwako?, ni wazi itakuwa maelfu ya watu, mpaka ifikie hatua ya kuketi katika viti vya wafalme ni lazima atakuwa amewavuta wengi.

Lakini Bwana akamwambia: Alifanikiwa kumvuta mtu mmoja tu kwangu. Nilifanya hivyo Ili kumtia moyo alimvuta mlevi mmoja aliyekuwa anakaribia kufa barabarani. Na hiyo ilimtia moyo sana kiasi cha kumfanya aweze kuendelea kukaa  miaka mingi zaidi barabarani kujaribu kumvuta mtu mwingine kwangu. Lakini mbingu nzima ilikuwa inamfurahia kutaka aje huku juu, nami pia nilitamani aje apokee ujira wake. Huyo ni Angelo.


Lakini ni kitu gani kilimfanya Angelo aweze kuwa mfalme hapa? Niliuliza.


Alikuwa mwaminifu kwa vyote alivyopewa aliyashinda yote mpaka alipokuwa kama mimi, yaani KUFA KWA AJILI YA IMANI.


Lakini je! yeye naye alishindaje shindaje, na alikufaje kufaje kwa ajili ya Imani? Niliuliza tena.

Aliushinda ulimwengu kwa UPENDO wangu. Wachache sana wanaweza kushinda wakiwa na vichache. Watu wangu wengi wanaishi katika mazingira mazuri zaidi hata ya wafalme walioishi karne moja iliyopita lakini bado hawana shukrani kwa hayo.Lakini Angelo yeye hakuwa hivyo, yeye aliweza hata kushukuru kwa boksi aliloliokota barabarani na kuligeuza hilo kuwa hata sehemu yake ya kufanyia ibada. Alianza kupenda kila kitu alichokiona na kila mtu,aliweza kupenda hata tunda la tofaa zaidi hata ya watu wanavyoweza kufurahia sherehe kubwa wazifanyapo. Alikuwa mwaminifu kwa kila nilichompa japokuwa nilichompa hakikuwa kikubwa kulinganisha na wengine lakini yeye alikuwa mwaminifu katika hivyo.


Nilikuonyesha maono juu yake wakati ule, kwasababu ulishampita mara nyingi barabarani.

Ndipo nilipotaka kufahamu nilifanya nini nilipomuona.


Bwana akasema ulimnyooshea  kidole chako na kumwambia rafiki yako, kuwa watu kama hao wanaosimama kwenye vituo vya mabasi ni watu waliotumwa na shetani kuuvuruga ukristo, watu waliopoteza mweleko wa imani.


Niliposikia hivyo nilijisikia mnyonge na mwenye aibu nyingi, ndipo nikamwomba Bwana anisamehe akasema umeshasamehewa.


Bwana akaendelea kusema, alikuwa na mengi ya kuwapa watu wangu lakini hawakupenda kumsogelea. Alikuwa mwaminifu kwa alichokipata  alinunua biblia yake, na baadhi ya vitabu kusoma lakini alipojaribu kwenda katika makanisa hakuna mtu aliyempokea. Kama wangempokea basi wangekuwa wamenipokea mimi. 


Ndipo nilipozidi kutaka kufahamu Angelo alikufaje kufaje?


Bwana akasema: Aliganda katika baridi kujaribu kumwokoa mlevi mmoja barabarani.

Ndipo nipomuliza Bwana najua anastahili kuwepo hapa lakini je! si ni wale watu wanaokufa kwa ajili ya injili yako ndio wanaohesabika kuwa ni mashahidi wako waaminifu. Inakuwaje kwa huyu?

Angelo alikuwa anakufa kwa ajili yangu kila siku, aliweza kuwa tayari kuutoa uhai wake kwa ajili ya mtu mwenye uhitaji. Kama Mtume Paulo alivyosema, hata nikiutoa mwili wangu wote uungue na moto kama sina upendo mimi si kitu, lakini kama utautao uhai wako katika upendo hiyo inahesabika sana mbele za Mungu. Angelo alikuwa anakufa kila siku kwasababu alikuwa haishi kwa ajili yake, bali kwa ajili ya wengine. Japokuwa alikuwa anajiona mwenyewe kuwa ni mdogo katikati ya watakatifu lakini kiuhalisia alikuwa ni mkubwa sana. Wale watu wanaojiona kuwa ni wakubwa na kusifiwa na watu wengi wao wanaishia kuwa wadogo huku.


Mwisho wa nukuu.


*******

Ndugu watu wengi wanadhani ili ukubaliwe na Mungu na kupata nafasi ya kumkaribia ni mpaka ufanane na mwinjilisti fulani au nabii fulani, au mwalimu fulani. Lakini hawajui kuwa kila mtu kapewa kipimo chake cha imani. Na kule kinachohesabika ni je umekutumiaje hicho ulichopewa?. Mwanafunzi mmoja anaweza kupewa maswali 10 na kati ya hayo akapata 9 na kukosa 1..Wakati huo huo mwanafunzi mwingine anaweza kupewa maswali 100, akapata 60 na kukosa 40, kwa namna ya kawaida unaweza kusema yule wa maswali 100 ndiye aliyefaulu zaidi ya mwingine, lakini tukirudi kwenye asilimia utagundua kuwa yule aliyepewa maswali 10, ndiye aliyefaulu zaidi ya mwenzake, amefaulu kwa asilimia 90%..Ukilinganisha na yule wa maswali 100 yeye kafaulu kwa asilimia 60%. Ambayo ni ndogo.


Kama aliweza kuwa mwaminifu katika maswali 10 basi atakuwa mwaminifu katika maswali 100, ndivyo ilivyo na kwetu sisi, kila mmoja kapimiwa kipimo chake. Swali je! kipimo chako unakitumiaje?. Umehubiriwa injili mara ngapi ugeuke lakini hutaki?, umehudhuria ibada ngapi lakini bado unaipuuzia neema. Umesikia shuhuda ngapi ubadilike lakini bado upo vile vile,? Unaona ni shida kutenda kazi unachofundishwa kila siku. Siku ile utakuwa wapi?, utawezaje kusimama na yule kipofu aliyekule vijijini yeye aliposikia tu Neno hata bila kuona akaamini na kubatizwa. Lakini wewe unajiona kwasasa hivyo vitu havina umuhimu, Bwana atakapotoa thawabu kwa wale waliomtii utakuwa wapi?. Yeye mwenyewe alisema maneno haya.


Luka 16:10 “Aliye mwaminifu katika lililo dogo sana, huwa mwaminifu katika lililo kubwa pia; na aliye dhalimu katika lililo dogo, huwa dhalimu katika lililo kubwa pia.”

Nakutia moyo wewe uliyechukua uamuzi wa kumfuata Bwana katika hali zote, kwa moyo wako wote. Wakati wa faraja utakuja na Bwana atakulipa kulingana na uaminifu wako.


Mungu akubariki sana. Tafadhali “share” ujumbe huu kwa wengine.

No comments:

Post a Comment