"Tazama, naja kama mwivi. Heri akeshaye, na kuyatunza mavazi yake, asiende uchi hata watu wakaione aibu yake...ufunuo 16:15"

Monday, October 16, 2017

TOKENI KWAKE, ENYI WATU WANGU: Part 1


Majina ya makufuru na Kanisa Katoliki:

Wakati mikesha ya Pasaka inadhaniwa kuwa ni siku muhimu ya kukumbuka ushindi tulioupata  kwa njia ya BWANA wetu YESU KRISTO pale Kalvari, wengine wanaitumia kuwakosesha watu  wadhaifu wa imani na cha ajabu na kusikitisha zaidi shetani amenyanyua viongozi hawa wanaojiita ni wa dini ili kuwapotosha watu wasiomjua Mungu na sio tu kupotosha bali  na  kulikufuru Jina la Mungu mwenyezi (YESU KRISTO). Si ajabu biblia imewataja katika


   2Wakoritho 11:13" Maana watu kama hao ni mitume wa uongo, watendao kazi kwa hila, wanaojigeuza wawe mfano wa mitume wa Kristo.
14 Wala si ajabu. Maana Shetani mwenyewe hujigeuza awe mfano wa malaika wa nuru.
15 Basi si neno kubwa watumishi wake nao wakijigeuza wawe mfano wa watumishi wa haki, ambao mwisho wao utakuwa sawasawa na kazi zao. "

Kanisa Katoliki limekuwa na SALA maalumu inayosomwa  kila "EASTER" (Mkesha wa Pasaka), inayohudhuriwa na viongozi wote wa kanisa hilo ikiwemo PAPA, Hii Ni MISA maalumu inayoandaliwa kwa kusudi maalumu la kumtukuza "SHETANI/LUCIFER" na kumkufuru Bwana wetu YESU KRISTO.

Misa hii haifanyiki kwa siri, ni jambo lililowazi la kila mtu kuona, sala hiyo huwa inaimbwa katika lugha ya kilatini, tazama video chini ujionee na hii ndiyo tafsiri ya maneno yake:


" Lucifer uangazaye nuru yako kwa wanadamu 
..O Lucifer usiyeweza kushindwa.
..KRISTO NI MWANA WAKO
..Aliyepanda kutoka kuzimu
         ..Aliyeangaza nuru yake ya amani, na anaishi na anatawala
..Ulimwengu pasipo mwisho."





Unaweza ukajionea mwenyewe jinsi sala hiyo inavyomtaja shetani/Lucifer kuwa ni MUNGU na YESU KRISTO ni mwana wake. Hivyo baba wa Yesu ni shetani..JE! HAYA SI MAKUFURU?..
Ufunuo 18:4 inasema "...... TOKENI KWAKE, ENYI WATU WANGU!, msishiriki dhambi zake, wala msipokee mapigo yake.Kwa maana dhambi zake zimefika hata mbinguni, na Mungu amekumbuka maovu yake. "

Ndugu ikiwa unampenda Bwana hautashiriki uovu huo wa mwokozi wako kuitwa mwana wa shetani,na kwamba shetani ni Mungu, ikimbie dini hii ya uongo na inayowapeleka wengi kuzimu wakidhani wanamwabudu Mungu kumbe ni ibilisi. Iokoe roho yako toka katika mifumo ya dini na madhehebu mwangalie Bwana Yesu maana yeye ndiye njia, kweli na uzima mtu hatofika kwa BABA Isipokuwa kwa njia yake yeye tu!

Amina.

No comments:

Post a Comment